Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,252
- 36,513
Ukweli uwekwe wazi.
Kazi kubwa aliyoifanya Magufuli kuiongoza Serikali kufikia malengo yenye mafanikio ikiwemo la kufika Uchumi wa Kati kabla ya 2025 ni wazi amejitengenezea maadui wengi waa ndani na nje ya nchi. Hebu ongozana nami kwa ufupi kwenye maeneo muhimu
1. UGENISHAJI KATIKA RASILIMALI
Magufuli alikataa rasilimali za nchi kumilikiwa kwa sehemu kubwa na makampuni ya kigeni ambapo Serikali yake imepeleka sheria bungeni na kuibadili ili nchi iweze kunufaika na rasilimali zake.
Ukiangalia uamuzi wa kujenga ukuta kuzunguka eneo la machimbo ya Tanzanite Mererani imepelekea Tanzania kuingia kwenye orodha ya vinara wa biashara ya Tanzanite duniani ambapo awali India, Kenya na SA walikuwa wameshika soko.
Kuanzisha masoko ya madini ya ndani imesaidia kupunguza utoroshwaji wa madini yetu na kuingizwa kwenye black market.
2. MIUNDOMBINU
Rais Magufuli amesimamia nankutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa barabara na madaraja nchini, sambamba na kufungua reli kuelekea Tanga, Moshi na Arusha huku akiimarisha reli kongwe ya Kigoma kuwa ktk SGR hivyo kufanikisha upanuaji wa huduma za Bandari ya Dar es Salaam kwa nchi zilizo land locked. Miradi hii mikubwa ilibuniwa na hata awamu zilizopita lakini haikutekelezwa kutokana na kukosekana rasilimali fedha.
Ingewezekana kukopa kutoka kwa nchi wahisani lakini JPM alizingatia mzigo mkubwa wa madeni na kuamua kujiondoa kwenye unyonge wa masharti magumu hatimaye miradi hii imetekelezwa kwa fedha zitokanazo na makusanyo ya kodi.
Ujenzi na upauaji wa viwanja vya ndege mikoa mingi umeenda sambamba na kununua ndege mpya 11 ambapo pamoja na kufufua ATCL lakini unaipa nafasi sekta ya utalii kutumia fursa hii kuleta watalii wengi nchini.
Bandari zimeongezewa ubora hata ununuzi/ujenzi wa meli mpya za abiria na mizigo ni mambo yaliyofanyika ndani ya miaka 5 yake ya kwanza. Ujenzi wa ICDs Dodoma na mikoa ya jirani ni wazi connection ya SGR na Bandari utafanikisha ukuaji mkubwa wa uchumi na kuyasukuma maendeleo ya Taifa mbele zaidi
3. VITAMBULISHO VYA WAJASIRIAMALI
Hii ni haueni kubwa kwa wafanyamiashara almaarufu wamachinga kwani walionekana hawana mchango wowote kwenye jamii na walionekana ni wasumbufu. Vitambulisho hivi vimesaidia micro-business kuchangiia pato la Taifa na hata kuwajengea mazingira ya kutosumbuliwa na wamepunguza ugumu au mfumuko wa bei mitaani.
Wajasiriamali wadogo wamekiwa wakitozwa ushuru Tshs 500 kutwa ambazo haziingii serikalini na ukiangalia wanatoa zaidi ya Tsha20,00 kwa mwaka kwa ushuru huo. Hivyo tozo ya Tshs 20,000 kwa mwaka ni faraja kwa wamachinga na wenye mitaji midogo.
4. UFISADI
5. ULINZI NA USALAMA
6. KUINUA KILIMO
7. UBORESHAJI SEKTA YA AFYA
8. KUPAMBANA NA RUSHWA
9. MISHAHARA HEWA
10. MAHAKAMA YA MAFISADI
11. VYETI FEKI
12. KULIPA MALIMBIKIZO YA WAALIMU
13. KUPAMBANA NA CORONA.
14....
Nimeorodhesha na kudadavua maeneo kadhaa ya maendeleo yaliyofikiwa na serikali ya awamu ya tano, ni wazi Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hawafurahii haya maendeleo.
Katika kampeni za mgombea wao wa urais amekuwa akitumia jukwaa la siasa kutukana na kubeza maendeleo hadi kufikia kusema kwamba ununuzi wa ndege ni matumizi mabaya ya fedha za umma. Kuna wakati anawaambia wananchi kwamba kama Magufuli kajenga mabarabara na madaraja basi hayo yampigie kura.
Zaidi sana Chadema wamejipambanua kupitia kampeni za mwaka huu kwamba ni maadui wa maendeleo ya nchi.
Mgombea wao ameshasema kwamba, ataweka dhamana madini na rasiilimali za nchi ilikujenga miundombinu na kadhalika. Pia wamejinasibu kutaka kubadili katiba kama takwa la kwanza lakini wanajisahau kwamba sisi wananchi tunajua namna walivyobadili katiba ya CHADEMA ili kumpa uenyekiti wa maisha Mbowe. Sisi tuna akili na tunatambua hila zao wanazotuhadaa kwenye kampeni zao.
CHADEMA wanamtukana sana Magufulina kumbeza kwa sababu amesimama imara kuiletea nchi maendeleo na kukataa ghiliba za mabeberu ambao wanataka kuifanya Tanzania kuwa nchi yao ya kinyonyaji.
JPM
Kazi kubwa aliyoifanya Magufuli kuiongoza Serikali kufikia malengo yenye mafanikio ikiwemo la kufika Uchumi wa Kati kabla ya 2025 ni wazi amejitengenezea maadui wengi waa ndani na nje ya nchi. Hebu ongozana nami kwa ufupi kwenye maeneo muhimu
1. UGENISHAJI KATIKA RASILIMALI
Magufuli alikataa rasilimali za nchi kumilikiwa kwa sehemu kubwa na makampuni ya kigeni ambapo Serikali yake imepeleka sheria bungeni na kuibadili ili nchi iweze kunufaika na rasilimali zake.
Ukiangalia uamuzi wa kujenga ukuta kuzunguka eneo la machimbo ya Tanzanite Mererani imepelekea Tanzania kuingia kwenye orodha ya vinara wa biashara ya Tanzanite duniani ambapo awali India, Kenya na SA walikuwa wameshika soko.
Kuanzisha masoko ya madini ya ndani imesaidia kupunguza utoroshwaji wa madini yetu na kuingizwa kwenye black market.
2. MIUNDOMBINU
Rais Magufuli amesimamia nankutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa barabara na madaraja nchini, sambamba na kufungua reli kuelekea Tanga, Moshi na Arusha huku akiimarisha reli kongwe ya Kigoma kuwa ktk SGR hivyo kufanikisha upanuaji wa huduma za Bandari ya Dar es Salaam kwa nchi zilizo land locked. Miradi hii mikubwa ilibuniwa na hata awamu zilizopita lakini haikutekelezwa kutokana na kukosekana rasilimali fedha.
Ingewezekana kukopa kutoka kwa nchi wahisani lakini JPM alizingatia mzigo mkubwa wa madeni na kuamua kujiondoa kwenye unyonge wa masharti magumu hatimaye miradi hii imetekelezwa kwa fedha zitokanazo na makusanyo ya kodi.
Ujenzi na upauaji wa viwanja vya ndege mikoa mingi umeenda sambamba na kununua ndege mpya 11 ambapo pamoja na kufufua ATCL lakini unaipa nafasi sekta ya utalii kutumia fursa hii kuleta watalii wengi nchini.
Bandari zimeongezewa ubora hata ununuzi/ujenzi wa meli mpya za abiria na mizigo ni mambo yaliyofanyika ndani ya miaka 5 yake ya kwanza. Ujenzi wa ICDs Dodoma na mikoa ya jirani ni wazi connection ya SGR na Bandari utafanikisha ukuaji mkubwa wa uchumi na kuyasukuma maendeleo ya Taifa mbele zaidi
3. VITAMBULISHO VYA WAJASIRIAMALI
Hii ni haueni kubwa kwa wafanyamiashara almaarufu wamachinga kwani walionekana hawana mchango wowote kwenye jamii na walionekana ni wasumbufu. Vitambulisho hivi vimesaidia micro-business kuchangiia pato la Taifa na hata kuwajengea mazingira ya kutosumbuliwa na wamepunguza ugumu au mfumuko wa bei mitaani.
Wajasiriamali wadogo wamekiwa wakitozwa ushuru Tshs 500 kutwa ambazo haziingii serikalini na ukiangalia wanatoa zaidi ya Tsha20,00 kwa mwaka kwa ushuru huo. Hivyo tozo ya Tshs 20,000 kwa mwaka ni faraja kwa wamachinga na wenye mitaji midogo.
4. UFISADI
5. ULINZI NA USALAMA
6. KUINUA KILIMO
7. UBORESHAJI SEKTA YA AFYA
8. KUPAMBANA NA RUSHWA
9. MISHAHARA HEWA
10. MAHAKAMA YA MAFISADI
11. VYETI FEKI
12. KULIPA MALIMBIKIZO YA WAALIMU
13. KUPAMBANA NA CORONA.
14....
Nimeorodhesha na kudadavua maeneo kadhaa ya maendeleo yaliyofikiwa na serikali ya awamu ya tano, ni wazi Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hawafurahii haya maendeleo.
Katika kampeni za mgombea wao wa urais amekuwa akitumia jukwaa la siasa kutukana na kubeza maendeleo hadi kufikia kusema kwamba ununuzi wa ndege ni matumizi mabaya ya fedha za umma. Kuna wakati anawaambia wananchi kwamba kama Magufuli kajenga mabarabara na madaraja basi hayo yampigie kura.
Zaidi sana Chadema wamejipambanua kupitia kampeni za mwaka huu kwamba ni maadui wa maendeleo ya nchi.
Mgombea wao ameshasema kwamba, ataweka dhamana madini na rasiilimali za nchi ilikujenga miundombinu na kadhalika. Pia wamejinasibu kutaka kubadili katiba kama takwa la kwanza lakini wanajisahau kwamba sisi wananchi tunajua namna walivyobadili katiba ya CHADEMA ili kumpa uenyekiti wa maisha Mbowe. Sisi tuna akili na tunatambua hila zao wanazotuhadaa kwenye kampeni zao.
CHADEMA wanamtukana sana Magufulina kumbeza kwa sababu amesimama imara kuiletea nchi maendeleo na kukataa ghiliba za mabeberu ambao wanataka kuifanya Tanzania kuwa nchi yao ya kinyonyaji.