Madereva, ushauri huu mnaukubali?

Madereva, ushauri huu mnaukubali?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Katika elimu za kidunia za kujihami na majanga mbali mbali tuwapo barabarani, kuna baadhi ya wazee wanashauri hili:-​
  • Iwapo upo kwenye gari na ghafla ukaona mtu unayemfahamu amekatisha ghafla kwa mbele, akiwa amekuwekea mazingira ya wewe umkwepe au ufunge breki ghafla; wanashauri ni bora umpitie ili kuepusha ajali, kwa sababu ukimkwepa tu, au ukafunga breki, lazima utasababisha ajali na watu watakufa; wanasema yale ni mauza uza ya barabarani.​
  • Iwapo ulienda sehemu (mtaalamu) kwa ajili ya kutafuta mali, mamlaka n.k na ukaambiwa kuna vitu vitatokea; na kwa ghafla ukiwa barabarani ukakutana na mfanano wa ndugu au mtu unayemfahamu au kitu chochote kile, ukikipitia utakuwa umefaulu mtihani; ukikikwepa hutopata ajali zaidi ya kufeli mtihani.​

Kwa hiyo, kama hujawahi kwenda popote mara ghafla kitu kiko barabarani, kanyaga kwa usalama wako na uliowapakia.

Karibu kwa maoni.​
 
Hizi story ni zimetokea kushushwa na kupendwa Afrika.. Mtu unaendesha umechoka na usingizi juu umeanza kuota. Umestuka unasingizia umetumiwa jini.. Hivi sisi Waafrika ndio tujikute wataalamu sana wa uchawi?
 
Back
Top Bottom