Mafanikio ambayo Yanga wameyafikia pasipo kutarajia ndio yanayowaumiza

Mafanikio ambayo Yanga wameyafikia pasipo kutarajia ndio yanayowaumiza

choza choza

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2019
Posts
2,081
Reaction score
3,831
Hii ipo Dunia nzima pale ambapo timu imefikia matarajio ambayo hawakuyategemea ghafla.

Monaco ya 2016, iliyokua na Mbappe, Bernado Silva, Fabinho, Falcao, Bakayoko, Benjamin Mendy, Moutinho nk, ilivurugika tu punde baada ya kuchukua League 1 na kufika Nusu Fainali CL, hawakutarajia mafanikio hayo hivyo ikawa ngumu kuwabakiza mastaa wake hasa vilabu vikubwa vilipokuja kupiga hodi.

Bangala, Mayele, nk, uwezo wao umeonekana na vilabu vikubwa vyenye hela kuliko Yanga, lazima vibishe hodi kutaka huduma zao.

Kocha Nabi anajua ingekua ni ngumu sana kuifikisha tena Yanga kwenye peak iliyopo na anajua kuna nyota kadhaa wataondoka hivyo kaamua kulinda heshima yake (ambapo Mzee Claudio Ranieri alichelewa kufanya hivyo Leicester).
 
ujinga
ujinga
Ujinga
Ujinga
Mpira siku hizi asilima 90 unachezwa Nje.
Sio kama enzi za Fergie na Mzee wenger.
Ndio maana siku hizi unaona Team inaamua kuajiri Director Flan kumtoq Team Flan tena kwa Dau kubwa Kwa sababu tu anajua kitu flan Mifano ipo wapi na inaonekana.
Angalia
1.Aseno saiv wana Edu
2.PSG director wao wamemng'oa Italy huko
3.Tottenham iliwagharimu wafate mtaalam Italy
4.Barca waliyumba sio kisa messi kusepa La hasha uongozi ulikuja kuyumba
5.Man U sio kwamba haisajili ila uongozi ni mbovu
6.Newcastle haina kocha mkali kivile ila Uongozi na Pesa
7.Chesii sio kwamba hawasajili ila uongozi walio nao bila yule mdada na Abramovic wanateseka.
8.Liverpool juzi wametoa Mkurugenzi Ujeruman tena kwa hela kubwa
BADO UNATAKA MIFANO?
Look
Brighton ilitoa kocha ikatoa Trossard ila imekuaje still ni good team coz ina uongozi unaosimamaia Maono

Madrid wanafanya yale yote sio kisa Kocha wala wachezaji ila issue ni uongozi wa PEREZ

FOOTBALL INAHITAJI UONGOZI SIKU HIZI WATU WAKUSIMAMIA MAONO
 
Pep nae ataondoka city pamoja na mfungaji wake Haaland??
Kesi ya Pep pale City ni tofauti, City sio underdog wa vilabu vingine pale ulaya, anauhakika wa kuendelea kunasa mastaa kibao hata kina KDB wakiondoka sababu pesa ndefu ipo

Kumbuka leicester ghafla ilivyowapoteza mastaa wengi baada ya ubingwa, sababu wao ni underdog kama ilivyo Yanga kwa sasa
 
Kingine ni aina ya usajili uliopo Tz, unasajili kundi la wachezaji 10 kwa mpigo, unawapa mkataba wa miaka 2, kwahiyo inafika muda unawachezaji 10 wote mikataba imeisha na unakuta wamefanya vizuri , inakua ngumu kuwabakiza
 
Back
Top Bottom