Madereva taksi punguzeni u-bubu

Madereva taksi punguzeni u-bubu

RIGHT MARKER

Senior Member
Joined
Apr 30, 2018
Posts
129
Reaction score
473
Mhadhara - 39:
Kazi ya udereva TAXI ni biashara kama biashara nyingine. Ukiwa mfanyabiashara hupaswi kuwa bubu (mkimya) kupita kiasi. Halikadhalika udereva Taxi pia.

Leo natoa ushauri kwa madereva TAXI wote hasa waliopo kwenye mikoa yenye vivutio vya utalii kama vile Arusha, Dar, Zanzibar, Kilimanjaro, Mbeya, Tanga, Songwe, Pwani Bagamoyo, n.k, hata bodaboda pia wanaweza kutumia akili hii.

Kama wewe ni dereva Taxi unapokuwa na abiria hupaswi kuwa bubu (mkimya) ndani ya gari lako hata kama abiria hajui kuongea lugha yako jitahidi kutafuna lugha yake kadiri uwezavyo. Ukimya wako unaweza kuchelewesha riziki yako.

Haiwezakani umemchukua abiria Airport au bandarini anakwambia nipeleke hoteli fulani halafu wewe ndani ya gari umekuwa bubu mpaka unamfikisha hotelini. Unapaswa kuwa mchangamfu kwa kumtajia abiria vivutio vya utalii, maeneo makubwa ya starehe, nyumba kubwa za ibada na vinginevyo vilivyopo ndani ya mkoa wako huku ukimchombeza kuwa akihitaji usafiri wa kwenda kwenye maeneo hayo wewe upo kwa ajili hiyo. Hiyo ni mbinu mojawapo ya kuipigia debe kazi yako.

Bila shaka abiria uliyemchukua ni mgeni (kwa maana ya kwamba hafahamu maeneo ya kula bata na vivutio vilivyopo ndani ya mkoa). Kwa hiyo utakavyokuwa unamwelezea anaweza kuvutiwa kutembelea maeneo hayo, ucheshi na uchangamfu wako unaweza kumvutia akuchukue wewe kwa ajili ya kumzungusha.

MCHANGAMSHE ABIRIA WAKO: "Ndugu karibu sana kwenye mkoa wetu....Mkoa wetu ni mkubwa sana na una maeneo mazuri mengi ya kurelax pamoja na vivutio mbalimbali....kama vile majimoto, kimondo, mapango, fukwe nyingi za bahari za kupunga upepo, majengo ya wakoloni, mawe na mito ya ajabu, n.k...Ukihitaji kupelekwa huko mimi nipo naweza kukuachia business card yangu".​

Right Marker
Dar es salaam.
 
Nilijua tu ni madesa ya kupakua na kupest.

Katika usafiri wa kukodi siyo rahisi sana kumchombeza abiria.

Wengi wapo busy na simu na pia wengine wanahasira na kufoka kwamba umepita njia yenye foleni na hivyo bill itakuwa kubwa (Bolt&Farasi.

Unafika anakuuliza bei? Ukimtajia anang'aka mbona kubwa?

Yaani ni kununiana mwanzo mwisho.

Bolt wanashauri na kuelekeza kwamba dereva asiingilie mazungumzo wala kufanya mjadala na abiria kuhusu mada mbalimbali.
 
Mimi nadhani hayo aachwe abiria mwenyewe aulize kama atakuwa interested kuyajua,mtu ana stress zake kichwani amekuja mkoani kwako kwenye semina ya kikazi sometimes kuja kujadiliwa kama afukuzwe kazi au abaki halafu umletee habari za majimoto sijui mito na vimondo atakuelewa?

Huko ni kuchuriana na hakuna kitu sipendi kama nimekodi bodaboda au Bajaj halafu driver atake kunipigisha story njia nzima,yaani hela yangu initie kero?
 
Full nuno aisee.. Kwanza barabara za Daslam zilivyo na changamoto, huo muda wa stori ni finyu sana.

Hawajambo kwa Msuguri☺️
😂😂 watafune hata jojo basi,
Ila kwa bei zao zilivyo kubwa mnuno lazima uendelee

Huko nimehama kama wiki 2 zilizopita
 
😂😂 watafune hata jojo basi,
Ila kwa bei zao zilivyo kubwa mnuno lazima uendelee

Huko nimehama kama wiki 2 zilizopita

Mmmh! Ukahamia wapi?

Nitaweka jojo. Ila mbona huli jojo na wala hununi?

Kuna mmoja nilimbeba toka Sinza Mori to Big Bon-Kariakoo.

Mwanzo wa safari ilisoma elfu 7500. Kufika mwisho inasoma elfu 10 mia 5. Hii ilitokana na ruti aliyoichagua ya Bagamoyo road- via A. Mwinyi via Muhimbili na foleni ya Fire.

Aliguna mbona bei kubwa nikamwambia njia yako ndefu. Akalipa elfu 11 na change hakusubiri.
 
Mmmh! Ukahamia wapi?

Nitaweka jojo. Ila mbona huli jojo na wala hununi?

Kuna mmoja nilimbeba toka Sinza Mori to Big Bon-Kariakoo.

Mwanzo wa safari ilisoma elfu 7500. Kufika mwisho inasoma elfu 10 mia 5. Hii ilitokana na ruti aliyoichagua ya Bagamoyo road- via A. Mwinyi via Muhimbili na foleni ya Fire.

Aliguna mbona bei kubwa nikamwambia njia yako ndefu. Akalipa elfu 11 na change hakusubiri.
🤣🤣🤣tena bora nyie wa taxi mtandao wale wa kizamani wana bei za kitalii hao ni kuwanunia tu
 
Mhadhara - 39:
Kazi ya udereva TAXI ni biashara kama biashara nyingine. Ukiwa mfanyabiashara hupaswi kuwa bubu (mkimya) kupita kiasi. Halikadhalika udereva Taxi pia.

Leo natoa ushauri kwa madereva TAXI wote hasa waliopo kwenye mikoa yenye vivutio vya utalii kama vile Arusha, Dar, Zanzibar, Kilimanjaro, Mbeya, Tanga, Songwe, Pwani Bagamoyo, n.k, hata bodaboda pia wanaweza kutumia akili hii.

Kama wewe ni dereva Taxi unapokuwa na abiria hupaswi kuwa bubu (mkimya) ndani ya gari lako hata kama abiria hajui kuongea lugha yako jitahidi kutafuna lugha yake kadiri uwezavyo. Ukimya wako unaweza kuchelewesha riziki yako.

Haiwezakani umemchukua abiria Airport au bandarini anakwambia nipeleke hoteli fulani halafu wewe ndani ya gari umekuwa bubu mpaka unamfikisha hotelini. Unapaswa kuwa mchangamfu kwa kumtajia abiria vivutio vya utalii, maeneo makubwa ya starehe, nyumba kubwa za ibada na vinginevyo vilivyopo ndani ya mkoa wako huku ukimchombeza kuwa akihitaji usafiri wa kwenda kwenye maeneo hayo wewe upo kwa ajili hiyo. Hiyo ni mbinu mojawapo ya kuipigia debe kazi yako.

Bila shaka abiria uliyemchukua ni mgeni (kwa maana ya kwamba hafahamu maeneo ya kula bata na vivutio vilivyopo ndani ya mkoa). Kwa hiyo utakavyokuwa unamwelezea anaweza kuvutiwa kutembelea maeneo hayo, ucheshi na uchangamfu wako unaweza kumvutia akuchukue wewe kwa ajili ya kumzungusha.

MCHANGAMSHE ABIRIA WAKO: "Ndugu karibu sana kwenye mkoa wetu....Mkoa wetu ni mkubwa sana na una maeneo mazuri mengi ya kurelax pamoja na vivutio mbalimbali....kama vile majimoto, kimondo, mapango, fukwe nyingi za bahari za kupunga upepo, majengo ya wakoloni, mawe na mito ya ajabu, n.k...Ukihitaji kupelekwa huko mimi nipo naweza kukuachia business card yangu".​

Right Marker
Dar es salaam.
IA imefanya kazi nzuri.
 
Back
Top Bottom