Madai ya Wenyeviti wa CCM Vs Kubenea

Selous

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2008
Posts
1,325
Reaction score
145


Hivi Guninita usipoenda tukufanye nini? Ole wako usiende....
 
huyu guninita si yule alikuwa ccm, then chadema tena ccm? mahakama ndo mtoa haki kikatiba karibu kwenye ulingo bwana guniata, hata hivyo uwe tayari kujibu maswali mengi ndani ya kiapo, kuhusu uhusiano wako na mafisadi, ushirikiano wako na akina mulla ambao kule mbeya wanajulikna kama majangili wa mali asili za nchi yetu. ukimaliza kujibu hayo maswali watanzania watapenda pia kujua ulivyoshiriki kifiadi kuua ule maradi wa mabasi wa wanafunzi jijini dsm wakati huo ukiwa ndo sijui mshika dau kwenye uvccm
 
Sawa Guninita tumekusikia baba.Sijui wakati huu ukitoka CCM utahamia chama gani,manake wewe umekaa kama sakayonso
 
Baada ya Wenyeviti wa CCM kutoa taarifa kutishia kulishitaki gazeti la MwanaHalisi na Mhariri wake, Saed Kubenea,

Tanzania Daima - CCM kumshitaki Kubenea

Gazeti hilo limetoa taarifa ifuatayo, ikiwa ni siku moja kabla ya Waandishi wa habari kufanya maandamano kupinga kufungiwa kwa gazeti hilo.


Taarifa
 
Last edited:
hakuna anayeza kuzui haki hata siku moja . kwenye ukweli haki utawala daima.
propaganda CCM hazijaanza leo wala jana tumezizoea .
Mwana Halisi keep it.
don`t fear those who destroy body .fear who can destroy body and soul.
 
Wameshindwa ile mbaya Tarime sasa they are creating another Tarime .Hizi ni dalili tosha za dola dhaifu kuanguka vibaya .Wacha tungoje tuone .Wako wengi walisema wanaenda huko Mahakamani hadi sasa hawajafika akiwemo Masha na kundi lake .Sasa Guninita .Haya yetu macho
 
Hivi huko mahakamani mbona hawaendi na kucha wanatangaza wana mpango huo? Hivi kuna sababu ya wao kutoa kauli kuwa wataenda mahakamani badala ya kuamua tu kwenda mahakamani?
 
Guninita hana jipya akae atulie ameona JK ameshajua nini anafanya....anatapatapa
 
Bora mahakama iaumue kisha muongo ajulikane. kubenea au Guninita
 


Tujiandae vema, ukweli haupindi hata siku moja, je wataenda?
 
washazoea kuonekana kwenye tv na wasomwe magazetini vitendo
loh!!!!!1

lowassa mahakama no

mgonja mahakamani no

msabaha mahakamani no

miakamba mahakamani no

vifisadi vidogo vidogo

heeeeeeeeeeee gunnita nae loh!!!!!!!!!!!! we baba uchoki na aibu za duinia hii!!!!

m nafikiri hata kuendelea na hii mada haina maana wakati toka lini majambazi yakajipeleka mahakamani!!!mlifikiri mkono mjinga kukaa kimya??????????????


.......

.........
 
Mahakama ni sehemu ya haki.
Kubenea alisema aliyosema akijua kuna mahakama.
Kubenea anajua hatari ya kwenda mahakani na ndiyo sababu yule mjinga Mkuchika hakuthubutu, badala yake katumia mabavu.
Ole wake Guninita asipokuwa makini atakimbia na huo uenyekiti wake wa sisiemu.
Haya. Shauri yake. Ngoja ninyamaze maana kesho atatishia tena gazetini kumshitaki mchukia mafisadi kwamba alisema kuwa atamshitaki Kubenea. Mwene, mimi sina ubavu huo wa kwenda mahakamani au kumwagiwa na tindikali.
Kwa heri.
 
Mzee mwenzangu Kubenea, ...chukua zangu tano.

Mtu mzima hatishiwi nyau!! Kama wanataka kwenda wambie wakaishi huko huko mahakamani hadi kesi iishe. Tumechoka na vijimaneno vyao visivyo na mshiko,... kama jibwa kuuubwa linalobweka bweka hovyo lakini halina meno. Waambie tena, "neeendeeeni hata usiku wa manane", tuone kama wathubutu kukanyaga huko!
 
Kikubwa ninaiomba mahakama ifanye kazi kama chombo huru kabisa cha kutetea haki. Kitakuwa kitendo cha aibu sana na kudhalilisha mahakama iwapo mahakama itakubali kutumimiwa na mafisadi hawa wa CCM ili kuisupress haki ya mtanzania, ya habari na kujieleza, ili tu kuwaridhisha mashetani ( mafisadi) wachache akina Guninita na wenzake wanaomtuma.

Huyu Guninita atakuwa anatumiwa na akina Lowassa, na wenzake ili kunyamazisha sauti thabiti na kweli ya MwanaHalisi.

Kwa ufisadi huu wa nchi yetu hata kama Kubenea na watanzania wote tutanyamazishwa kwa vitisho vya mafisadi hakika hata miti na mawe vitasema maana huu ufisadi uko kila kona.

Aluta continua Kubenea
 
Hivi huko mahakamani mbona hawaendi na kucha wanatangaza wana mpango huo? Hivi kuna sababu ya wao kutoa kauli kuwa wataenda mahakamani badala ya kuamua tu kwenda mahakamani?


Mkjj,Hao ni kawaida yao kutisha wakitaka kugain public confidence.Ni maneno ya mfa maji haachi kutapatapa.Aibu imewakaa mpaka shingoni.
 
Hata hivyo uongozi wa MwanaHALISI unaendelea kusisitiza kuwa kile kilichoandikwa ni kweli na sahihi na utaendelea kusimamia ukweli huo.

Saed Kubenea
Mkurugenzi Mtendaji

Kubenea for president!,

wakienda huko tuna ushahidi mwingi wa kukusaidia dhidi ya hao mafisadi, wasidhani uko peke yako, I promise you ndugu yangu mbingu zitashuka chini wakithubutu kwenda huko, watu wazima huwa hawatishianii nyau!
 
Namshukuru sana Guninita na wenzake na nawahimiza waende mahakamani haraka kwa sababu naamini kupitia kesi hiyo tutajua mengi, hata yale ambayo Mwanahalisi waliamua kutoyaandika. Bravo Guninita, suiishie njiani please
 
Maskini Gegeduka akisikia joto la maji basi hujivua gamba akifikiri atapata nafuu ya joto na kumbe ndio anaiva kuwa kitafunio
 
Wenyeviti wa CCM wa mikoa, Deo Sanga, Clement Mabina, Khamis Mgeja, John Guninita, Onesmo Ngole, William Kusila na Hypolitus Matete, wamewaita waandishi wa habari na kudai kwamba wamepelaka barua kwa MwanaHalisi wakitaka kuombwa radhi vinginevyo wataenda mahakamani.

Hata hivyo, Saed Kubenea, hadi saa 7.58 mchana huu hajapokea hiyo barua ambayo waandishi wameambiwa imepelekwa toka juzi.

Kimsingi wanataka waombwe radhi na MwanaHAlisi, gazeti ambalo halipo mtaani, ni amri ambayo hakuna JAji atakeyeitoa maana ni sawa na kumwambia Jaji atoe hukumu ya kumtaka mtu ajirushe toka gorofa ya 20 au ajirushe baharini
 

Attachments

Last edited:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…