Maelezo ya kina kuhusu Uber. Usafiri salama na wa bei ya chini kwa mtanzania

Habari zenu wadau, binafsi mimi ni mwajiriwa katika auditing firm ila naona kuna plenty of opportunities za kutengeneza more money kwenye market.

Nimesikia sana kutoka kwa raia mbalimbali kuhusu jinsi gani biashara ya transport through UBER inavyolipa.

Nimeambiwa per day unaweza hata tengeneza hata laki kabla ya makato mengine kama mafuta na posho ya dereva.

Wazo likanijia la kukusanya mtaji ninunue chombo cha usafiri nifanye hii kitu. Ila ningependa kujua mwenye more insight kwenye hii biashara.

Je, market ikoje kwa sasa compared na zamani? Is it worth it? Natamani nisikie maoni yenu tafadhali. Asante!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Posta to makumbusho 4000/= na A/c Juu
Sio rahisi

Sent using Jamii Forums mobile app
Ulitaka iwe kiasi gani ili ikulipe?,tatizo letu wa Africa tunapenda sana shortcut,kwaiyo ulitaka Posta to Makumbusho iwe Tsh 15,000/-,nani atapanda izo Uber kwa kipato gani cha mtanzania wa kawaida,elewa na market ya watu unaofanya nao biashara ni kina nani,hawa watanzania wengi wana nyota ya daradara,leo hii mtu atoe 15 elfu toka Makumbusho to Posta ana wazimu!!?,bei hizo kuwa ndogo ni ili kuendana na uchumi wenu vile vile ushindani,kwaiyo ili kuendana na ushindani uliopo kampuni zina shusha bei kwa abiria ili abiria wawe wengi,hiyo hiyo Uber sometime bei huongezeka kutokana na mahitaji ya magari wakati huo,kama biashara ingekua hailipi Uber zisingekuwepo mtaani,faida ipo ila siyo super profit kama zamani!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeendesha taxify kwa miezi mitatu. Nachoweza kusema ni kwamba hii biashara ilikua na faida ilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2017.

Hivi sasa imekua "Saturated". Maana yake ni kwamba watoa huduma wamezidi wateja, hivyo kipato ni finyu mno. Madereva wengi wa Uber au Taxify wanaficha ukweli ila kwa sasa ile biashara ni ngumu.

Ukitaka kuona kidogo maslahi, Jiunge kote, Uber na Taxify, ukiwa network moja, utaishia maumivu tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeipiga sio mda mrefu na nilikua na mzungu mmoja Kwenye gari ananiambia tatizo nini nikimwambia subir nikufikishe kwako utajua tatizo nin Leo ni ijumaa gar ilitakiwa iwe road inapiga kazi Ila wanauzia matunda kaz uber ngumu kweli kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hii biashara uber na taxify inamlipa sana kuliko mwenye gari.

wao kila siku wanaandikisha wenye magari wajae... mnajikuta watoa huduma wengi kuliko wateja...
 
Sijaisikia hiyo ikoje?
Hii kama hizo ila tofauti yake ni kuwa unaweka sehemu unayoenda na kuweka kadirio la bei (kwa uber bei inakuja yenyewe baada ya kuweke sehem uendayo).
Baada ya kuweka bei yako wewe abiria, madreva watajitokeza ambao nao wataweka bei zao (wengine zinaweza kufanana na yako au juu zaidi hata chini pia). Kama kuna dreva ana bei ya kuridhisha kwako abiria, unachagua ndio anakuja.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mkuu iko poa zaidi
 

Kaka tunaomba mrejesho. Mlifikia wapi malalamiko yenu? Je changamoto zimepungua walau kidogo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…