DOKEZO Madai ya uharibifu wa Bustani

DOKEZO Madai ya uharibifu wa Bustani

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Ndg.Mhariri,

Naomba kutoa malalamiko yangu nikiwatuhumu Afisa Madini Mkoa wa Simiyu na Afisa Mtendaji wa Kata ya Dutwa kwa kushindwa kusimamia kikamilifu kwa namna moja au nyingine madai ya malipo ya bustàni yangu iliyo haribiwa na maji yenye kemikali yaliyo tiririshwa na mwekezàji wa Mgodi na.2 uliopo Kati ya Bariadi na Busega tarehe 5, June.

Hivyo Basi, kutokana na hali hiyo niliamua Mimi na wenzagu watano kudai haki yetu kisheria kwa kudai fidia ya uharibifu uliojitokeza kupitia wataalam wa kilimo, viongozi wa serikali wilaya na mkoa vilevile kufikisha malalamiko yangu kwa Katibu wa Wanawake CCM taifa alipokuwa ziarani Mkoani Simiyu na nakumpa nakala ya malalamiko ya madai yangu na kudai atayashughulikia. Lakini cha kushangazà wenzetu watatu walilipwa Chini ya madai Yao, huku Mimi na wenzangu wawili mpaka sasa hatujui hatima yetu.

Nimeamua kuandika haya nikiambatànisha na barua ya tathimini ya malipo na utambulisho ili mamlaka zinazohusika akiwemo Waziri wa Madini, Waziri mkuu na Rais Samia Suluhu Hassan waweze kunisaidia mimi na wenzagu kupatata haki yetu. Kwani Mimi Ni mkulima na ninategemea kilimo ili niweze kujikimu Manisha na familia yangu

IMG_20241214_130116_4.jpg

IMG_20241214_130045_2.jpg
IMG_20241214_130014_1.jpg
 
Back
Top Bottom