Machinga warudi mikoani wakalime,kilimo hiki kinalipa

Machinga warudi mikoani wakalime,kilimo hiki kinalipa

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Nimewasikia wafanyabiashara wa kariakoo wakipendekeza serikali iwarejeshe machinga vijijini wakalime. Nimewasikia wanasiasa wakiunga mkono hoja hii wakidai endapo vijana watajiajiri kwenye kilimo maisha yatakuwa mazuri kwao na familia zao.

Niliposikia kauli hizi nikajiuliza machinga ni wakina nani?Katika kutafuta majibu nikaelekeza fikra kwenye malango ya machangi kuingia kazini kwao. Lango la Kwanza nililoangazia ni kariakoo, hapa ntatoa mfano mmoja tu ambao mliopo Dar es salaam mnaweza Leo au kesho mkatuwekea hapa uthibitisho.

Damka asubuhi saa kumi na mbili nenda kituo Cha treni,dalafala na mwendokasi Cha gerezani. Angalia idadi ya vijana wanaoletwa mjini kutokea Mbagala, Gongo la Mboto na mbezi, Hawa ndio wanachinga. Ukiangalia wengi wao wana familia na Wana watoto wadogo. Tunaambiwa kirahisi kabisa na viongozi wa wanachinga na viongozi wa kisiasa kwamba Hawa watu Ni kero mjini hivyo wafanyiwe figisu warejee kijijini. Naamini viongozi na watu wanaowaza namna hii Wana matatizo ya akili.

Kundi hili linakwenda kuhatarisha usalama wa Raia mtaani, wanakwenda kuanzisha panya road na mkiwakamata mtaambiwa ninyi ndio mmewafukuza kwenye vipato vyao.

Nimuulize RC na timu yake, Hawa wanachinga waliwekwa barabarani na JPM na Hadi siku anafungua kituo chake Cha Mbezi tulimsikia akiwaita wakafanye biashara ndani ya kituo na wasibughudhiwe. Leo nani anaweza kutuonyesha kariakoo machinga wamehamishiw wapi? Mbezi Luis wametengewa eneo wapi? Gongo la Mboto na Chanika wapi pametengwa? Tegeta, boko na bunju je? Mbagala, Tandika na temeke? Huku kote hakuna maeneo wakauze Nini?

Lakini pia Jambo lakushangaza nikusikia Rukwa nao wanapambana na Machinga, Kigoma, Tabora, Mtwara, Lindi, Tanga, Shinyanga na Mikoa Kama hii nayo wanapambana na Machinga. Are we serious? Kwamba huku nako Kuna machinga? Kwamba Wakuu wa wilaya nje ya Dar na Mwanaza pamoja wakuu wa Mikoa nao Wana agenda ya machinga? Nadhani wakuu wa Mikoa mingine fanyeni kazi acheni kusumbua raia, Tabora tuseme wamekwama Hadi Rais? Rukwa? Moshi?

Badala ya machinga kurudi vijijini wanarudi mitaani na hapo ndipo mtajifunza Nini wafanyakazi, mkiibiwa mtajua kwanini ajira ni muhimu.
 
Mkuu,wewe binafsi ukiachishwa hicho unachokifanya sasa hivi unaweza kuwa mwizi?kuwa mwizi/kibaka ni Tabia wala haichagizwi na ugumu wa maisha..Acha kupotosha na kututisha kuhusu uhalifu Machinga ni wafanyabiashara wanaokwepa kulipa Kodi full stop.
 
Siyo machinga tu wana CCM wote warudi wakalime hamna lolote wanalolifanyia taifa
 
Kingelipa usingekuwa mjini,kwani we utaki pesa
 
Maxhinga ni wafanyabiashara wanaokwepa kodi kwa makusudi. Wakifukuzwa mitaroni na mbele ya maduka asilimia 80%,wataenda tafuta fremu ili wakodi wauze bishara zao
 
Nimewasikia wafanyabiashara wa kariakoo wakipendekeza serikali iwarejeshe machinga vijijini wakalime. Nimewasikia wanasiasa wakiunga mkono hoja hii wakidai endapo vijana watajiajiri kwenye kilimo maisha yatakuwa mazuri kwao na familia zao.

Niliposikia kauli hizi nikajiuliza machinga ni wakina nani?Katika kutafuta majibu nikaelekeza fikra kwenye malango ya machangi kuingia kazini kwao. Lango la Kwanza nililoangazia ni kariakoo, hapa ntatoa mfano mmoja tu ambao mliopo Dar es salaam mnaweza Leo au kesho mkatuwekea hapa uthibitisho.

Damka asubuhi saa kumi na mbili nenda kituo Cha treni,dalafala na mwendokasi Cha gerezani. Angalia idadi ya vijana wanaoletwa mjini kutokea Mbagala, Gongo la Mboto na mbezi, Hawa ndio wanachinga. Ukiangalia wengi wao wana familia na Wana watoto wadogo. Tunaambiwa kirahisi kabisa na viongozi wa wanachinga na viongozi wa kisiasa kwamba Hawa watu Ni kero mjini hivyo wafanyiwe figisu warejee kijijini. Naamini viongozi na watu wanaowaza namna hii Wana matatizo ya akili.

Kundi hili linakwenda kuhatarisha usalama wa Raia mtaani, wanakwenda kuanzisha panya road na mkiwakamata mtaambiwa ninyi ndio mmewafukuza kwenye vipato vyao.

Nimuulize RC na timu yake, Hawa wanachinga waliwekwa barabarani na JPM na Hadi siku anafungua kituo chake Cha Mbezi tulimsikia akiwaita wakafanye biashara ndani ya kituo na wasibughudhiwe. Leo nani anaweza kutuonyesha kariakoo machinga wamehamishiw wapi? Mbezi Luis wametengewa eneo wapi? Gongo la Mboto na Chanika wapi pametengwa? Tegeta, boko na bunju je? Mbagala, Tandika na temeke? Huku kote hakuna maeneo wakauze Nini?

Lakini pia Jambo lakushangaza nikusikia Rukwa nao wanapambana na Machinga, Kigoma, Tabora, Mtwara, Lindi, Tanga, Shinyanga na Mikoa Kama hii nayo wanapambana na Machinga. Are we serious? Kwamba huku nako Kuna machinga? Kwamba Wakuu wa wilaya nje ya Dar na Mwanaza pamoja wakuu wa Mikoa nao Wana agenda ya machinga? Nadhani wakuu wa Mikoa mingine fanyeni kazi acheni kusumbua raia, Tabora tuseme wamekwama Hadi Rais? Rukwa? Moshi?

Badala ya machinga kurudi vijijini wanarudi mitaani na hapo ndipo mtajifunza Nini wafanyakazi, mkiibiwa mtajua kwanini ajira ni muhimu.

naomba ni kukatishe uzi wako kwa mchango wako.

watu wengi tunakimbilia sehemu ambazo fursa zake zimekuwa juu kimitaji,maisha,kuwa wengi.

swala hili kama uliweza kulisoma hawa unao wasema ni vijana kutoka mikoani ambako serikali ijataka kuwekeza ili mtu kujifikiria kuja mjini au mijini.

miji kuwa na kila kitu kama viwanda,vyuo na maofisi .
yani utashangaa ofisi ya misitu hipo mjini na afisa mkuu wa misitu yupo dar au mwanza.

kuna vitengo na kazi ambazo lazima kulazimisha maeneo.
kama vitengo vya uhamiaji vingekuwa na sehemu kubwa kwenye mipaka ndio sehemu kubwa ya wahamiaji kuliko kujazana airport tena ikiwa mjini.

viwanda vyenye kuzalisha bizaa fulani,maeneo ambayo mikoa kuwa washika mkia wa mapato.

ni mengi
 
Back
Top Bottom