Machungwa ya Muheza Yaua

Machungwa ya Muheza Yaua

Filipo Lubua

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2011
Posts
339
Reaction score
578
Ni machungwa ya Muheza, yenye sifa kemkem
Yamejaa kila muji, hakuna asoyajua
Yanauzwa bei chee, na fukara anamudu
Ni machungwa tamanika, bali ndani yameoza

Yanazidi ya handeni, yamenea nchi nzima
Sio Dar na Arusha, hata Mwanza yashafika
Yauzwa barabarani, wa malori ni wateja
Ni machungwa tamanika, bali ndani yameoza

Hayauzwi mchanani, usiku ndo mudawe
Wachagua upendalo, moja lakutosheleza
Huwezi kulala njaa, hayuzwi kwa pesa nyingi
Ni machungwa tamanika, bali ndani yameoza

Walaji wafakamia, tena wala na maganda
Hawajali zao afya, hawajali kuendesha
Tena walia gizani, hata maji hawaoshi
Ni matamu ya Muheza, bali ndani yameoza

Ukifika Dasalaam, yamejaa Buguruni
Ukenda uwanja wa fisi, hapo ndipo soko kuu
Kuna bei za jumla, rejareja utapata
Ni matamu ya Muheza, bali ndani yameoza

Arusha yapo Mrina, hata Naaz yamejaa
Ukifika usiseme, yenyewe yatajileta
Chukua la chapuchapu, au kalye hotelini
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Huko mwanza yamejaa, kila kona utaona
Wateja waongezeka, vijana hata wazee
Haya machungwa jamani, kwani yana ladha gani?
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Watu wamedanganyika, kununua ya Muheza
Ya nyumbani hawapendi, wanasema ni machachu
Mwishowe wanajutia, miharisho ianzapo
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Wateja hawambiliki, wanakula na uozo
Wanadai yanakidhi, kwenye njaa ya haraka
Chalinze ukiyaona, hata wewe tatamani
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Abudula wa Tabata, nalia nimkumbukapo
Alisema ni matamu, halali bila kuyala
Mwisho yakamsulubu, yakamfanya kijiti
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Nilimwonya mara nyingi, asiyale si salama
Ila ye akakaidi, akaona namghasi
Akatoa fedha zake, akanunua kwa pupa
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Abudula akayala, mwisho kaanza endesha
Kamfunza na mkewe, naye akawa dereva
Wote wakaanza endesha, chanzo hayo ya Muheza
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Walimwengu sikieni, si salama ‘aya machungwa
Ningekuwa mwenye nchi, marufuku ningepiga
Yasingeuzwa nchini, na masoko ningefunga
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Tatizo ni moja kubwa, na watawala walaji
Watokapo ofisini, gulioni wapitia
Wanunua mojamoja, tena ya bei ghali
Ni matamu ya Muheza, ila ndani yameoza

Sikiza usikiaye, sishupaze shingo yako
Machungwa ya kununua, sio haya ya Muheza
Mbona mazuri yapo, kwani situnde mwenyewe?
Achana na ya Muheza, katunde nyumbani kwako


© Filipo Lubua, Nov. 30, 2012
 
Asante Filipo Lubuva kwa mistari mitamu yenye ujumbe mzito. Mimi mistari siiwezi hasilani ingawa nina rula.
Ila nasema hiviii: UKIMWI JAMANI UTATUMALIZA!
 
Last edited by a moderator:
Filipo safi sana, kuna mafunzo mengi kwenye hayo matunda. Sasa utayaepuka vipi wakati yanauzwa kwa bei nafuu, na kila mahali yapo? Njaa mbaya jamani!
 
Mkuu Lubua, kutunga mashairi ni kitu kinachofikirisha sana...kwa bongo zilizolala kama sie inakuwa kazi ya muda mrefu sana kutengeneza hata ubeti mmoja tu wenye maana.

Nimejaribu hapa kujibu (kwa namna fulani) shairi lako:


Na mbadala hayana, ya Muheza ni ya pekee
Utamuwe u bayana,ukiyala kwa upekee
Wala uozo hayana,usichague ya bei chee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani

Mola aso hiyana, machungwa katoa chee
Wachuuzi waso uungwana, bei zao za kipekee
Hawapendi kuungama, uozo wa kipekee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani

Waonjaji nao bayana, ni tatizo la kipekee
Wachuuzi waso bayana, huonjesha ‘mapedeshee’
Zimewajaa hiyana, papara kama za mee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani

Kampala hata Havanna, ya Muheza ndio pekee
Kwa afya za waungwana, machungwa ndio pekee
Kwa wachuuzi waungwana, uozo taweka dee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani
 
Mkuu Lubua, kutunga mashairi ni kitu kinachofikirisha sana...kwa bongo zilizolala kama sie inakuwa kazi ya muda mrefu sana kutengeneza hata ubeti mmoja tu wenye maana.

Nimejaribu hapa kujibu (kwa namna fulani) shairi lako:


Na mbadala hayana, ya Muheza ni ya pekee
Utamuwe u bayana,ukiyala kwa upekee
Wala uozo hayana,usichague ya bei chee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani

Mola aso hiyana, machungwa katoa chee
Wachuuzi waso uungwana, bei zao za kipekee
Hawapendi kuungama, uozo wa kipekee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani

Waonjaji nao bayana, ni tatizo la kipekee
Wachuuzi waso bayana, huonjesha ‘mapedeshee'
Zimewajaa hiyana, papara kama za mee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani

Kampala hata Havanna, ya Muheza ndio pekee
Kwa afya za waungwana, machungwa ndio pekee
Kwa wachuuzi waungwana, uozo taweka dee
Si wazee si vijana, machungwa nambari wani
Mkuu SMU, Upo sana kwenye mistari!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: SMU
hahahah nimeienda na linafurahisha, jaokua limeniacha na maswali mengi
 
Filipo safi sana, kuna mafunzo mengi kwenye hayo matunda. Sasa utayaepuka vipi wakati yanauzwa kwa bei nafuu, na kila mahali yapo? Njaa mbaya jamani!

Mkuu Mundu, vya dezo vinaua ndugu yangu. Kwani shida iko wapi, kwanini watu wasioteshe michungwa yao nyumbani wakayatunda matunda yasiyovunda?
 
chezea machungwa ya Tanga weye! Ndo maana virusi vinazidi kuzaliana huko!
 
Back
Top Bottom