mhuogomkavu
Senior Member
- Jun 23, 2017
- 116
- 102
Kwanza niwape pole kwa mnayoyapitia tangu mwaka 2016 baada ya kuingia uongozi mpya kwenye Shirikisho la Riadha.
Ninafahamu walio wengi hawatafahamu nini kinachoendelea ndani ya Riadha Tanzania kwani wengi wamejikita kwenye michezo mingine.
Ni hivi, tangu aingie madarakani Rais wa Riadha Tanzania Anthony Mtaka style yake ya kuongoza imekuwa ni ya kupiga deal. Nafahamu huko kwenye Ukuu wa Mkoa anapewa heshima na watu ila masikini hawajui ya kwenye riadha tunateseka.
Nilikuwa naongea na wanariadha fulani, ni mateso makubwa na ufisadi wa kutisha huko. Natamani haya majipu yamulikwe haraka na tutapike nyongo zote mwaka huu kabla haujaisha
Hawa viongozi wa Shirikisho wanalifanya Shirikisho kama Taasisi binafsi mpaka kufikia hatua ya kukataa kutumia Ofisi halali iliyopo katika Uwanja wa Taifa karibu na Uwanja Taifa lakini wao wanataka wafuatwe kwenye Ofisi zao! Viongozi wengine wanapohitaji fedha za kuendesha shughuli za Shirikisho wanajua wanachokifanya. Ni maumivu makubwa sana!!
Rais wa Shirikisho bwana Anthony Mtaka na Makamu wake William Kallaghe inafikia wakati mnashinikiza baadhi ya viongozi wa Riadha Tanzania kuandaa ripoti za matumizi za uongo au hewa ilimradi tu fedha hizo zionekane zimetumika kumbe wamezitia ndani. Mtakumbuka alichofanyiwa Katibu Mkuu aliyejiuzulu bwana Willhelm Gidabuday ambaye alilazimishwa kuandaa ripoti ya matumizi ya Tshs milioni 87 ilihali hakuna matumizi ya aina hiyo. Muulizeni Gidabuday popote alipo. Alitaka kuongea na Waandishi wa Habari kuonyesha wizi huu ila alizuiwa
Nakumbuka ujumbe wake kuita wanahabari baadae akasema ana matatizo ya kifamilia. Nakumbuka aliandika hivi wakati anaahirisha;
“TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI ;
YAH: KUAHIRISHA KWA PRESS CONFERENCE
Ndg Wanahabari,
Napenda kuwajulisha kuwa NIMEAHIRISHA KWA MUDA kile nilichopanga kuzungumza Nanyi kesho Alhamisi March 5/2020 kutokana na dharura ya kifamilia.
Hadi hapo mtakapojulishwa.
Ahsanteni.
Wilhelm F. Gidabuday.”
Sijui ni nani alimkingia kifua Anthony Mtaka🤔 na sijui huyu Gidabuday yupo wapi na mafaili haya ya ubadhilifu!
Nakumbuka pia mwaka 2017 ilikuwa mwezi Machi kama sikosei Wanariadha walishiriki Mashindano ya Dunia ya Mbio za Nyika nchini Uganda lakini baada ya kurudi nchini Mtaka na genge lake badala ya kuwapongeza alimporomesha matusi Gidabuday kisa amewalipa Wanariadha na Makocha stahiki zao. Je, huo ndo utumishi mwema kweli? Hivi watu huko nje ya Ukuu wa Mkoa wanajua mateso haya tunayopata? Huyu anastahili madaraka zaidi au ndio atatumaliza? Kama hivi tu tunaumizwa hivi kwa mfano akaelekea kwenye zile ndoto anazozitaka tutapona kweli?
Tena haitoshi wakati Wanariadha wakiwa Uganda nakumbuka Anthony Mtaka Ulipeleka ujumbe wako kuwavuruga wanamichezo kule. Ushahidi nitauleta muda si mrefu! Haya mambo tumechoshwa nayo. Rudi ukawe mkuu wa Mkoa wa Simiyu utuachie Shirikisho.
Juzi juzi hapa baada ya kuona Dodoma wamefanya Marathon nikakumbuka Washindi wa Mbio za Dodoma Hapa Kazi Marathon kukuzonga kwa miaka minne tangu 2016 hadi 2019 wakidai zawadi zao, ukaona uwaite Arusha Wanariadha, Makocha na viongozi wa Arusha kwenye Baa moja maarufu, bila kumjulisha Katibu Mkuu ukawagawia fedha kwa walioenda Uganda na wale waliokuwa wanadai Mabati. Na fedha ulizowalipa zilitoka kwenye mfuko maalum wewe unaujua. Hizo pesa zilikuwa na matumizi mengine ila wewe ukazichepusha. Kama unabisha, tupe taarifa za matumizi ya pesa za Shirikisho☹️. Miaka 4 hujawahi kuandika ripoti ya matumizi ya pesa na bado unataka kuitwa kiongozi muadilifu! Mikutano haifanyiki na umejificha kwenye kichaka cha utendaji mzuri serikalini ila kwenye Riadha mambo yanaharibika.
Fedha zimekuwa zikiingizwa kwenye Shirikisho bila taarifa rasmi na zinatolewa. Hivi zile pesa zaidi ya milioni 20 tulizopewa na Tanesco zilizokuwa kule Benki ya Azania historia yake ipoje na ziko wapi?
Bwana Mtaka anatumia kofia yake ya Mkuu wa Mkoa kuitisha vikao vya Shirikisho na kuanza kuwajadili viongozi ambao wanakwenda kinyume na matakwa yake hata kama wako sahihi. Mara nyingi anawatisha kwa kutumia wadhifa wake na hata wajumbe wengine wanaogopa kumpinga ndio maana mnaona tupo kimya kwa muda mrefu. Sasa basi!
Hivi kweli Uongozi wa riadha hautaki kuwalipa Wanariadha wanaodai zaidi ya Tshs. 6,000,000/= tangu mwaka 2015!!!!! 😳Tena wanariadha hawa walifanya vizuri sana kwenye Mbio za Nyika za Dunia Beijing na wengine walioahidiwa motisha baada ya kufanya vizuri kwenye Kilimanjaro Marathon‼️
Ndugu zangu, kiukweli Riadha Tanzania tuna Viongozi wanaokatisha tamaa, Viongozi ambao wanajali maslahi yao na kutumia shirikisho kama sehemu ya kujitengenezea fedha.
Huu ni wakati wa kufanya mabadiliko makubwa. Tusiogope!
SERIKALI TUNAOMBA SIKIENI KILIO HIKI MAANA TUNAUMIZWA SANA🙏
Ninafahamu walio wengi hawatafahamu nini kinachoendelea ndani ya Riadha Tanzania kwani wengi wamejikita kwenye michezo mingine.
Ni hivi, tangu aingie madarakani Rais wa Riadha Tanzania Anthony Mtaka style yake ya kuongoza imekuwa ni ya kupiga deal. Nafahamu huko kwenye Ukuu wa Mkoa anapewa heshima na watu ila masikini hawajui ya kwenye riadha tunateseka.
Nilikuwa naongea na wanariadha fulani, ni mateso makubwa na ufisadi wa kutisha huko. Natamani haya majipu yamulikwe haraka na tutapike nyongo zote mwaka huu kabla haujaisha
Hawa viongozi wa Shirikisho wanalifanya Shirikisho kama Taasisi binafsi mpaka kufikia hatua ya kukataa kutumia Ofisi halali iliyopo katika Uwanja wa Taifa karibu na Uwanja Taifa lakini wao wanataka wafuatwe kwenye Ofisi zao! Viongozi wengine wanapohitaji fedha za kuendesha shughuli za Shirikisho wanajua wanachokifanya. Ni maumivu makubwa sana!!
Rais wa Shirikisho bwana Anthony Mtaka na Makamu wake William Kallaghe inafikia wakati mnashinikiza baadhi ya viongozi wa Riadha Tanzania kuandaa ripoti za matumizi za uongo au hewa ilimradi tu fedha hizo zionekane zimetumika kumbe wamezitia ndani. Mtakumbuka alichofanyiwa Katibu Mkuu aliyejiuzulu bwana Willhelm Gidabuday ambaye alilazimishwa kuandaa ripoti ya matumizi ya Tshs milioni 87 ilihali hakuna matumizi ya aina hiyo. Muulizeni Gidabuday popote alipo. Alitaka kuongea na Waandishi wa Habari kuonyesha wizi huu ila alizuiwa
Nakumbuka ujumbe wake kuita wanahabari baadae akasema ana matatizo ya kifamilia. Nakumbuka aliandika hivi wakati anaahirisha;
“TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI ;
YAH: KUAHIRISHA KWA PRESS CONFERENCE
Ndg Wanahabari,
Napenda kuwajulisha kuwa NIMEAHIRISHA KWA MUDA kile nilichopanga kuzungumza Nanyi kesho Alhamisi March 5/2020 kutokana na dharura ya kifamilia.
Hadi hapo mtakapojulishwa.
Ahsanteni.
Wilhelm F. Gidabuday.”
Sijui ni nani alimkingia kifua Anthony Mtaka🤔 na sijui huyu Gidabuday yupo wapi na mafaili haya ya ubadhilifu!
Nakumbuka pia mwaka 2017 ilikuwa mwezi Machi kama sikosei Wanariadha walishiriki Mashindano ya Dunia ya Mbio za Nyika nchini Uganda lakini baada ya kurudi nchini Mtaka na genge lake badala ya kuwapongeza alimporomesha matusi Gidabuday kisa amewalipa Wanariadha na Makocha stahiki zao. Je, huo ndo utumishi mwema kweli? Hivi watu huko nje ya Ukuu wa Mkoa wanajua mateso haya tunayopata? Huyu anastahili madaraka zaidi au ndio atatumaliza? Kama hivi tu tunaumizwa hivi kwa mfano akaelekea kwenye zile ndoto anazozitaka tutapona kweli?
Tena haitoshi wakati Wanariadha wakiwa Uganda nakumbuka Anthony Mtaka Ulipeleka ujumbe wako kuwavuruga wanamichezo kule. Ushahidi nitauleta muda si mrefu! Haya mambo tumechoshwa nayo. Rudi ukawe mkuu wa Mkoa wa Simiyu utuachie Shirikisho.
Juzi juzi hapa baada ya kuona Dodoma wamefanya Marathon nikakumbuka Washindi wa Mbio za Dodoma Hapa Kazi Marathon kukuzonga kwa miaka minne tangu 2016 hadi 2019 wakidai zawadi zao, ukaona uwaite Arusha Wanariadha, Makocha na viongozi wa Arusha kwenye Baa moja maarufu, bila kumjulisha Katibu Mkuu ukawagawia fedha kwa walioenda Uganda na wale waliokuwa wanadai Mabati. Na fedha ulizowalipa zilitoka kwenye mfuko maalum wewe unaujua. Hizo pesa zilikuwa na matumizi mengine ila wewe ukazichepusha. Kama unabisha, tupe taarifa za matumizi ya pesa za Shirikisho☹️. Miaka 4 hujawahi kuandika ripoti ya matumizi ya pesa na bado unataka kuitwa kiongozi muadilifu! Mikutano haifanyiki na umejificha kwenye kichaka cha utendaji mzuri serikalini ila kwenye Riadha mambo yanaharibika.
Fedha zimekuwa zikiingizwa kwenye Shirikisho bila taarifa rasmi na zinatolewa. Hivi zile pesa zaidi ya milioni 20 tulizopewa na Tanesco zilizokuwa kule Benki ya Azania historia yake ipoje na ziko wapi?
Bwana Mtaka anatumia kofia yake ya Mkuu wa Mkoa kuitisha vikao vya Shirikisho na kuanza kuwajadili viongozi ambao wanakwenda kinyume na matakwa yake hata kama wako sahihi. Mara nyingi anawatisha kwa kutumia wadhifa wake na hata wajumbe wengine wanaogopa kumpinga ndio maana mnaona tupo kimya kwa muda mrefu. Sasa basi!
Hivi kweli Uongozi wa riadha hautaki kuwalipa Wanariadha wanaodai zaidi ya Tshs. 6,000,000/= tangu mwaka 2015!!!!! 😳Tena wanariadha hawa walifanya vizuri sana kwenye Mbio za Nyika za Dunia Beijing na wengine walioahidiwa motisha baada ya kufanya vizuri kwenye Kilimanjaro Marathon‼️
Ndugu zangu, kiukweli Riadha Tanzania tuna Viongozi wanaokatisha tamaa, Viongozi ambao wanajali maslahi yao na kutumia shirikisho kama sehemu ya kujitengenezea fedha.
Huu ni wakati wa kufanya mabadiliko makubwa. Tusiogope!
SERIKALI TUNAOMBA SIKIENI KILIO HIKI MAANA TUNAUMIZWA SANA🙏