Maduka mengi yaendelea kufungwa Kariakoo, Jumanne ya Juni 25, 2024

Maduka mengi yaendelea kufungwa Kariakoo, Jumanne ya Juni 25, 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Licha ya kuripotiwa kuwepo kwa suluhu kwenye baadhi ya madai ya Wafanyabiashara waliyowasilisha Serikalini na kufanyika kikao cha pamoja lakini mpaka kufikia Saa tatu Asubuhi hali ya mgomo inaonekana kuendelea maeneo ya Kariakoo ambapo maduka mengi yameendelea kufungwa.

Itakumbukwa kwamba jana June 24, 2024, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa wito kwa Wafanyabiashara wa Kariakoo kufungua maduka yao na kuwataka wasitishe mgomo.

Hata hivyo alidai Serikali inaweza kuweka ulinzi eneo la Kariakoo hata kwa mwezi mzima, kama wataamua kutofungua maduka mpaka madai yao yatakapopatiwa majawabu.

photo_2024-06-25_08-57-19.jpg

photo_2024-06-25_08-43-48.jpg

photo_2024-06-25_08-43-46.jpg

photo_2024-06-25_08-43-45.jpg
 
Serikali inaumiza Wananchi aisee, sijui shida kubwa iko wapi? Wakati wa kampeni huwa wanatuahidi pepo lakini wakishakalia uongozi wananchi huwa tunaishi maisha ya jehanam, ifikie wakati Serikali iache blah blah kwenye mambo ya nayo gusa Watu.
 
Licha ya kuripotiwa kuwepo kwa suluhu kwenye baadhi ya madai ya Wafanyabiashara waliyowasilisha Serikalini na kufanyika kikao cha pamoja lakini mpaka kufikia Saa tatu Asubuhi hali ya mgomo inaonekana kuendelea maeneo ya Kariakoo ambapo maduka mengi yameendelea kufungwa.

Itakumbukwa kwamba jana June 24, 2024, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa wito kwa Wafanyabiashara wa Kariakoo kufungua maduka yao na kuwataka wasitishe mgomo.

Hata hivyo alidai Serikali inaweza kuweka ulinzi eneo la Kariakoo hata kwa mwezi mzima, kama wataamua kutofungua maduka mpaka madai yao yatakapopatiwa majawabu.

Mungu awabariki muendelee kuyafunga kwani hasara ni za kwenu sisi tunasubiri marejesho tu mkishindwa tunakamata dhamana.
 
Safi sana wafanyabiashara.shikilieni hapohapa Hadi bibi chura aje mwenyewe atengue Sheria kandamizi zilizopitishwa na bunge kibogoyo.
 
Safi sana wafanyabiashara.shikilieni hapohapa Hadi bibi chura aje mwenyewe atengue Sheria kandamizi zilizopitishwa na bunge kibogoyo.
😂😂😂
Kwake hii ngoma ni nzito na kwa jinsi alivyopoteza mvuto watu hawatamuelewa kama vipi hili jambo lifanywe la kitaifa, Aende Lissu na Juma Duni Haji wakazungumze na Wafanyabiashara nadhani wataelewa. Japo hii serikali yetu sasa hivi imekosa kabisa ushawishi. Wawatumie hata Viongozi wa Vyama pinzani. Kwani tunajenga nchi moja
 
Safi, hii ni ishara nzuri ya kuonesha ukomavu na msimamo dhahiri kwa wafanyabiashara.
Hii nchi haiwezi kwenda kwa maneno bila vitendo.
Siasa uchwara zimezidi kwenye maisha ya watu.
Ni muda sasa wa viongozi kusikiliza na kuzitafutia suluhisho chanya hoja za wafanyabiashara
 
Safi, hii ni ishara nzuri ya kuonesha ukomavu na msimamo dhahiri kwa wafanyabiashara.
Hii nchi haiwezi kwenda kwa maneno bila vitendo.
Siasa uchwara zimezidi kwenye maisha ya watu.
Ni muda sasa wa viongozi kusikiliza na kuzitafutia suluhisho chanya hoja za wafanyabiashara
Msiwashabikie hao wanapoteza muda wa kufanya biashara.kufa kufanana wamachinga pigeni kazi huu ni muda mwafaka kwenu kutengeneza faida.
 
Uhalisia
 

Attachments

  • FB_IMG_17186935862077137.jpg
    FB_IMG_17186935862077137.jpg
    405.7 KB · Views: 1
Back
Top Bottom