Madereva 47 kutoka Tanzania wameokolewa na M23, wakimbilia Rwanda Kusubiri Msaada wa ziada

WashaHost

Member
Joined
Jan 20, 2023
Posts
27
Reaction score
36
Magari ndo yameenda hivyo, Okoa roho gari boss atanunua jingine
Milioni 320 imeenda.
Nitairudishaje hiii!!??
Watanzania mkibanwa kwenye kodi,tozo,bei ya mafuta,bidhaa mbalimbali, basi mjue tunatafuta namna ya kurudisha hasara zetu!!
 
Mbona watz hua tuko nyuma kwenye uokoaji si Zima moto, majini Wala kuokoa mateka?
 
Chama cha Madereva wa Malori Tanzania (CHAKAMATA) kimesema kuwa madereva kadhaa kati ya waliokamatwa kwenye machafuko nchini DR Congo wamefanikiwa kuingia nchini Rwanda salama huku baadhi ya mali zao zikiporwa.

Kwa mujibu wa taarifa inasemekana zaidi ya madereva 40 wamekamatwa katika eneo la vita Goma huku jitihada zikiendelea kufanywa ili kuwaokoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…