Madalali wasajiliwe na walipee kodi

Madalali wasajiliwe na walipee kodi

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Wakati umefika tuwe na sheria ya kutaka madalali wasajiliwe na walipe kodi kwani licha ya kuingiza kipato kupitia udalali, wanaongezea watu gharama za maisha huko wao hawalipwi kodi.

Dalali akikutafutia nyumba/chumba, unatakiwa umlipe kodi ya mwezi mmoja mbali na kodi unayopaswa kumlipa mwenye nyumba na huu mzigo wote ni wa mpangaji ambae kipato chake teyari anakilipa kodi kupitia PAYE au indirect tax ila huyu dalali halipi kodi yoyote wakati mwenye nyumba sheria inambana alipe kodi baada ya kupangisha.

Mfano, umepata chumba cha shilingi 200,000 kwa mwezi na unatakiwa ulipe kwa miezi mitatu, maana yake utapaswa kulipa jumla ya shilingi 800,0000 ambapo shilingi 600,000 zinaenda kwa mwenye nyumba na shilingi 200,000 kwa dalali.

Sasa dalali kama huyu akiwa na vyumba 10 na akavipangisha vyote ndani ya mwezi, si anakuwa ameingiza shilingi 2000,000 ndani ya mwezi. Sasa kwanini mtu kama huyu asisajiliwe na ailipe kodi wakati mtumishi wa umma mwenye mshahara mfano wa shilling 400,000 kwa mwezi analipa kodi? Haingii akilini.

Kumbukumbu kuna madalali wanapangisha majumba yenye kodi za malaki na hawalipwi kodi kisa hakuna sheria inawabana wakati mmachinga anaetembeza viatu mitaani au anaepanga bidhaa zake chini anatakiwa kulipia kitambulisho cha mmachinga ambacho kwa uhalisia ni kodi kwa jina la kitambulisho cha mmachinga.

Binafsi naamini watumishi wa umma wapatao laki tano na kitu na wale wa sekta binafsi kupitia PAYE pamoja na wafanyabiashara wachache kupitia TRA, ndio wanaolazimika kulipa kodi wakibeba mzigo wa kodi unaopaswa kubebwa na watanzania wanaokaribia milioni 60.

Matokeo ya hali hii ni watumishi wa umma na wale wa binafsi na wafanyabiashara wachache kubebeshwa mzigo mkubwa wa direct tax mbali na indirect tax wanazolipa wanaponunua bidhaa na huduma mbalimbali na hivyo kuwapunguzia kipato na kurudisha nyuma maendeleo yao.

Kama mama ntile analipia kitambulisho cha mmachinga, kwani hawa madalali, boda boda na wafanyakazi wengine wasilipe kodi?

Ukweli ni kwamba, kila mwenye kipato kupita shughuli ilio rasimi au isiyo rasimi, akilipa kodi, mzigo wa kodi utapungua kwa kila mtanzania kwani tutakuwa tume-share mzigo huo kwa watu wengi zaidi badala ya mzigo huo kubebwa na wachache.

Kuna watu kweli wana biashara ndogo na vipato vidogo wanaostahili kutolipa kodi lakini kuna wengi wanajificha au sheria inawaficha katika hili kundi na mfano ni hawa madalali na bodaboda(boda boda wanaweza kulipa hata kodi ya shilingi 5000 au 10000 kwa mwezi).

Hata wamiliki wa hizi bodaboda, wa taxi na hata wale wa Bajaji, nao wanapaswa kulipa kodi kwani wanaingiza kipato kupitia hizi biashaara hivyo na wao wachangie na kama ni kusamehe, basi wasamehewa vijana wanaojiriwa kuendesha hivi vyombo vya moto lakini sio wamiliki wa hivi vyombo(Bajaji, taxi na bodaboda).

Ukweli ni kwamba,rasilimali za nchi hii zingetumika vizuri, zingetosha kabisa kuipatia nchi mapato ya kutosha na tungeweza kusamehee wengi tu kulipa kodi ila ndio hivyo waliokabidhiwa dhamana ya kuongoza nchi hii wameingia mamikataba ya hovyo na matokeo yake rasilimali zetu zinanufaisha wageni na mfano mzuri ni gesi ya Mtwara ambayo kwa sehemu kubwa inanufaisha mabeberu kama alivyosema Magufuli.

Kwakuwa wote kwa ujumla wetu tunailea CCM iliyotufikisha hapa, basi wote tugawane gharama za kuilea CCM na si wachache wabebe mzigo kwa niaba ya wengi(wote tulipe kodi).

Kama kodi hizi zinatuuma, tuungane kuikataa CCM inayolea hata wale wanaotafuna kodi zetu kama ripoti Za CAG za kila mwaka zinavyobainisha, vinginevyo tuache unafiki na kulalamika kwani tumeridhika na hali hii

Ukipenda boga(CCM), upende na ua lake(kodi usizo stahili na zisizo rafiki), Vinginevyo tuungane kuikataa CCM na makandokando yake yote.
 
Mimi naona madalali walipwe na mpangishaji kama walivyo mawakala na si kwa mpangaji.
 
Baada ya madalali kuanza kulipa kodi. Wafuatie wabunge.
 
Kwa nini?
Dalali ni kama wakala, anarahisisha kazi kwa mpangishaji kama ilivyo mawakala kurahisisha kazi kwa makampuni(kwa kutolea mfano)

Kama wateja hawawalipi mawakala wanaofanya kazi sawa na madalali, kwa nini wawalipe madalali?

Unapojenga nyumba/fremu ya kupangisha, jukumu la kutafuta wateja ni lako kwa gharama zako maana wewe ndio unayewekeza. Hivyo ndivyo yanavyofanya makampuni kupitia mawakala wao.

Dalali anatakiwa alipwe na mpangishaji na wala si mpangaji.
 
Mkuu ipo kodi ya zuio yaani "withholding tax" ambayo ni wajibu kwa mpata huduma kuitoza kwa mtoa huduma. Hivyo hata kama unalipa kodi kwa mwenye nyumba na pia kutoa ada za udalali, katika mkataba unaouingia unapaswa iwekwe wazi na kuonyesha malipo ya 95% kwa kipato chao, na 5% inapaswa kulipwa kama kodi ya mapato.

Elimu ya kodi ya zuio inapaswa kutolewa sana kwa mlipa kodi. Kwa kuwa kila huduma unayoilipia inapaswa kuwekewa zuio la kodi na kuiwasilisha TRA. Hapa pia ni eneo ambalo pia kuna kiasi kikubwa cha kodi ya mapato hupotea.
 
Na sisi madalali wa vyeo kwenye taasisi mnatuweka kundi gani.
 
TRA hawajui eneo hilo kama lipo na wanaofanya hizo kazi wanapata mapato. Sector isiyo rasmi ina kipato chake. Shida ni namna ya kufanya walipe kodi. Haiwezekani katika population ya watu milioni 60, miloni tatu tu ndio wawe wanalipa kodi.

Ni aibu mno kwa wanaoangalia vyanzo vya kodi. Mzigo wa kodi hauwezi kubebwa na watu wachache kiasi hicho.
 
Dalali ni kama wakala, anarahisisha kazi kwa mpangishaji kama ilivyo mawakala kurahisisha kazi kwa makampuni(kwa kutolea mfano)

Kama wateja hawawalipi mawakala wanaofanya kazi sawa na madalali, kwa nini wawalipe madalali?

Unapojenga nyumba/fremu ya kupangisha, jukumu la kutafuta wateja ni lako kwa gharama zako maana wewe ndio unayewekeza. Hivyo ndivyo yanavyofanya makampuni kupitia mawakala wao.

Dalali anatakiwa alipwe na mpangishaji na wala si mpangaji.
Upo sahihi,sisi ni wapumbavu kulipa kodi ya mwezi kwa dalali.Hiyo ni kazi ya mwenye nyumba maana amefanyiwa biashara.
 
TRA hawajui eneo hilo kama lipo na wanaofanya hizo kazi wanapata mapato. Sector isiyo rasmi ina kipato chake. Shida ni namna ya kufanya walipe kodi. Haiwezekani katika population ya watu milioni 60, miloni tatu tu ndio wawe wanalipa kodi.
Ni aibu mno kwa wanaoangalia vyanzo vya kodi. Mzigo wa kodi hauwezi kubebwa na watu wachache kiasi hicho
Wanataka kodi bila kuumiza vichwa na pia si wabunifu.
 
Wakati umefika tuwe na sheria ya kutaka madalali wasajiliwe na walipe kodi kwani licha ya kuingiza kipato kupitia udalali, wanaongezea watu gharama za maisha huko wao hawalipwi kodi.

Dalali akikutafutia nyumba/chumba, unatakiwa umlipe kodi ya mwezi mmoja mbali na kodi unayopaswa kumlipa mwenye nyumba na huu mzigo wote ni wa mpangaji ambae kipato chake teyari anakilipa kodi kupitia PAYE au indirect tax ila huyu dalali halipi kodi yoyote wakati mwenye nyumba sheria inambana alipe kodi baada ya kupangisha.

Mfano, umepata chumba cha shilingi 200,000 kwa mwezi na unatakiwa ulipe kwa miezi mitatu, maana yake utapaswa kulipa jumla ya shilingi 800,0000 ambapo shilingi 600,000 zinaenda kwa mwenye nyumba na shilingi 200,000 kwa dalali.

Sasa dalali kama huyu akiwa na vyumba 10 na akavipangisha vyote ndani ya mwezi, si anakuwa ameingiza shilingi 2000,000 ndani ya mwezi. Sasa kwanini mtu kama huyu asisajiliwe na ailipe kodi wakati mtumishi wa umma mwenye mshahara mfano wa shilling 400,000 kwa mwezi analipa kodi? Haingii akilini.

Kumbukumbu kuna madalali wanapangisha majumba yenye kodi za malaki na hawalipwi kodi kisa hakuna sheria inawabana wakati mmachinga anaetembeza viatu mitaani au anaepanga bidhaa zake chini anatakiwa kulipia kitambulisho cha mmachinga ambacho kwa uhalisia ni kodi kwa jina la kitambulisho cha mmachinga.

Binafsi naamini watumishi wa umma wapatao laki tano na kitu na wale wa sekta binafsi kupitia PAYE pamoja na wafanyabiashara wachache kupitia TRA, ndio wanaolazimika kulipa kodi wakibeba mzigo wa kodi unaopaswa kubebwa na watanzania wanaokaribia milioni 60.

Matokeo ya hali hii ni watumishi wa umma na wale wa binafsi na wafanyabiashara wachache kubebeshwa mzigo mkubwa wa direct tax mbali na indirect tax wanazolipa wanaponunua bidhaa na huduma mbalimbali na hivyo kuwapunguzia kipato na kurudisha nyuma maendeleo yao.

Kama mama ntile analipia kitambulisho cha mmachinga, kwani hawa madalali,boda boda na wafanyakazi wengine wasilipe kodi?

Ukweli ni kwamba, kila mwenye kipato kupita shughuli ilio rasimi au isiyo rasimi, akilipa kodi, mzigo wa kodi utapungua kwa kila mtanzania kwani tutakuwa tume-share mzigo huo kwa watu wengi zaidi badala ya mzigo huo kubebwa na wachache.

Kuna watu kweli wana biashara ndogo na vipato vidogo wanaostahili kutolipa kodi lakini kuna wengi wanajificha au sheria inawaficha katika hili kundi na mfano ni hawa madalali na bodaboda.(boda boda wanaweza kulipa hata kodi ya shilingi 5000 au 10000 kwa mwezi).

Ukweli ni kwamba,rasilimali za nchi hii zingetumika vizuri, zingetosha kabisa kuipatia nchi mapato ya kutosha na tungeweza kusamehee wengi tu kulipa kodi ila ndio hivyo waliokabidhiwa dhamana ya kuongoza nchi hii wameingia mamikataba ya hovyo na matokeo yake rasilimali zetu zinanufaisha wageni na mfano mzuri ni gesi ya Mtwara ambayo kwa sehemu kubwa inanufaisha mabeberu kama alivyosema Magufuli.

Kwakuwa wote kwa ujumla wetu tunailea CCM iliyotufikisha hapa, basi wote tugawane gharama za kuilea CCM na si wachache wabebe mzigo kwa niaba ya wengi(wote tulipe kodi).

Kama kodi hizi zinatuuma, tuungane kuikataa CCM inayolea hata wale wanaotafuna kodi zetu kama ripoti Za CAG za kila mwaka zinavyobainisha, vinginevyo tuache unafiki na kulalamika kwani tumeridhika na hali hii

Ukipenda boga(CCM), upended na ua lake(kodi usizo stahili na zisizo rafiki) vinginevyo tuungane kuikataa CCM.

Sahihi kabisa

Na kodi ni wajibu

Halafu maendeleo hayanavyama
 
Upo sahihi,sisi ni wapumbavu kulipa kodi ya mwezi kwa dalali.Hiyo ni kazi ya mwenye nyumba maana amefanyiwa biashara.
Tatizo kama hutaki, utakosa nyumba ya kupanga unless ubahatishe kupata pa kupanga bila dalali kuhusika.

Wenye nyumba wanashirikiana na madalali kwa kiasi kikubwa.
 
Madalali wote wana kitambulisho cha mmachinga. Hakuna anaefahamu wanaingiza shilungi ngapi kwa siku, mwezi au mwaka.
 
Back
Top Bottom