Machinga wa Mwanza mmepoa sana, si Makoroboi wala Langolango. Njooni Dar mjifunze amsha amsha

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Business is not for everyone.
Wafanyabiashara machinga wa makoroboi na langolango mmepoa sana, soko zima husikii kelele za kuita wateja wala zile spika za amsha amsha.

Utadhani uko supermarket, hata supermarket kuna music laini hupigwa.

Hakuna kubembeleza wala kumshawishi mteja, hakuna kusema karibu, unataka utanunua hutaki nenda.

Hali ni tofauti kwa wenzao wa Karume na mitaa ya Kariakoo. Kama ni mgeni utarudi kwenu na mawenge ya kelele usiku kucha.

Mmepoa, mmepoa.
 
ilibidi uwaibie kidogo uone amsha amsha itakuepo au watakimbiza mwizi kimya kimya
 
ushamba wenu wa makelele msiupeleke sehemu nyengine!
 
Mkuu vp hijab zilikuwepo za kutosha? Maana nasikia garden za Tanga Zina maua mazuri ya kupanda nyumbani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…