Machinga wavamia eneo la Kanisa Dar es Salaam

Machinga wavamia eneo la Kanisa Dar es Salaam

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
13 November 2021
MACHINGA WAVAMIA ENEO LA KANISA BAADA YA KUHAMISHWA, TAHARUKI KUBWA YAIBUKA



Mgogoro mkubwa umeibuka kati ya Kanisa la Orthodox lililopo Mbuyuni, Salasala jijini Dar es Salaam na wafanyabiashara ndogondogo wa eneo hilo maarufu kama wamachinga, ambapo uongozi wa kanisa hilo unadai kwamba eneo lao limevamiwa na wafanyabiashara hao na kujenga vibanda kiasi cha kusababisha washindwe kufanya ibada. Global TV imefika eneo la tukio nakuzungumza na pande zote mbili, ambapo upande wa wafanyabiashara hao, wanadai kwamba hilo ni eneo la wazi na kwamba hawajavamia eneo la kanisa, kauli ambazo zimeungwa mkono na viongozi wa serikali ya mtaa.

Source : Global TV online


Toka maktaba :

24 October 2021


MAKAMU wa RAIS DKT PHILIP MPANGO AKUTANA na BABA MTAKATIFU wa ORTHODOX AFRICA....



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango leo Oktoba 24,2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Baba Mtakatifu Beatitude Theodoros II (The Pope and Patriarch of Alexandria and all Africa)Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Greek Orthodox Ikulu Jijini Dar es salaam. Makamu wa Rais amesema Tanzania imefurahishwa na ujio wa Baba Mtakatifu huyo na kumuomba kuendelea kuiweka nchi ya Tanzania katika maombi yake ya kila siku. Amesema tangu kupata uhuru Tanzania imekua kitovu cha Amani na kuendelea kuheshimu umuhimu wa dini zote kupitia ibara ya 19 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha amesema viongozi wa dini nchini Tanzania wamekua ndio msingi wa Amani iliopo nchini. Makamu wa Rais ameongeza kwamba Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inatambua mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za dini hapa nchini kwa kushirikiana vema na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo husasani katika sekta za elimu na afya hasa katika maeneo ya pembezoni ya nchi. Ametaja mchango wa kanisa la Orthodox nchini ambao ni pamoja na ujenzi Kliniki 90 pamoja na Hospitali katika mkoa wa kagera na shule katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Source : Global TV online
 
Machinga walifikili Chadema peke yao ndiyo wataisoma namba,

Eti eneo la wazi,Kama eneo Ni la wazi ilitakuwa wapewe na Serikali sikivu,
Machinga inatakiwa wafukuzwe kwenye eneo Hilo kwa mabomu,

Serikali iendelee kuwapiga wamachinga kwenye mshono labda akili zitawaijia siku zijazo.
 
Cairo, Egypt

Theodors II (Pope and Patriarch of Alexandria and All Africa)



Source : Academy for Cultural Diplomacy
 

Egypt's President al-Sissi makes historic Christmas visit to Coptic church in Cairo



Egypt's President Abdul Fattah al-Sisi visited a Coptic Christmas mass on Tuesday making him the first Egyptian leader to do so since ==President Nasser.== Egypt with 8 million of it citizens who are coptics..
 

Moscow, Russia

Putin Gets Blessed By Head Of Russian Orthodox Church Kirill After Presidential Inauguration




Patriarch Kirill, the head of the Russian Orthodox Church, has blessed newly sworn-in President Vladimir Putin in the 15th-century Annunciation Cathedral. The Patriarch performed a prayer service at the cathedral, considered the jewel of Russian architecture. One of the greatest medieval churches in the Russian capital, it once served as a private church of the Muscovite monarchs. After the prayer, the patriarch addressed the head of state on behalf of all clergy and believers, saying that all of these people supported Putin because they see him as “a leader who, apart from successfully managing the country, is also a person devoted to his motherland.”

Source : Rossiya 24
 
Wakaazi wengi wa Dar es Salaam hukurupuka bila kwanza kujua historia, wanafikiri kuwa dhehebu la Orthodox ni kama "kanisa" la Mlima wa Moto au la Gwajima.

Tupende kujiuliza maswali, kusoma historia na pia kuheshimu watu wengine wawe wa "kanisa la Gwajima au la Mlima wa Moto au dhehebu la imani yoyote ile na kuacha kusema Magufuli alituachia tufanye vyoyote vile.
 
Tusipobadilisha sera za uchumi kuondokana na umachinga uliokithiri huko mbele ni giza nene sana.
 
machinga ni watu wenye uwezo mdogo sana wa kuchakata maamuzi yanayotokana na kauli za wanasiasa.

tuliwaambia kuwa yule marehemu alikuwa anawatumia tu ili kutengeneza jeshi ambalo siku za usoni angekuja kulitumia katika harakati zake za kuwa rais wa maisha wa tanzania. wakatubishia na kutusimanga.

wakatuambia hapana, jamaa anatupenda sana, ana mapenzi ya dhati na sisi ndio maana katuruhusu tufanye biashara kiholela hadi kwenye maeneo ambayo siyo rasmi.

nasema hivi, Mama na watendaji wako kazieni hapohapo. wanyosheni mpaka watoke damu.
 
13 November 2021
MACHINGA WAVAMIA ENEO LA KANISA BAADA YA KUHAMISHWA, TAHARUKI KUBWA YAIBUKA



Mgogoro mkubwa umeibuka kati ya Kanisa la Orthodox lililopo Mbuyuni, Salasala jijini Dar es Salaam na wafanyabiashara ndogondogo wa eneo hilo maarufu kama wamachinga, ambapo uongozi wa kanisa hilo unadai kwamba eneo lao limevamiwa na wafanyabiashara hao na kujenga vibanda kiasi cha kusababisha washindwe kufanya ibada. Global TV imefika eneo la tukio nakuzungumza na pande zote mbili, ambapo upande wa wafanyabiashara hao, wanadai kwamba hilo ni eneo la wazi na kwamba hawajavamia eneo la kanisa, kauli ambazo zimeungwa mkono na viongozi wa serikali ya mtaa.

Source : Global TV online


Toka maktaba :

24 October 2021


MAKAMU wa RAIS DKT PHILIP MPANGO AKUTANA na BABA MTAKATIFU wa ORTHODOX AFRICA....



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango leo Oktoba 24,2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Baba Mtakatifu Beatitude Theodoros II (The Pope and Patriarch of Alexandria and all Africa)Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Greek Orthodox Ikulu Jijini Dar es salaam. Makamu wa Rais amesema Tanzania imefurahishwa na ujio wa Baba Mtakatifu huyo na kumuomba kuendelea kuiweka nchi ya Tanzania katika maombi yake ya kila siku. Amesema tangu kupata uhuru Tanzania imekua kitovu cha Amani na kuendelea kuheshimu umuhimu wa dini zote kupitia ibara ya 19 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha amesema viongozi wa dini nchini Tanzania wamekua ndio msingi wa Amani iliopo nchini. Makamu wa Rais ameongeza kwamba Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inatambua mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za dini hapa nchini kwa kushirikiana vema na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo husasani katika sekta za elimu na afya hasa katika maeneo ya pembezoni ya nchi. Ametaja mchango wa kanisa la Orthodox nchini ambao ni pamoja na ujenzi Kliniki 90 pamoja na Hospitali katika mkoa wa kagera na shule katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Source : Global TV online
Ndugu yangu pole kwa kulishwa matango pori na Global TV. Hilo kanisa halijawahi kuwa na ibada zinafanyika hapo.

Siku Moja tangu wamachinga kuanza kujenga vibanda vyao kwenye hilo eneo la wazi uongozi wa kanisa ulionekana kuwa hai na kuanza kuchapia uzio unaolizinguka kanisa hilo na jana usiku wa saa nane ndipo uongozi huo ulipotafuta watu wa kuvunja vibanda vyao na kuharibu Mali zako.

Kinachosemekana ni kwamba Kanisa hilo lina mgogoro na serikali.

My take
Waandishi chipukizi wa habari wanatakiwa wafundwe upya namna ya upashaji habari vinginevyo wanazidi kuharibu balada ya kutengeneza
 
Ndugu yangu pole kwa kulishwa matango pori na Global TV. Hilo kanisa halijawahi kuwa na ibada zinafanyika hapo.

Siku Moja tangu wamachinga kuanza kujenga vibanda vyao kwenye hilo eneo la wazi uongozi wa kanisa ulionekana kuwa hai na kuanza kuchapia uzio unaolizinguka kanisa hilo na jana usiku wa saa nane ndipo uongozi huo ulipotafuta watu wa kuvunja vibanda vyao na kuharibu Mali zako.

Kinachosemekana ni kwamba Kanisa hilo lina mgogoro na serikali.

My take
Waandishi chipukizi wa habari wanatakiwa wafundwe upya namna ya upashaji habari vinginevyo wanazidi kuharibu balada ya kutengeneza

Twende mbele zaidi tuache hiyo nadharia ya 'kutosali', je taasisi ya kidini haiwezi kumiliki eneo kwa ajili ya shughuli za kusali au kiuchumi na kijamii kwa siku za mbele.

TOKA MAKTABA :

29 Oct 2018
BREAKING: Waislamu wavamia ofisi ya DC Hai, tunataka haki!!



Waislamu wa Misikiti ya kata tatu tofauti katika Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Wameandamana kuelekea katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya Ya Hai, Lengai ole Sabaya, kupeleka mashtaka yao ya kuporwa shule walioyoijenga kwa michango yao.
 
Tusipobadilisha sera za uchumi kuondokana na umachinga uliokithiri huko mbele ni giza nene sana.
Ni kweli, maana hilo sio soko, hicho ni kiwanja, cha kujiuliza je eneo la soko halipo huo mtaa? Kama halipo waombe eneo la soko lenye huduma zote muhimu kama Raisi alivyosema siyo watu kujuamulia kukaa kwenye viwanja hovyo hovyo hata kama ni eneo la serikali bado kama siyo soko haitakiwi kujenga mabanda, kingine serikali inatakiwa kuweka marufuku ya ujenzi wa mabanda maana ni rahisi kushika moto, wajengewe vizimba vya cement sokoni, kikubwa naona watu wengi wameamuka kufanya biashara za sokoni basi serikali ijenge masoko mengi biashara zifanyike huko.
 
13 November 2021
MACHINGA WAVAMIA ENEO LA KANISA BAADA YA KUHAMISHWA, TAHARUKI KUBWA YAIBUKA



Mgogoro mkubwa umeibuka kati ya Kanisa la Orthodox lililopo Mbuyuni, Salasala jijini Dar es Salaam na wafanyabiashara ndogondogo wa eneo hilo maarufu kama wamachinga, ambapo uongozi wa kanisa hilo unadai kwamba eneo lao limevamiwa na wafanyabiashara hao na kujenga vibanda kiasi cha kusababisha washindwe kufanya ibada. Global TV imefika eneo la tukio nakuzungumza na pande zote mbili, ambapo upande wa wafanyabiashara hao, wanadai kwamba hilo ni eneo la wazi na kwamba hawajavamia eneo la kanisa, kauli ambazo zimeungwa mkono na viongozi wa serikali ya mtaa.

Source : Global TV online


Toka maktaba :

24 October 2021


MAKAMU wa RAIS DKT PHILIP MPANGO AKUTANA na BABA MTAKATIFU wa ORTHODOX AFRICA....



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango leo Oktoba 24,2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Baba Mtakatifu Beatitude Theodoros II (The Pope and Patriarch of Alexandria and all Africa)Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Greek Orthodox Ikulu Jijini Dar es salaam. Makamu wa Rais amesema Tanzania imefurahishwa na ujio wa Baba Mtakatifu huyo na kumuomba kuendelea kuiweka nchi ya Tanzania katika maombi yake ya kila siku. Amesema tangu kupata uhuru Tanzania imekua kitovu cha Amani na kuendelea kuheshimu umuhimu wa dini zote kupitia ibara ya 19 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha amesema viongozi wa dini nchini Tanzania wamekua ndio msingi wa Amani iliopo nchini. Makamu wa Rais ameongeza kwamba Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inatambua mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za dini hapa nchini kwa kushirikiana vema na serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo husasani katika sekta za elimu na afya hasa katika maeneo ya pembezoni ya nchi. Ametaja mchango wa kanisa la Orthodox nchini ambao ni pamoja na ujenzi Kliniki 90 pamoja na Hospitali katika mkoa wa kagera na shule katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Source : Global TV online

hao machinga ccm si walisema tuko uchumi wa kati? sasa iweje kuvamia maeneo ya watu?
 
Unaweza kukuta kuwa Kanisa halina hati kwa sababu walijua kuwa kila mtu anajua hilo eneo ni la kwao. Kama waliwahi kuwa na hati ni kiasi cha kwenda Ardhi kufanya search ili wapewe nakala. Mpaka ukipatikana wajenge uzio haraharaka. Huu mgogoro ni wa Afisa Ardhi wala sio wa Afisa Biashara au diwani. Na huyo anaewadharau wenye rangi kama yake ana matatizo.

Amandla...
 
Back
Top Bottom