Maelezo zaidi ya historia ya khanga za Boimanda na Ummie Alley Hamid

Maelezo zaidi ya historia ya khanga za Boimanda na Ummie Alley Hamid

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Naweka hapa chini maelezo ya ziada kuhusu historia ya Khanga za Boimanda kama alivyoniandikia dada yangu Ummie Alley Hamid kutoka Zanzibar.

Katika maelezo yake kanikumbusha mambo ambayo nilikuwa nimeyasahau.
Vazi la khanga lilikuwa vazi muhimu na maarufu kwa mama zetu.

Nakumbuka ilikuwa ikitoka khanga mpya kuna gari linapita mitaani likitangaza
na hiyo khanga imewekwa kama tangazo na mtu akiieleza ile khanga ilivyo na
maneno ambayo yameandikwa kwenye khanga hiyo.

Pamoja na matangazo hayo kuna muziki unapigwa kupitia maspika katika gari
hiyo.

Katika maspika hayo katika miaka ile ya 1950 katikati utamsikia Salum Abdallah
muziki wa Egyptian au Al Watan ukipigwa kutoka gramaphone iliyokuwa ndani ya
gari.

Kuna khanga ambayo nakumbuka imepita mtaani kwetu Kipata na mtangazaji
akawa anayaeleza maneno yaliyoandikwa akisema, ''Mvua ya nyemi nyemi haimkatazi
mgeni kwenda kwake wala mwenyeji kula chake.'':

Msome aliyoniandikia dada yangu Bi. Ummie Alley Hamid hapo chini katika yale
yaliyopungua katika makala yangu:

"Kaka Mohamed Said leo umenifumbulia fumbo ambalo nilikuwa silijuwi la mtu anaeitwa Boimanda.

Nikiwa mdogo nisiozidi miaka 10, hapa Unguja zilitoka kanga jina BOIMANDA KODI KAINGIA BILA YA HODI.

Kanga wakati ule zikinadiwa kwa kupiga upatu, wanawake wakisikia upatu wanakimbilia milangoni kutizama mali gani mpya imetoka.

Kanga za Boimanda zilikuwa na rangi ya manjano, nyeusi na nyeupe.

Kama sikosei zilikuwa design ya msumeno.

Nazikumbuka kwa sababu Mar. Bibi yangu Bi Zuweina Bint Suleiman Almarjeby (Allah yrhamha), alizipenda sana na alizifungisha.

Kufungisha kanga ulikuwa unatowa “arbuni” au “rubuni” (advance) ya kiasi ulichonacho kama pesa 4 (senti kumi) au zaidi.

Mpiga upatu anakupa risiti na kisha unakwenda kulipa kidogo kidogo Mtendeni kwa “Miwani Mkubwa” au “Miwani Mdogo” hadi utimize shilingi 2 bei ya doti ya Kanga kisha unakwenda kuchukua mvao wako.

Wanawake wengi walishindwa kumaliza malipo na “vijisenti” vyao viliishia “arijojo” kuwanufaisha mabepari wafanya biashara.

Mar. Bibi nilimuuliza nani Boimanda? Akanambia ni Mwendawazimu wa Dar es salaam anaingia nyumba yoyote ile bila ya hodi pindipo akisikia neno “kodi”.

Kwa kweli sikuelewa vizuri na utoto wangu lakini hadi leo nakumbuka kanga za BOIMANDA KODI KAINGIA BILA YA HODI.

Ahsante sana Sh. Mohamed kwa historia hii ambayo imenigusa na kunikumbusha mambo ambayo sikuyaona ila nimeyasikia na leo nikiwa nishaingia uzeeni ndio napata utango na usuli wake.

Allah amrehemu Bibi yangu na Boimanda na wote uliowataja waliotangulia mbeke ya haki. Na wewe JAZAKA LLAHU L KHAIR."
 
Kuna kanga ziliingia miaka ile zina michoro ya miduara miduara mikubwa tulikua tukiziita BOIMANDA sikumbuki ni kwa nini. Na Yale maneno ya kwenye kanga yalikua hayaji holela. Tulikua tunasubiria matoleo ya maneno ya kanga kama kitabu cha SANI vile.
 
Leo Allama Mohamed Said na Bi Ummie mmenikumbusha mbali sana. Licha ya wazee wetu kuwa wapenzi wa Khanga na kuturithisha mila hiyo, mie na "divert" kiduchu.

Kwa kuongezea tu.

Mtaa wa Lumumba na Udoe. Kuna bibi yangu marehem Bi Masha, (ndugu na bibi yangu halisa) akipika sambusa aina mbili. Sambusa za mchele na sambusa za kawaida.

Upikaji wa sambusa ufundi wake na kazi yake kubwa ipo katika kutengeneza "manda". Manda ni ule mkate laini unaotengenezwa kiustadi kufungia vionjo vilivyo ndani ya sambusa, iwe nyama, mboga au viazi. Ukikosea tu kutengeneza manda basi huna sambusa.

Hizi manda zina utaalam wa kutengeneza kwake, si kila mtu awezae. Ni mpaka ufundishwe ufundike.Na ukitaka kuzitengeneza kwa wingi kiasi cha sambusa za biashara basi inabidi upate wasaidizi wa kutengeneza hizi manda. Hao ndiyo wakiitwa Boimanda.

Nakumbuka hilo kwa sababu tukitumwa na marehem Bi Masha kwenda Seyun Hotel au Saba Saba hotel (kwa Mangush), hizo "hoteli" zote zilikuwa mtaa wa Msimbazi, tumwambie Mangush kuwa Boimanda anaitwa akamsaidie bi Masha. Nnauhakika itakuwa si huyu wa kodi kwani mimi nnaongelea 60s na si 50s. Lakini hilo jina "Boimanda" limenikumbusha utotoni na wazee wangu.

Kwa kuongezea tu, kaukau zinatokana na mabaki ya manda iliokwisha katwa katwa kufanyia sambusa. Nani utotoni aliekulia Dar., katika 50s na 60s hajala kaukau? Aghalabu sana.

Allah awarehem wazee wetu waliotangulia aturehem na sisi na airehem jamii yetu nzima. Atuepushe na kiza na atuongoze na kututandazia Nuru isiyo na mwisho, nje na ndani ya umauti. Amin.
 
Faizafox na Mohamed Said utafikiri hawa viumbe ni mapacha.
Hongereni kwa kuleta hapa vitu vya kale japo siye tulikuwa bado kuzaliwa!
 
Faizafox na Mohamed Said utafikiri hawa viumbe ni mapacha.
Hongereni kwa kuleta hapa vitu vya kale japo siye tulikuwa bado kuzaliwa!
Allama Mohamed Said ni wa "kaliba" ya kudondoshea "vifaru" (armoured tanks) utawezaje kumfananisha na kaliba (mimi) isiyo na uwezo hata wa kudondosha tongwa?

Allah amzidishie Nuru kaka yangu Mohamed Said ametutoa wengi kizani na anazidi kutuongezea Nuru. Anatu "inspire" wengi sana na kila nionapo mada yake basi huwahi niione Dar yetu kwa macho yale ya utotoni. AlhamduliLlah.

Aandikapo Allama Mohamed Said, Dar., ile tuliyokulia hujaa machoni na hutukumbusha wengi tuliowajua fika. Moyo hufarijika sana.
 
Napenda sana Arts ya Uandishi vionjo na ladha ya vineno flani hivi basi huleta burudaaaan murua kabsaaa[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Hilo jina Boimanda sijalisikia siku nyingi sana.

Mission Quarters stand up!
 
Leo Allama Mohamed Said na Bi Ummie mmenikumbusha mbali sana. Licha ya wazee wetu kuwa wapenzi wa Khanga na kuturithisha mila hiyo, mie na "divert" kiduchu.

Kwa kuongezea tu.

Mtaa wa Lumumba na Udoe. Kuna bibi yangu marehem Bi Masha, (ndugu na bibi yangu halisa) akipika sambusa aina mbili. Sambusa za mchele na sambusa za kawaida.

Upikaji wa sambusa ufundi wake na kazi yake kubwa ipo katika kutengeneza "manda". Manda ni ule mkate laini unaotengenezwa kiustadi kufungia vionjo vilivyo ndani ya sambusa, iwe nyama, mboga au viazi. Ukikosea tu kutengeneza manda basi huna sambusa.

Hizi manda zina utaalam wa kutengeneza kwake, si kila mtu awezae. Ni mpaka ufundishwe ufundike.Na ukitaka kuzitengeneza kwa wingi kiasi cha sambusa za biashara basi inabidi upate wasaidizi wa kutengeneza hizi manda. Hao ndiyo wakiitwa Boimanda.

Nakumbuka hilo kwa sababu tukitumwa na marehem Bi Masha kwenda Seyun Hotel au Saba Saba hotel (kwa Mangush), hizo "hoteli" zote zilikuwa mtaa wa Msimbazi, tumwambie Mangush kuwa Boimanda anaitwa akamsaidie bi Masha. Nnauhakika itakuwa si huyu wa kodi kwani mimi nnaongelea 60s na si 50s. Lakini hilo jina "Boimanda" limenikumbusha utotoni na wazee wangu.

Kwa kuongezea tu, kaukau zinatokana na mabaki ya manda iliokwisha katwa katwa kufanyia sambusa. Nani utotoni aliekulia Dar., katika 50s na 60s hajala kaukau? Aghalabu sana.

Allah awarehem wazee wetu waliotangulia aturehem na sisi na airehem jamii yetu nzima. Atuepushe na kiza na atuongoze na kututandazia Nuru isiyo na mwisho, nje na ndani ya umauti. Amin.
Maalim Faiza,
Amin.

Nami umenirejesha mbali sana kabisa.

Pale Seyun Hotel pembeni kulikuwa na barza maarufu ya wazee wetu wa mjini.

Labour Commissioner Said Makutika alikuwa hapungui hapo kwa mazungumzo na wazee wenzake kila jioni.

Seyun Hotel ilikuwa ikisifika sana kwa maandazi yake mazuri kiasi jamaa wa mitaa ya jirani utawakuta asubuhi wamejazana pale kununua maandazi yale pale.
 
Allama Mohamed Said ni wa "kaliba" ya kudondoshea "vifaru" (armoured tanks) utawezaje kumfananisha na kaliba (mimi) isiyo na uwezo hata wa kudondosha tongwa?

Allah amzidishie Nuru kaka yangu Mohamed Said ametutoa wengi kizani na anazidi kutuongezea Nuru. Anatu "inspire" wengi sana na kila nionapo mada yake basi huwahi niione Dar yetu kwa macho yale ya utotoni. AlhamduliLlah.

Aandikapo Allama Mohamed Said, Dar., ile tuliyokulia hujaa machoni na hutukumbusha wengi tuliowajua fika. Moyo hufarijika sana.
Ndugu zanguni huyu dada yangu ni bingwa na huwezi kumjua hadi umsome ila yeye hupenda sana kujidogosha.
 
Maalim Faiza,
Amin.

Nami umenirejesha mbali sana kabisa.

Pale Seyun Hotel pembeni kulikuwa na barza maarufu ya wazee wetu wa mjini.

Labour Commissioner Said Makutika alikuwa hapungui hapo kwa mazungumzo na wazee wenzake kila jioni.

Seyun Hotel ilikuwa ikisifika sana kwa maandazi yake mazuri kiasi jamaa wa mitaa ya jirani utawakuta asubuhi wamejazana pale kununua maandazi yale pale.
Huwezi kuamini nilikutana na mpishi wa yale maandazi ya Seyun nilipobahatika kwenda Haj. Yupo hai anaitwa Abeid na yupo anaishi jijini Jeddah kwa sasa ni mpishi katika "kasr" (palace) moja la Maamir (watoto wa Kifalme) wa huko.
 
Huwezi kuamini nilikutana na mpishi wa yale maandazi ya Seyun nilipobahatika kwenda Haj. Yupo hai anaitwa Abeid na yupo anaishi jijini Jeddah kwa sasa ni mpishi katika "kasr" (palace) moja la Maamir (watoto wa Kifalme) wa huko.
Maalim Faiza,
Haj Trustee walikuwa na nyumba Jeddah mwaka 1997 tulikwenda Umrah na tukafikia kwenye hiyo nyumba.

Kiongozi wa msafara Abdallah Jabir akatuletea lunch akatuambia mpishi ni jamaa yetu kutoka Jumba la Mfalme.

Sijui kama ni Abeid wa Seyun.
 
Maalim Faiza,
Haj Trustee walikuwa na nyumba Jeddah mwaka 1997 tulikwenda Umrah na tukafikia kwenye hiyo nyumba.

Kiongozi wa msafara Abdallah Jabir akatuletea lunch akatuambia mpishi ni jamaa yetu kutoka Jumba la Mfalme.

Sijui kama ni Abeid wa Seyun.
Ni yeye huyo, hapana mwengine zaidi yake mwenye ukarimu huo. Ma shaa Allah.

Nilipata bahati ya kukaa Jeddah kwa muda baada ya Haj, kwa kaka yangu Bwana Hussein "Shaft" ndipo nilipokutana na Abeid na ilikuwa ni hivyo hivyo, kapata taarifa kuna wageni akasema msipike huko. Chakula kitatoka kwangu. Basi naam, ilikuwa ni ada, kila siku chakula anatuletea mwenyewe kutoka kasr na upishi wake uliotukuka.

Nadhani unamfaham Hussein Shaft ni ndugu yetu wa Kariakoo anaishi huko zaidi ya miaka 40 sasa.
 
SHEIKH NIJUZE KIDOGO nina hamu ya kufahamu je MOHAMMED SAID weye ndiye yule mtunzi wa vitabu kama vile"Kivuli Kinaishi" au ni ufanano wa majina tu
 
Back
Top Bottom