Madini yaliyopo kwenye hifadhi nadhani tuyaache kwa sasa

Madini yaliyopo kwenye hifadhi nadhani tuyaache kwa sasa

senzighe

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2012
Posts
2,108
Reaction score
1,666
Ni kama nimesikia kwamba tufikirie kuanza kuchimba madini yaliyopo katika baadhi ya hifadhi zetu.

Hoja haipingwi kwa kupigwa rungu lakini nilikuwa nadhani tufikirie na yatokanayo baada ya kuanza kuvamia hizi mbuga na kuanza kufukua chini.

Huenda ikawa mazingira tuliyoyapigania kwa muda mrefu na kuifanya Tanzania kuwa kivutio yakaporomoka na kuharibiwa na kuifanya Tanzania isiwe ya kuvutia tena.

Ni kweli kabisa na hili halina shaka kwamba Simba na Tembo huwa hawali madini yaliyop chini ardhini lakini hakuna shaka vilivile kwamba vilivyopo juu ya ardhi vina thamani tena endelevu.

Kwa sasa tuendelee tu na madini yaliyopo nje ya hifadhi kwani ni mengi tu na hayaishi leo na hata hivyo kuna changamoto nyingi ambazo hatujazitatua za madini yanayochimbwa katika maeneo mengine nje ya hifadhi.

Tujikite kwanza huko,tuache kwenda mbio.
 
Mama hajasema tuanze kuyachimba. Amewapa wataalamu wafanye uchambuzi faida na hasara yakichimbwa na yasipochimbwa then washauri kwa serikali. Acha kupotosha.
 
Nyie yaacheni tu , halafu kuna boya atakuja ayapige bei chap 😋😋 mtaanza kujilaumu tena.
 
Mbona bwawa la umeme limejengwa kwenye hifadhi?
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Myaache ili iwaje? Acheni ujinga huo wa kujisifu nina hiki nina kile halafu hunufaiki nacho , uza madini jenga miundombinu ya umeme na maji , yanini sasa yaendelee kukaa hapo aridhini? kwani ni mbegu hizo kwamba mmepanda mnasubiri ziote
 
Back
Top Bottom