TIASSA
JF-Expert Member
- Jun 17, 2014
- 2,926
- 3,530
Wasalaam Madokta;
Mara kama ya tatu sasa nakutana na hawa jamaa ambao huonyesha madhara ya vitu mbalimbali kama chumvi, vipodozi, mayai ya kisasa, soda na kilichonistaajabisha juzi walikuwa wakionyesha virus vilivyomo kwenye condom.
Unajua walifanyaje? Walichukua Salama Condom wakaweka maji kama lita moja hivi, wakaweka yai la kisasa, wakaweka spirit ile ya saloon, baada ya muda yai likaanza kuwa kubwa, ile rangi ya purple ya spiriti kwenye condom ikaisha yote wakasema imeliwa na virusi, baadaye wakaweka chumvi juu ya ile condom, daaa ni mlolongo mrefu ila wanadai virus vinaonekana.
Kingine walichukua yai la kisasa wakalipaka Carolite, wakaweka Gryceline, chumvi na Spirit moto ukawaka wanyewe. Sasa najiuliza, Je haya makitu ni kweli? Au wanajaribu kucheza na chemical reaction?!
Mara kama ya tatu sasa nakutana na hawa jamaa ambao huonyesha madhara ya vitu mbalimbali kama chumvi, vipodozi, mayai ya kisasa, soda na kilichonistaajabisha juzi walikuwa wakionyesha virus vilivyomo kwenye condom.
Unajua walifanyaje? Walichukua Salama Condom wakaweka maji kama lita moja hivi, wakaweka yai la kisasa, wakaweka spirit ile ya saloon, baada ya muda yai likaanza kuwa kubwa, ile rangi ya purple ya spiriti kwenye condom ikaisha yote wakasema imeliwa na virusi, baadaye wakaweka chumvi juu ya ile condom, daaa ni mlolongo mrefu ila wanadai virus vinaonekana.
Kingine walichukua yai la kisasa wakalipaka Carolite, wakaweka Gryceline, chumvi na Spirit moto ukawaka wanyewe. Sasa najiuliza, Je haya makitu ni kweli? Au wanajaribu kucheza na chemical reaction?!