Goodluck TZ
JF-Expert Member
- Oct 24, 2015
- 1,448
- 661
Kwanza kabisa tambua Madee alikuwa haimbi Hip Hop bali alikuwa anarap kama wa fm academia tu...kwenye mafanikio
Unaukumbuka wimbo wa Nikusaidieje wa Prof J unajua ulimpa mafanikio gani? Kwanza unajua Mali za Joh Makini au kwakuwa hajitangazi??? Unatambua madee na nyimbo zake za mduara aimbe miaka buku hafikii utajiri wa Joh Makini achilia mbali Fid Q...
Hip hop sivyo anavyodhani yeye, mbona hao kina Mwana FA, ROMA, wanapiga hela na bado harakati zinaendelea??? Tatizo Babu Tale na Mkubwa na Wanae wanahitaji wabana pua ndio maana akabadili mfumo...
Wanaoimba wameshajifia kibaaaaao, wapo wapi hawa Mr Nice, TID, Mb Dog, Z Anton, Pingu na Deso n.k.... asikashifu kisa anabana pua moja Sasa hivi...Kwanza kwa mziki gani anaoimba haswa zaidi ya PUMBA TUPU
Madee nimemdharau sana,ila simlaumu, inaonekana haujui mchango wa hip hop katika maendeleo na mafanikio ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya nchini. Angeufahamu mchango wake asingekuja na crazy opinion like dat. Hip hop ndio genre pekee inayo_relate na Watz wengi wenye maisha ya kawaida, hip hop ni harakati zisizokwisha.Utasemaje unasikilizwa na wahuni tu ikiwa ndio genre pekee yenye kuzungumzia message? ni genre inayogusia maisha yetu ya kila siku,hip hop haipo kibiashara ila ipo kiharakati zaidi. Madee akumbuke kwamba ni hip hop ndio iliyowafanya Watz kupenda muziki wa kizazi kipya, bila hip hop asingekuwa anazungumzia hayo mafanikio anayoyazungumzia leo, ni hip hop ndio iliyowasafishia wao njia kufika hapo walipo, ni vyema akawaheshimu wanaofanya hip hop hata kama hawana mafanikio makubwa, at least they didn't sell their souls to the corporate like other artists did, they remained loyal to the hip hop roots wakiendeleza harakati. Without Diplomats, Niggaz With Matatizo,Mr II a.k.a II Proud a.k.a Sugu,Professor Jay bongo flava would never be the same.Thanks to em nigga!
Cha Kwanza unapaswa uelewe hip hop is not about business, ukiona msanii analalamika anachana hapati faida basi alikurupuka kuimba hakuzijua nguzo tano za hip hop.... hip hop is all about harakati ndugu, hivyo ni kama wahubiri injili au misikitini for free kufikisha neno la Mungu/Allah....ukiona mchungaji anakwambia kazi ya uchungaji hailipi au sheikh anakwambia hailipi changanya na zako utapata jibu....Joh makini ana mali gani sasa boss... we unayezijua unaweza zilinganisha na fame yake.... halafu kumbuka joh ni mmoja ya watu wachache wanaofanya muziki biashara..... tuje kwa hao wanaojiita wanasimamia misingi kama kina nicky mmbishi... kila siku wanalalamika mnawafollow insta ila hmataki hata kununua mixtape... upande wetu huku harmonize tu achana na manyangumi makubwa akitoa album, tshirt, show vyote tunalipia...
madee kawachana kweli masela wengi wanajifanya hiphop halafu wanataka vya bure
Wasanii wengi siku hizi wamegoma kutoa album wamebaki Taarabu,dansi na gospel tu,mapato yao makubwa yanatokana na show wanazopata na wengi hupata show baada ya video muziki wao kuonekana kwenye TV au Youtube.Kenya wao wanatoa album na wanauza vizuri (King Kaka,Sauti Sol,Octopizo wametoa album hivi karibuni)
Cha Kwanza unapaswa uelewe hip hop is not about business, ukiona msanii analalamika anachana hapati faida basi alikurupuka kuimba hakuzijua nguzo tano za hip hop.... hip hop is all about harakati ndugu, hivyo ni kama wahubiri injili au misikitini for free kufikisha neno la Mungu/Allah....ukiona mchungaji anakwambia kazi ya uchungaji hailipi au sheikh anakwambia hailipi changanya na zako utapata jibu....
Hivyo Madee ameropoka haijui hip hop
sema wewe hauna utamaduni wa kununua albam CD.Watanzania hatuna utamaduni wa kununua kazi za wasanii wetu iwe taarabu,dansi,bongo fleva,gospel au hip hop.Music wa sasa sio wa CD kina Diamond,Kiba,Yamoto Band lini walitoa CD?
kwani madee ka specify hiphop ya bongo tu?Mkuu mbona mbona unyamwezini wakina jay z, kanye, dr dre na drake wanapiga pesa ndefu sana
huu ndio UKWELI ambao WAHUNI na MACHIZI wengi hawawezi kuukubali ijapokuwa hawanunui kazi.Msanii wa muziki kutoka Tip Top Connection Madee amefunguka na kueleza ni kwanini wasanii wengi wa muziki wa Hip Hop nchini wanashindwa kufanya vizuri licha ya nyimbo zao kupendwa mitaani.
Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na video yake ya wimbo, Migulu Pande, ameiambia Times Fm kuwa Hip Hop inapendwa na kundi la ‘wahuni’ wachache na machizi mtaani ambao ni ngumu kwenda dukani kununua kazi anayoipenda.
Katika hatua nyingine, Mdee amesema kama yeye angeendelea kudumu na staili yake ya kurap kama zamani mpaka sasa, angekuwa amekwisha potea kwenye ‘Game’ na ulimwengu wa muziki.
“Watu wanataka changes, kama biashara haikulipi kwanini uendelee kufanya inakuingizia hasara kila kukicha, ningekuwa narap mpaka leo nisingekuwepo kwenye game ningepotea, dunia yenyewe inabadilika sasa kwa nini wewe usibadilike” alisema Madee.
View attachment 348466
kwanini sasa hamnunui kazi za wasanii au mnataka wafilisike mjiimbie wenyewe.kama ameamua kuuacha mziki wetu asitukashifu kwamba tunaoupenda ni wahuni na machizi atuheshimu huyo
Kwa USA mziki wowote ni business so automatically wasanii watakua wafanyabiashara cuz wanauza records. Pac alivyo sema ye ni businessman kwenye hiyo clip ilikua baada ya trial yake iliyo mhusisha na rape alivyo hojiwa na waandishi alitaka ku clarify mambo so akasema anachokiimba ili kiuze lazima atoe product mitaa inayotaka kusikia... So he was slinging words.mkuu movement ya Hiphop imechange... cha ajabu nyie bado mmeshikilia mambo ambayo hiphop ilikuwa ikifanya enzi za 1980's.... mara ngapi tumewasikia wanahiphop nguli wakiclaim kuwa wao ni Businessmen kuanzia 2pac na jay z...au labda na wenyewe hawajui maana ya hiphop kama madee...sasa hivi hiphop haipo tena kwenye kumkomboa mtu mweusi maana imeshasambaa kwa watu wote, iwe mchina , mzungu au mhindi..
Hiphop ni sanaa kama zilivyo sanaa zingine, kwahyo mtu anapoifanya kama kazi lazima tutegemee apate kipato kutokana na kazzi hiyo
mkuu, hapa sio unyamwezini...wahuni na machizi wa kule wana fedha za kutosha na wananunua kazi za wasanii tofauti na hapa bongo.Mkuu mbona mbona unyamwezini wakina jay z, kanye, dr dre na drake wanapiga pesa ndefu sana
yeah! ndio maana anairhangaa serikali kwa kutohalalisha bange.Afande Sele ni kielelezo tosha cha Muziki huo
sema wewe hauna utamaduni wa kununua albam
kwenyCD.e library yangu ninayo albam CD ya Asa - The Beautiful Imperfection, Guru- Jazzmatazz, KCK - Kid Can Kill, FM Academia - Chuki ya nini, Stopa - Mtu 3 ndani ya track moja.
So tukubali wanunuzi wa kazi za sanaa especially official albam ni watu wachache sana.