Madhara ya usingizi wa kiroho

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
1,497
Reaction score
2,681
1. Unasababisha umasikini

Mithali 6:9-11
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?

10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!

11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang'anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.

2. Kuibiwa na kupoteza watu wa muhimu, vitu vya muhimu na fursa za muhimu

1 Wafalme 3:20-21

20 Akaondoka kati ya usiku, akamwondoa mtoto wangu ubavuni pangu, mimi mjakazi wako nilipokuwa usingizini, akamweka kifuani pake, na mtoto wake mwenyewe, aliyekuwa amekufa, akamweka kifuani pangu.

21 Nilipoondoka asubuhi nimnyonyeshe mtoto wangu, kumbe? Amekufa. Hata asubuhi nilipomtazama sana, kumbe! Siye mtoto wangu niliyemzaa.

3. Hufungua Mlango wa adui kupanda mbegu za uovu

Mathayo 13:25
lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

4. Ukilala usingizi kiroho unakosa ulinzi dhidi ya nguvu za Giza

1 Samweli 26:7

Basi Daudi na Abishai wakawaendea watu usiku; na tazama, Sauli alikuwapo kati ya magari amelala usingizi, na fumo lake limechomekwa chini, karibu na kichwa chake; naye Abneri na watu wake wamelala wakimzunguka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…