Madiwani wa Chadema wawekwa kitimoto kwa kukisaliti chama

Madiwani wa Chadema wawekwa kitimoto kwa kukisaliti chama

Mshume Kiyate

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2011
Posts
6,764
Reaction score
896
CHADEMA imewaweka kitimoto madiwani wake watatu wa Manispaa ya Arusha kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho katika hoja ya kumtambua meya wa jiji hilo, Gaudence Lyimo.
Habari zilieleza kuwa madiwani hao walijadiliwa katika kikao kilichofanyika kwenye hoteli ya Bristol chini ya mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe na katibu mkuu Dk Willibrod Slaa. Baada ya kukiri makosa hayo katika kikao hicho kilichofanyika Machi 24 mwaka huu, madiwani hao waliomba radhi kwa maandishi na kuahidi kutorudia kitendo hicho kilichochukuliwa kama usaliti wa chama.
Taarifa zimewataja madiwani hao kuwa pamoja na diwani wa kata ya Sekei, Chrispine Tarimo, diwani wa kata ya Eunutoto, Elbariki Malley na diwani viti maalumu, Rehema Mohamed. diwani Tarimo alisomewa tuhuma za kukisaliti chama kuhudhuria kikao cha kamati ya Elimu,Afya na uchumi. Elbariki yeye alisomewa tuhuma za kuambatana na Meya wa Arusha kwenye ziara ya kutembelea ujenzi wa barabara.
Source: Mwananchi Machi 29, 2011
 
Ni kweli maendeleo yanahitajika kwenye kata zetu, lakini msisitizo ni kwamba suala la umeya lazima litolewe ufumbuzi kwanza, maana ndiyo linalobeba sura halisi ya Demokrasia Arusha!
Kukiuka msimamo wa pamoja ni Usaliti, wanastahili hatua za kinidhamu!
 
Kizuri na cha muhimu ni kutambua makosa yao

Hili ndilo ambalo wanasiasa wengi sasa hivi haweatambui, wanajoina vichwa ngumu

Safi sana madiwani na hongereni viongozi wa CDM kwa ujasiri wa kuwachukulia hatua wanaopinda kwenye mstari...

hili litakipa chama uimara na sio kuchekacheka na wanaoharibu chama kama jamaa yangu fulani hivi aliegeuza chama jalala kwa kusomba kila kundi la watu...wasaliti wamo, wanga wamo, wezi wamo, viriba timba vimejaa kibao humo...kama kokoro lisilochagua cha kuvua
 
mimi nadhani ni vema walasusia vikao vinavyoendeshwa na meya lakini vya kamati ni vema wakaingia wananchi waliwachagua wakawe madiwani sio meya , siasa zenu mauti ya wananchi wa jiji la arusha
 
tofauti za chama zinajadiliwa na vikao sio magazeti. keep it up CHADEMA
 
Ni kweli maendeleo yanahitajika kwenye kata zetu, lakini msisitizo ni kwamba suala la umeya lazima litolewe ufumbuzi kwanza, maana ndiyo linalobeba sura halisi ya Demokrasia Arusha!
Kukiuka msimamo wa pamoja ni Usaliti, wanastahili hatua za kinidhamu!
Safi sana huo ndio ukweli wenyewe.
 
mwenzenu mtoa mada amejipinda kweli kuiandika hii ili wale mapro CCM waje na comment za kejeri matokeo yake thread imemdodea, pole chatu dume, kwani huwa hampigiani simu na akina maji mshindo, kupen'ge, kashaga, nduka & co? maana labda wenzako leo hawajaingiziwa bado mgawo wenu wa internet bundle, maana Makamba anahisi kazi mliopewa haina tija kwenye forum ya wasomi, zaidi zaidi mnakitia hasara chama tu, na siku hizi ruzuku imepunguwa
 
mwenzenu mtoa mada amejipinda kweli kuiandika hii ili wale mapro CCM waje na comment za kejeri matokeo yake thread imemdodea, pole chatu dume, kwani huwa hampigiani simu na akina maji mshindo, kupen'ge, kashaga, nduka & co? maana labda wenzako leo hawajaingiziwa bado mgawo wenu wa internet bundle, maana Makamba anahisi kazi mliopewa haina tija kwenye forum ya wasomi, zaidi zaidi mnakitia hasara chama tu, na siku hizi ruzuku imepunguwa

Rev Masanilo mbona unaangaika hivyo, mimi ni Intependent thinker hiyo ni juu yako wewe kuongea unachojisikia msalimie sana Max nsimba
 
Rev Masanilo mbona unaangaika hivyo, mimi ni Intependent thinker hiyo ni juu yako wewe kuongea unachojisikia msalimie sana Max nsimba
This in unwanted person here.
Nijuavyo mimi chadema ni chama cha kiimla. wote lazima mfyate mkia. I will never be ready. Ukiwa kiongozi basi wewe ndo mwenye akili kuliko wachini yako na wala hukosei kama malaika. kama jeshini vile!
 
Back
Top Bottom