RAHA KAMILI
JF-Expert Member
- Dec 5, 2014
- 203
- 83
Askofu Malasusa ameyasema hayo tarehe 23.01.2017 alipokuwa akizungumza na Fahari news katika uzinduzi wa tawi jipya la benki ya (Maendeleo Bank) lililozinduliwa Kariakoo Jijini Dar es Salaam.
Meneja wa tawi hilo jipya Bi Nuru Shedrack alisema uzinduzi wa tawi hilo la Kariakoo linatoa fursa kwa wafanyabiashara kwa kusogezewa huduma ya kibenki karibu na sehemu zao za kazi ili kuepuka usumbufu na hatari ya kutembea na fedha jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha yao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank Bw. Ibrahim Mwangalaba alisema Bank ya Maendeleo itaendelea kuboresha utoaji wa huduma ikiwa ni pamoja na Kusogeza Karibu zaidi Huduma zake kwa wateja.