KERO Madereva wa Magari ya Mizigo tumekwama mpaka wa Malawi na Tanzania kwa wiki 2, tunawasubiri NEMC

KERO Madereva wa Magari ya Mizigo tumekwama mpaka wa Malawi na Tanzania kwa wiki 2, tunawasubiri NEMC

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mwanongwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2023
Posts
611
Reaction score
567
photo_2024-12-06_11-16-17.jpg
Mimi ni mmoja wa madereva wa magari makubwa ya mizigo, pia ni mmoja wa waathirika wa changamoto ya mkwamo wa magari ambayo imetokea Kasumulu eneo la mpakani kati ya Malawi na Tanzania.

Kwa muda wa takriban wiki mbili magari yetu ambayo ambayo yana mizigo ya skrepa kutoka Malawi kwenda Uganda na Rwanda yamezuiwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa sababu ambazo hazieleweki.

Ni kama NEMC wamekuwa wakitufanyia figisu ili magari yetu yasitoke eneo hili.

Mara ya kwanza NEMC walituzuia tusiingie Tanzania wakitaja sababu za kimazingira.

Baada ya kukaa vikao vyao walituruhusu kuingia Tanzania kwa sharti la kwamba, kwa wale madereva ambao mizigo yao ya skrepa imefunikwa na turubai watatakiwa walipe kiasi cha Shilingi Milioni 1, wale ambao mizigo yao imepakiwa kwenye kontena au box body watatakiwa kulipa laki mbili na nusu.
photo_2024-12-06_11-16-50.jpg
Baada ya kulipia, NEMC wakatuambia watatakiwa kutupa escort ili kusindikiza misafara yetu huko tuendako lakini kwa wiki mbili sasa tumeisubiri hiyo escort kutoka NEMC na hamna kitu imefanyika.

Tukiwapigia simu wanasema watakuja lakini hawaji. Yaani hapa kuna gari zaidi ya 50 zimekwama tunasubiri hiyo escort kutoka NEMC. Gari zinazokwenda Uganda ni nyingi zaidi ambazo zimezuiwa.

Hata documents kutoka watu wa custom ziko tayari ila NEMC wamezuia tukisubiri hiyo escort.

Muda unakwenda, gharama zinapanda na sababu za maana hatupewi. Tunaomba Serikali iingilie kati tuweze kuruhusiwa.

Pia, soma; √ - NEMC: Hatujakataa kusindikiza Taka hatarishi kutoka Malawi kwenda Uganda, Bali Wakala ndiye kachelewa kulipia. Madereva wawasiliane na Wakala wao
photo_2024-12-06_11-16-49.jpg

photo_2024-12-06_11-16-47.jpg

photo_2024-12-06_11-16-43.jpg
 
Baada ya kukaa vikao vyao walituruhusu kuingia Tanzania kwa sharti la kwamba, kwa wale madereva
Viongozi wa juu amri zao zinapuuzwa na kusinginwa kwa kiasi kijubwa na watendaji mpakani pamoja na NEMC

Toka maktaba:

10 September 2024
Kasumulu, Tanzania

AMRI YA RAIS KUPITIA WAZIRI YAFIKISHWA NA RC HOMERA

RC HOMERA AFIKA BODA YA KASUMULU KUTATUA CHANGAMOTO YA MADEREVA WA MALORI 46, AMTAJA RAIS SAMIA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt:Samia Suluhu Hassan amewafutia Adhabu(Faini) Madereva wa Malori 46 Walioshikiliwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira(NEMC) Mpakani mwa Tanzania na Malawi(Border ya Kasumulu) kwa Kosa la Kusafirisha Vyuma chakavu pasipo Kufuata Utaratibu.

Akizungumza kwa niaba ya Dkt: Samia Suluhu Hassan leo akiwa mpakani border hapo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Cde: RC Juma Z. Homera amesema Rais Samia kaamua kufanya hivyo kutokana na roho yake ya upendo kwa Watanzania hasa Vijana wanaojitafutia riziki kwaajiri ya kuzitunza Familia zao.


View: https://m.youtube.com/watch?v=bhcrWu03mCk
 
Back
Top Bottom