yoga
JF-Expert Member
- Jan 6, 2013
- 1,830
- 8,636
Habari zenu wapendwa, kwa ufupi kabisa niende moja kwa moja kwenye mada.
Nimebahatika kuutembelea mji wa Mwanza kwa wiki hii. Moja ya vitu vimenishtua ni hii hospitali ya wilaya ya Ilemela.
Kwa upande wa miundombinu hospitali imekamilka kwa asilimia 100 toka 2020. Hospitali hii imejengwa toka mwaka 2017
Inasemwa vifaa na watumishi havipo!
Hospitali imefungwa for two years toka ikamilike. Ukipita kwenye hospitali za Sekouture, Bugando na zile za private wagonjwa wamejazana kama magunia! Na nasikia hospitali nyingi za wilaya (mpya) zilizojengwa kwa mbwembwe awamu ya tano nikama zimetelekezwa. Hazijakamilika na zilizo kamilika hazifanyi kazi
Sasa hizi fedha mmetupa humu si zingetumika kuboresha hospitali zilizokuwepo kuliko kujenga hospitali mpya ambazo zinabaki kuwa magofu? Waziri wa TAMISEMI, Bashungwa unajua mpaka sasa ni hospitali ngapi za wilaya ambazo ni mpya zinafanya kazi?
Waziri wa Afya ushawaza kufuatilia hili la hospitali hizi za wilaya kutokufanya kazi? Kwanini tunawatesa watanzania hatakama tushajua watanzania wengi waga hawajielewi? Bila kukusahau mbunge wa ilemela, Mama Mabula hii hospitali ya wilaya yako vipi?
Mkurugenzi wa wilaya uko wapi na mkuu wako wa wilaya?? Ewe mkuu wa mkoa unaye fanya ziara za nje ya mkoa mpaka wapendwa wetu wanapata ajali huoni umuhimu wa hospitali hii kuhakikisha ina fanya kazi?
Niwaombe nkirudi Mwanza tena tukute hospitali hii inafanya kazi na sio kuitelekeza !! Bila kusahau uwanja wa ndege mnatutia aibu jamani kutushusha kwenye uwanja ambao passenger building nikama sebule ya nyuma za magomeni za NHC. Ilo jengo nalo mlikamilishe!!
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Mkurugenzi wa Wilaya Ilemela afafanua
Akizungumzia kuhusu madai ya kukosekana kwa vifaa na uhaba wa watumishi katika Hospitali ya Wilaya ya Ilemela, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Mhandisi Modest Apolinary alisema:
“Hizo taarifa siyo za kweli, huduma zinaendelea kama kawaida, majengo yamekamlika mengi na kuna fedha ambazo tumezipata tunaendelea kukamilisha baadhi ya majengo ambayo mengi yamefikia asilimia 70.
“Kuna shilingi milioni 500 ambazo tulipatiwa kwa ajili ya kujenga wodi tatu ambazo zimefikia asilimia 70. Mwezi uliopita pia kulikuwa na bajeti ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya majengo mengine ikiwemo mochwari.
“Ni kweli kuna baadhi ya huduma ambazo hazipatikani hospitalini kwetu kama vile upasuaji kwa kuwa kuna vifaa havikamilika, tukipata wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo tunawapeleka Bugando.
“Na ninadhani kufikia Juni mwaka huu ujenzi wa majengo ambayo hayajakamilika kwa sasa, utakuwa umeshakamilika kwa asilimia 100.
“Kuhusu dawa bado hatujapata fungu la dawa lakini huduma zinaendelea kama kawaida, hiyo haimaanishi hakuna dawa wala huduma kukosekana.”
Mganga Mkuu akiri uhaba wa vifaa
Naye, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Charles M. Samson alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema:
“Hospitali haijafungwa, huduma zinaendelea kama kawaida, hospitai inafanya kazi vizuri na hata mimi nipo hapa hospitali muda huu.
“Huduma zinaendelea kama kawaida, watumishi wapo 15, wanatosha kwa kuwa hii ni hospitali mpya, hatuna watumishi wa kwetu tumechukua sehemu mbalimbali.
“Unajua Serikali ilijenga hospitali hizi za wilaya 67 nchi nzima hivyo kuna changamoto za hapa na pale lakini haimaanishi huduma hakuna, kuhusu vifaa kweli nakiri kuna upungufu huo, Serikali inafanyia kazi na ninaamini kabla yam waka huu wa fedha kuisha tunaweza kuwa tumepata vifaa.”
Nimebahatika kuutembelea mji wa Mwanza kwa wiki hii. Moja ya vitu vimenishtua ni hii hospitali ya wilaya ya Ilemela.
Kwa upande wa miundombinu hospitali imekamilka kwa asilimia 100 toka 2020. Hospitali hii imejengwa toka mwaka 2017
Inasemwa vifaa na watumishi havipo!
Hospitali imefungwa for two years toka ikamilike. Ukipita kwenye hospitali za Sekouture, Bugando na zile za private wagonjwa wamejazana kama magunia! Na nasikia hospitali nyingi za wilaya (mpya) zilizojengwa kwa mbwembwe awamu ya tano nikama zimetelekezwa. Hazijakamilika na zilizo kamilika hazifanyi kazi
Sasa hizi fedha mmetupa humu si zingetumika kuboresha hospitali zilizokuwepo kuliko kujenga hospitali mpya ambazo zinabaki kuwa magofu? Waziri wa TAMISEMI, Bashungwa unajua mpaka sasa ni hospitali ngapi za wilaya ambazo ni mpya zinafanya kazi?
Waziri wa Afya ushawaza kufuatilia hili la hospitali hizi za wilaya kutokufanya kazi? Kwanini tunawatesa watanzania hatakama tushajua watanzania wengi waga hawajielewi? Bila kukusahau mbunge wa ilemela, Mama Mabula hii hospitali ya wilaya yako vipi?
Mkurugenzi wa wilaya uko wapi na mkuu wako wa wilaya?? Ewe mkuu wa mkoa unaye fanya ziara za nje ya mkoa mpaka wapendwa wetu wanapata ajali huoni umuhimu wa hospitali hii kuhakikisha ina fanya kazi?
Niwaombe nkirudi Mwanza tena tukute hospitali hii inafanya kazi na sio kuitelekeza !! Bila kusahau uwanja wa ndege mnatutia aibu jamani kutushusha kwenye uwanja ambao passenger building nikama sebule ya nyuma za magomeni za NHC. Ilo jengo nalo mlikamilishe!!
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Mkurugenzi wa Wilaya Ilemela afafanua
Akizungumzia kuhusu madai ya kukosekana kwa vifaa na uhaba wa watumishi katika Hospitali ya Wilaya ya Ilemela, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Mhandisi Modest Apolinary alisema:
“Hizo taarifa siyo za kweli, huduma zinaendelea kama kawaida, majengo yamekamlika mengi na kuna fedha ambazo tumezipata tunaendelea kukamilisha baadhi ya majengo ambayo mengi yamefikia asilimia 70.
“Kuna shilingi milioni 500 ambazo tulipatiwa kwa ajili ya kujenga wodi tatu ambazo zimefikia asilimia 70. Mwezi uliopita pia kulikuwa na bajeti ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya majengo mengine ikiwemo mochwari.
“Ni kweli kuna baadhi ya huduma ambazo hazipatikani hospitalini kwetu kama vile upasuaji kwa kuwa kuna vifaa havikamilika, tukipata wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo tunawapeleka Bugando.
“Na ninadhani kufikia Juni mwaka huu ujenzi wa majengo ambayo hayajakamilika kwa sasa, utakuwa umeshakamilika kwa asilimia 100.
“Kuhusu dawa bado hatujapata fungu la dawa lakini huduma zinaendelea kama kawaida, hiyo haimaanishi hakuna dawa wala huduma kukosekana.”
Mganga Mkuu akiri uhaba wa vifaa
Naye, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Charles M. Samson alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema:
“Hospitali haijafungwa, huduma zinaendelea kama kawaida, hospitai inafanya kazi vizuri na hata mimi nipo hapa hospitali muda huu.
“Huduma zinaendelea kama kawaida, watumishi wapo 15, wanatosha kwa kuwa hii ni hospitali mpya, hatuna watumishi wa kwetu tumechukua sehemu mbalimbali.
“Unajua Serikali ilijenga hospitali hizi za wilaya 67 nchi nzima hivyo kuna changamoto za hapa na pale lakini haimaanishi huduma hakuna, kuhusu vifaa kweli nakiri kuna upungufu huo, Serikali inafanyia kazi na ninaamini kabla yam waka huu wa fedha kuisha tunaweza kuwa tumepata vifaa.”