Wanajamii jamani mimi nampenda sana Rais wangu sijui nyie...
Ni mpenda maendeleo
Ni jasiri si muoga
Anajitoa kwaajili ya Watanzania.
Mchukia Rushwa
Mchukia Ufisadi
hakika akikaa miaka kama 10 naamini Tanzania tutakuwa mbali.
Kila binadamu anamadhaifu yake ila Rais wetu mazuri yamezidi madhaifu.
Yeye kuwa Rais amewezesha Taasisi za Serikali kusimama kwani hapo nyuma zilikuwa zinakandamizwa na wasiokuwa wazalendo hadi kupelekea nyingine kuuzwa.
Anapenda mali za Tanzania wafaidi Watanzania na si Wageni.
Amejitoa hasa, na hasa wanaofaidi haya ni Masikini ila Matajiri wale waliojipatia utajiri kwa kudhulumu watanzania wengi hawafurahii hili kabisa...wanatamani atoke saa ngapi ili warudi kula tena..
1.- Rais ameleta adabu Serikalini na katika taasisi zake...Sasa hivi ukienda Muhimbili unaheshimika, Unapokewa vizuri na kuhudumiwa hakuna nyodo.
2. - Ameweza tukawatambua waliokuwa wanawadhulumu vijana waliosoma kweli kweli wenye vyeti vyao vya kweli...kwa kuwagundua waliokuwa wanatumia vyeti feki.
3. - ameweza fanya tukawagundua waliokuwa wakijilipa mishahara kwa majina feki
4. - Ameweza pambana na anaendelea kupambana na wizi unaoendelea Bandarini
5. - Ameweza kuwatumbua wasiokuwa watendaji wazuri katika Taasisi za Serikali mfano: TRA, TANESCO, etc.
6. - Ameweza kuwafanya mawaziri aliowateuwa wamuwakilishe katika kazi kuheshimu kazi zao kwani hapo awali walikuwa wafanye kazi wasifanye mshahara unaingia poa tuu...ila sasa unamsikia waziri kabisa akilalamika Jamani mimi ninawatoto msiniharibie kazi...Waziri leo hii anatamani kulia kwa watu ili wasimuharibie kazi...ila hapo awali ilikuwa kawaida tuu kutofanya kazi na kulala bungeni.
7. - Ameweza kudhibiti fedha za umma na kwenda BOT kwani watu walikuwa washazigeuza kuwa za biashara zao.
8. - Ameweza kusababisha MAFISADI PAPA wakakamatwa kama Manji, Rugemarila, na wenzake wakati ingekuwa hapo awali wangeweza kutoroka tena kwa kusindikizwa hadi AIRPORT tena kwa escort tukaambiwa wametoroka..kama ilivyo Alex Massawe alivyofanya na wenzake.
9. - Ameweza kusimamisha Kampuni ya Ndege na kununua ndege ambayo ilikuwa inafilisika..sasa imerudia uhai tena.
10. Miundo mbinu inajengwa mbali mbali ie. Barabara, Airports, Maji kama juzi katoka kuzindua mradi Mwanza n.k.
11. Maji sasa maeneo ya KIMRA na MBEZI ambapo ilikuwa historia maji kutoka japo bomba limepita huko sasa yanatoka.
Ni mengi sana kumaliza ni issue wengine waongezee..
Hakika rais wetu anastahili sifa, na anachukiwa na wengi wabinafsi wanaopenda wao na familia zao tuu zifaidike kwa mali za Tanzania.
Wapinzani wangekuwa na akili wasingekuwa wanapiga kelele kuhusu Rais anachokifanya sasa bali wachape kazi wamuige Rais anachokifanya ili wajiongezee CREDIT.
Tatizo la wapinzani wetu hata jambo la kitaalamu wao wanaingiza siasa ndani yake. Utakuta mwanasiasa si mtaalamu wa Afya atataka aingilie suala la afya, Si mtaalamu wa mambo ya Usalama atataka aingilie...Waachieni wenye Professionals zao wafanye kazi zao.
Wapinzani wenzangu tufanye kazi, Mmepewa jimbo la Ubungo basi tuone matunda yenu.. Fanyeni kazi. Si hadi Mkuu wa Mkoa au Rais aongee kuhusu maji ndipo maji tuletewe...Hakika kama si Uongozi huu wa sasa Kimara na Mbezi kungeendelea kuwa na historia ya kutopata maji ila sasa kwa wale walioomba maji yanatoka..Mnyika ulikuwa Mbunge muda mrefu mbona hukuleta Maji??
Barabara za majimbo ya Ubungo jengeni hasa zile barabara kuu...mfano: Mbezi hadi Mpiji magohe hadi bunju, Mbezi hadi Kinyerezi, mbezi kwa Msuguli hadi Kinyerezi..etc. acheni kuongea tuu...Wabunge tendeeni kazi ubunge wenu mlopewa, wapelekeeni watu maendeleo. Mwenzako akifanya hiki wewe fanya lile..hizi si zama za porojo tena..
MWISHO NAMALIZIA KWA..
Chunguza utabaini: Kila taifa lililokuwa maskini, wananchi wake hawaendi bila kuwaamrisha kisha likaja mpata rais ambaye alikuwa mkali katika taifa lake taifa hilo liliweza pata maendeleo..mfano: Fuatilia sera za
Mao Tse-tung na CHINA YAKE ila aliinyoosha china ikasimama,
Hitla na German,
Gadaafi na Libya hadi kuoa vijana ilifikia wakawa wanalipiwa mahari - hahahaha ona sasa aliyewachonganisha kikowapi leo hii zile mahari hawazipati tena....etc..
Katika uongozi kuna uongozi mwingine lazima kidogo uapply udikteta ili nchi iendelee la sivyo baadhi ya watu watakurudisha nyuma....Na Rais wetu ningependa aaply hiyo kwa hii miaka kumi ili watu wanyooke...
Viongozi wa awali walipelekea hadi kila mmoja kutamani kuwa kiongozi ili aende akapate ulaji...Kwani alijua akiwa tu kiongozi ni ulaji.
Vijana wetu walikuwa wanasoma ili wakapate hela bali si kwa kuipenda kazi...Utasikia mtu anataka kuwa Mhasibu sababu ya alijua akiwa Mhasibu atapata hela za kupiga, Kijana alitaka kusomea Procurement akijua akiwa katika idara ile atapata hela za kupiga.
Hii taswira sasa kwa vijana ibadilike bali vijana wasome kwa uzalendo...
Uongozi ulikuwa unatafutwa hadi kutoa rushwa, sababu walijua mtu ukiwa Waziri, Mbunge utapata hela za kula pasipo kutoka jasho, ila sasa baadhi ya watu wanaukana uongozi / wanaachia ngazi sababu ya kuhofia wao sio watendaji wazuri...
Tanzania inaenda ikiwa ile tunayoitaka...
Nikisema kuandika nii mengiiii hata simalizi leo..naishia hapa..
Namuombea Rais wetu Maisha Mema, Mungu amuongozi katika kazi zake...