Madereva Taksi Mtandao (Bolt) wagoma, wataka ongezeko la nauli, Polisi waingilia kati

Madereva Taksi Mtandao (Bolt) wagoma, wataka ongezeko la nauli, Polisi waingilia kati

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mgomo mkubwa wa madereva wa taksi mtandao za mtandaoni za kampuni ya Bolt leo Oktoba 15,2024, mpaka yalipo makao makuu ya kampuni hiyo eneo la Morocco Kinondoni, wakishinikiza ongezeko la nauli.

Madereva wa Bolt wameandika malalamiko kuhusu ongezeko la makato ya kamisheni kutoka asilimia 15 hadi 25 kwa kila safari. Wanadai kuwa ongezeko hili linawatesa, huku wakisema madereva wa pikipiki na bajaj wakiathirika zaidi, wakati madereva wa magari wakikabiliwa na asilimia 15.

Vilevile, wameeleza wasiwasi kuhusu kushuka kwa bei za safari, wakisema kampuni inapaswa kuboresha huduma badala ya kushusha bei. Aidha, wamelalamikia usalama wao, wakisema kuwa taarifa zao muhimu ziko wazi, lakini abiria hawana wajibu wa kutoa taarifa za kutambulika, jambo linalowafanya wawe katika hatari.

Afisa mmoja wa Bolt ameeleza kuwa ndani ya saa 24, maamuzi kuhusu ongezeko la nauli na marekebisho ya kamisheni za madereva yatatolewa, kufuatia majadiliano yanayoendelea kati ya madereva na mwakilishi wa kampuni hiyo pamoja na mamlaka husika.
Pia, Soma:
+
Madereva Bolt Dar Waandamana Mpaka Ofisi za Bolt
+ Madereva waandamana kwenda LATRA wanataka Uber, Bolt wapandishe bei ya nauli
 
Mgomo mkubwa wa madereva wa taksi mtandao za mtandaoni za kampuni ya Bolt leo Oktoba 15,2024, mpaka yalipo makao makuu ya kampuni hiyo eneo la Morocco Kinondoni, wakishinikiza ongezeko la nauli.

Madereva hao wamelalamikia nauli za chini wanazolipwa na abiria, wakidai kuwa haziendani na gharama za uendeshaji, huku pia wakitaka kuongezwa kwa kamisheni zao.

Afisa mmoja wa Bolt ameeleza kuwa ndani ya saa 24, maamuzi kuhusu ongezeko la nauli na marekebisho ya kamisheni za madereva yatatolewa, kufuatia majadiliano yanayoendelea kati ya madereva na mwakilishi wa kampuni hiyo pamoja na mamlaka husika.
Pia, Soma:

+
Madereva Bolt Dar Waandamana Mpaka Ofisi za Bolt
+ Madereva waandamana kwenda LATRA wanataka Uber, Bolt wapandishe bei ya nauli
Kwani wamelazimishwa kufanya hiyo kazi?
 
Hivi Bolt wana gharama gani za uendeshaji mpaka wa demand 25%?

Kwanini madereva wetu wa vyombo vya usafiri wasiachane na hao kupe wakaendelea na utaratibu wetu wa zamani!
 
Akili za Mwanadamu zina maajabu sana. Ukiwa Posta Dsm unataka kwenda Kimara ukamfata Dereva Teksi atakupiga bei elfu 30. Cha ajabu dereva huyo huyo ukitumia Bolt atakupeleka kwa elf 15 na bado hiyo 15 atakatwa kamisheni ya 25% unabaki unajiuliza Hiiiiiiiiiii.
 
Mgomo mkubwa wa madereva wa taksi mtandao za mtandaoni za kampuni ya Bolt leo Oktoba 15,2024, mpaka yalipo makao makuu ya kampuni hiyo eneo la Morocco Kinondoni, wakishinikiza ongezeko la nauli.

Madereva wa Bolt wameandika malalamiko kuhusu ongezeko la makato ya kamisheni kutoka asilimia 15 hadi 25 kwa kila safari. Wanadai kuwa ongezeko hili linawatesa, huku wakisema madereva wa pikipiki na bajaj wakiathirika zaidi, wakati madereva wa magari wakikabiliwa na asilimia 15.

Vilevile, wameeleza wasiwasi kuhusu kushuka kwa bei za safari, wakisema kampuni inapaswa kuboresha huduma badala ya kushusha bei. Aidha, wamelalamikia usalama wao, wakisema kuwa taarifa zao muhimu ziko wazi, lakini abiria hawana wajibu wa kutoa taarifa za kutambulika, jambo linalowafanya wawe katika hatari.

Afisa mmoja wa Bolt ameeleza kuwa ndani ya saa 24, maamuzi kuhusu ongezeko la nauli na marekebisho ya kamisheni za madereva yatatolewa, kufuatia majadiliano yanayoendelea kati ya madereva na mwakilishi wa kampuni hiyo pamoja na mamlaka husika.
Pia, Soma:
+
Madereva Bolt Dar Waandamana Mpaka Ofisi za Bolt
+ Madereva waandamana kwenda LATRA wanataka Uber, Bolt wapandishe bei ya nauli
Mkuu ni Teksi siyo taksi. Hapa siyo Kenya bana.
 
Hilo ongezeko linaweza kuwa ni tozo za serikali ya CCM ndiyo limesababisha ongezeko la makato kutoka 15% hadi 25%, mitano tena kwa mama serikali yake inaupiga mwingi.

Au kama hamuafiki, basi tuandamane kwa ajili ya Maendeleo ya Watu ( kupitia ajira, ukulima, bolt, uvuvi n.k) pamoja na demokrasia ili sauti yetu kwa pamoja iwe Pipozz Pawa *People's Power.

Msisahau 2024 mchague chama mbadala ya chama dola kongwe
 
Hivi Bolt wana gharama gani za uendeshaji mpaka wa demand 25%?

Kwanini madereva wetu wa vyombo vya usafiri wasiachane na hao kupe wakaendelea na utaratibu wetu wa zamani!

Tozo, kodi, service charges n.k za Mwigulu Nchemba waziri wa hazina wa serikali ya chama dola kongwe
 
Bwada ya mgomo sasa wawakata pesa madreva kwa nguvu ,mfano mteja Ana request 6000 ikifika mwisho wa safari inaenda kuonekana mteja anatakiwA KULIPA 4000 ILA MAKATO WANAKATA KWENYE ILE 6000

WAnawakomoa kwanini wagomeee
 
Back
Top Bottom