WANDUGU, DOGO anataka kufungua duka la dawa phamacy kigamboni hapo, na ninafahamu kuna uvumi wa dawa bandia nyingi mtaani. mimi pia nitatia mguu kumsapoti, hivi kwa hapa dsm, ni maduka gani ya jumla ninaweza kupata dawa ambazo nina uhakika ni genuine na kwa bei nzuri. pia, dawa nyingine tunauziwa tunaona zimetoka india, UK etc, je, watu wanafuata kununua kulekule au kuna branch zao hapa bongi. kuna viwanda vya madawa vingine kama shellys vya hapa dsm, je, unaponunua unawafuata kiwandani au wana maduka yao.
kwa mwenye uelewa na biashara hii naomba tujadili kwa faida ya wote. asanteni.