Macron Na Starmer Watinga White House

Macron Na Starmer Watinga White House

Juuchini

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2018
Posts
1,644
Reaction score
2,300
Katika hali ya viongozi wa bara uroda kuchanganyikiwa, wanene waliotajwa hapo juu wameamua kumfuata mzee baba live. Watafanikiwa kumshawishi abadili msimamo?
 
Nawaza kama wataweza kumshawishi bwana Trump
 
Katika hali ya viongozi wa bara uroda kuchanganyikiwa, wanene waliotajwa hapo juu wameamua kumfuata mzee baba live. Watafanikiwa kumshawishi abadili msimamo?


Hawajamfuata bali wamealikwa. Toka Mwanzo Trump amefanya hivyo kwa viongozi wa mataifa makubwa ya Ulaya, kabla ya kikao chake na Putin.
 
Hawajamfuata bali wamealikwa. Toka Mwanzo Trump amefanya hivyo kwa viongozi wa mataifa makubwa ya Ulaya, kabla ya kikao chake na Putin.
Wakialikwa wanaenda haraka sana,sijui wanafaidi nini kule wakienda
 
Dunia inaenda kasi sana,ghafla US kawa chawa wa Rusia kwenye mzozo wa Ukraine!
Tatizo lengo kuu la Trump ni kushusha bei ya mafuta ili kusaidia uchumi wao ukue na kupunguza gharama za uzalishaji na uendeshaji shughuli za kiuchumi na hapo hapo kusimamisha vita mashariki na badala yake kuweka vikwazo vikali sana dhidi ya Iran kwenye kuuza mafuta yake sasa ili vikwazo vifanikiwe lazima mafuta yawe mengi sokoni hivyo inabidi Russia awe rafiki angalau kwa kinafiki na kumuondoshea vikwazo ili mafuta yake yaingie sokoni kwa wingi na kufanikisha lengo la kushusha bei na mafuta ya Russia yatakuwa mbadala wa yale ya Iran , issue ni je ule urafiki wa Russia na Iran ndio utafia hapo yale kupeana vifaa na misaada ya kivita ndio Russia atapotezea zile fadhila haya ngoja tujione siasa za kimataifa zinavyojichanua yetu macho na masikio.
 
Tatizo lengo kuu la Trump ni kushusha bei ya mafuta ili kusaidia uchumi wao ukue na kupunguza gharama za uzalishaji na uendeshaji shughuli za kiuchumi na hapo hapo kusimamisha vita mashariki na badala yake kuweka vikwazo vikali sana dhidi ya Iran kwenye kuuza mafuta yake sasa ili vikwazo vifanikiwe lazima mafuta yawe mengi sokoni hivyo inabidi Russia awe rafiki angalau kwa kinafiki na kumuondoshea vikwazo ili mafuta yake yaingie sokoni kwa wingi na kufanikisha lengo la kushusha bei na mafuta ya Russia yatakuwa mbadala wa yale ya Iran , issue ni je ule urafiki wa Russia na Iran ndio utafia hapo yale kupeana vifaa na misaada ya kivita ndio Russia atapotezea zile fadhila haya ngoja tujione siasa za kimataifa zinavyojichanua yetu macho na masikio.
Trump ana dili lake la kufanya na Iran, huhitaji kumuwekea vikwazo Iran Ili kuchezesha bei ya mafuta
 
Trump ana dili lake la kufanya na Iran, huhitaji kumuwekea vikwazo Iran Ili kuchezesha bei ya mafuta
Wairan washakataa hilo dili na vikwazo kashaweka tayari vya kwanza na sasa kaweka vya pili akitarget meli za kusambazia mafuta wanategemea vikwazo vikiwa vikali vitawarudisha wairan mezani kwenye dili ila wairan wako very smart kwa kuwa kwa sasa bado demand ya oil ni kubwa na bei iko juu labda mafuta ya russia vikwazo vikitoka na wasaudi wakizalisha zaidi bei itashuka na hapo sasa wairan watakosa soko labda pengine watabadili msimamo ila sidhani kwa kuwa uchumi wao wamejaribu kuudiversify bila kutegemea mafuta japo.bado huko ndio wanatengeneza pato kubwa
 
Tatizo lengo kuu la Trump ni kushusha bei ya mafuta ili kusaidia uchumi wao ukue na kupunguza gharama za uzalishaji na uendeshaji shughuli za kiuchumi na hapo hapo kusimamisha vita mashariki na badala yake kuweka vikwazo vikali sana dhidi ya Iran kwenye kuuza mafuta yake sasa ili vikwazo vifanikiwe lazima mafuta yawe mengi sokoni hivyo inabidi Russia awe rafiki angalau kwa kinafiki na kumuondoshea vikwazo ili mafuta yake yaingie sokoni kwa wingi na kufanikisha lengo la kushusha bei na mafuta ya Russia yatakuwa mbadala wa yale ya Iran , issue ni je ule urafiki wa Russia na Iran ndio utafia hapo yale kupeana vifaa na misaada ya kivita ndio Russia atapotezea zile fadhila haya ngoja tujione siasa za kimataifa zinavyojichanua yetu macho na masikio.
Russia sio mjinga waachane na rafiki wa maana aliyewasaidia kipindi kigumu halafu ghafla aungane na aliyekuwa adui yake .. hujiuliza tu kama usa angekuwa anamshinda rusia si angemmalizia akafia mbali huko .. rusia sio mjinga amuamini usa kiasi hicho huoni hata mashart kwa sasa rusia ndo anapanga hawezi kuwabwege hivyo ni kuendelea kumpa usa ukuu ambao utakuja kumuuzia tena hata akiruhusu kununua mafuta itakuwa ni kwa ruble ya russia maana russia anajua kuan siku atakuwa na mabillioni dolla hawezi kuyatumia
 
Back
Top Bottom