Madereva bodaboda 759 wafariki dunia kwa ajali ndani ya miaka mitatu

Madereva bodaboda 759 wafariki dunia kwa ajali ndani ya miaka mitatu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Naibu Waziri wa Mambo ya ndani Mhe. Daniel Sillo amesema katika kipindi cha kuanzia mwaka 2022 hadi 2024 jumla ya wananchi 1,113 wamepoteza maisha kutokana na ajali zilizosababisha na pikipiki kwa mchanganuo ufuatao;

  • Madereva wa Pikipiki waliopata ajali na kufariki 759
  • Abiria waliopanda Pikipiki na kupata ajali na kufariki 283
  • Watu waliokuwa wanatembea kwa miguu kando kando ya barabara au njiani ama walikuwa wanavuka barabara na kupata ajali kwa kugongwa na pikipiki na kufariki dunia ni 71

 
A
Duh aiseee hatari sana
Au tuseme wale wanaosimamia Sheria wamewazira maana barabarani wameachwa waendeshe wanavyotaka,akiendesha kulia haya,akipakia abiria watatu haya,asipovaa helmet haya,asipoheshimu zebra crossing haya,akiendesha huku anaongea na kipoozeo haya,akipita barabara za waenda kwa miguu sawa,akiendesha amelewa haya,akiendesha spidi ya kukata shingo haya,mbaya zaidi wameunda majenge ya kuwatisha madereva wengine hata kuwapiga,kuwajeruhi na kuwaharibia vyombo vyao vyao usafiri .haya yanatendeka mbele ya wasimamizi wa Sheria za barabarani.sheria ni msumeno "wasiachwe inatosha Sasa"🤔
 
Back
Top Bottom