Mafanikio ya Tanzania dhidi ya "Corona" yasihusishwe na uwezo wa Mungu

Mafanikio ya Tanzania dhidi ya "Corona" yasihusishwe na uwezo wa Mungu

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617
Nimekua nikisoma sehemu nyingi ambapo watu wengi sana, ndani na nje ya Tanzania wakisema kwa sauti na kwa wingi sana kwamba, kupungua kwa maambukizi ya Corona Tanzania imetokana na kumuamini Mungu, hivyo Mungu amejibu.

Hii inatokana na msimamo wa Magufuli wa kutofunga nyumba za ibada na kuwaomba wananchi wamuombe Mungu mara kwa Mara kuwalinda dhidi ya Corona, hata kutoa siku maalumu ili kuwepo kwa siku za kitaifa za kufanya maombi.

Bwana Yesu aliwahi kusikika akisema kwamba" Imani yako itakuponya", je hii inamaana kwamba watanzania ndio wenye imani lakini mataifa mengine hayana hiyo imani ndio sababu bado maambukizi yanaongezeka kwa kasi? Je, Magufuli ndiye rais pekee mwenye imani hapa duniani?

Tumeshuhudia viongozi mbalimbali duniani wakiwemo viongozi wa makanisa wengi ambao walikataa kufunga makanisa wakipoteza maisha kutokana na Corona, je hao wote hawana Mungu?

Tanzania kuna jambo au njia tofauti tuliyotumia ambayo haikuzingatiwa sana na nchi zingine, ndio chimbuko na sababu kubwa ya kupungua kwa maambukizi.
 
Kuanimi mungu sio sawa na kutofunga sehemu za ibada. Lile ni njengo tu.
Sasa kipi cha ajabu alichokifanya Magufuli/watanzania katika kumuamini Mungu hadi akawasikiliza na kuwakinga dhidi ya Corona kama kweli Mungu ndiye aliyesaidia kupunguza maambukizi Tanzania?
 
Sasa kipi cha ajabu alichokifanya Magufuli/watanzania katika kumuamini Mungu hadi akawasikiliza na kuwakinga dhidi ya Corona kama kweli Mungu ndiye aliyesaidia kupunguza maambukizi Tanzania?
Mungu hadhihakiwi bro

sifa zake na utukufu wake haulinganishwi na chochote

Mungu katumia mawe kumtajirisha laizer

Bro Tubu kwa Mungu
 
Mungu hadhihakiwi bro

sifa zake na utukufu wake haulinganishwi na chochote

Mungu katumia mawe kumtajirisha laizer

Bro Tubu kwa Mungu
Hakuna mtu aliyemdhihaki Mungu, ninachouliza ni kipi cha ziada ambacho Tanzania tulimfanyia Mungu hadi atusikilize lakini nchi zingine hawajakifanya ndio sababu hakuwasikiliza?, huko ndio kumdhihaki Mungu?
 
Nimekua nikisoma sehemu nyingi ambapo watu wengi sana, ndani na nje ya Tanzania wakisema kwa sauti na kwa wingi sana kwamba, kupungua kwa maambukizi ya Corona Tanzania imetokana na kumuamini Mungu, hivyo Mungu amejibu.

Hii inatokana na msimamo wa Magufuli wa kutofunga nyumba za ibada na kuwaomba wananchi wamuombe Mungu mara kwa Mara kuwalinda dhidi ya Corona, hata kutoa siku maalumu ili kuwepo kwa siku za kitaifa za kufanya maombi.

Bwana Yesu aliwahi kusikika akisema kwamba" Imani yako itakuponya", je hii inamaana kwamba watanzania ndio wenye imani lakini mataifa mengine hayana hiyo imani ndio sababu bado maambukizi yanaongezeka kwa kasi? Je, Magufuli ndiye rais pekee mwenye imani hapa duniani?

Tumeshuhudia viongozi mbalimbali duniani wakiwemo viongozi wa makanisa wengi ambao walikataa kufunga makanisa wakipoteza maisha kutokana na Corona, je hao wote hawana Mungu?

Tanzania kuna jambo au njia tofauti tuliyotumia ambayo haikuzingatiwa sana na nchi zingine, ndio chimbuko na sababu kubwa ya kupungua kwa maambukizi.

Kwanza Mungu hayupo na wala hajawahi kuwepo
 
Hakuna mtu aliyemdhihaki Mungu, ninachouliza ni kipi cha ziada ambacho Tanzania tulimfanyia Mungu hadi atusikilize lakini nchi zingine hawajakifanya ndio sababu hakuwasikiliza?, huko ndio kumdhihaki Mungu?
kutuponya tu ni ukuu wa Mungu umejionesha

hizo mbinu unazidai wewe ni Mungu pia ndie aliyetupa ufahamu huo
 
Mleta mada we ni mtu wa ajabu sana. Unamdharau Mungu anapokuwa kazini eee

Toba inakuhusu!
 
Ukiomba Mungu siyo lazima akuondolee tatizo linaokukabili. Nyakati nyingine anaweza akakuachia tatizo lako, lakini akakupa ujasiri na mtazamo mzuri wa kupambana na hali ngumu au jaribu. Kwa upande wa nchi ya Tanzania, tatizo halijaondoka, lkn wananchi wakiongozwa na viongozi wao wamekuwa na mtazamo mzuri na ujasiri. Matokeo yake kinga zao ziko juu. Halafu ugonjwa unaonekana kama umeisha.
 
kutuponya tu ni ukuu wa Mungu umejionesha

hizo mbinu unazidai wewe ni Mungu pia ndie aliyetupa ufahamu huo
Hii ni kwa wale wenye kuamini Mungu sio?, je sisi tunaoamini imani zetu za kijadi mnatuweka wapi, au hatuna nafasi wala haki ya kusikilizwa?. Sisi hatuamini huyo Mungu wenu.
 
Ukiomba Mungu siyo lazima akuondolee tatizo linaokukabili. Nyakati nyingine anaweza akakuachia tatizo lako, lakini akakupa ujasiri na mtazamo mzuri wa kupambana na hali ngumu au jaribu. Kwa upande wa nchi ya Tanzania, tatizo halijaondoka, lkn wananchi wakiongozwa na viongozi wao wamekuwa na mtazamo mzuri na ujasiri. Matokeo yake kinga zao ziko juu. Halafu ugonjwa unaonekana kama umeisha.
Kwa hiyo wale wanaojaribu kutuambia Mungu ndiye aliyesaidia kupunguza maambukizi Tanzania, wanatoa wapi huo ujasiri?
 
Hakuna mtu aliyemdhihaki Mungu, ninachouliza ni kipi cha ziada ambacho Tanzania tulimfanyia Mungu hadi atusikilize lakini nchi zingine hawajakifanya ndio sababu hakuwasikiliza?, huko ndio kumdhihaki Mungu?
Ww bado mjinga wa imani..ungesubir ukue kwanzs ndio uje huku. Watu tuko bize kumshukuru Mungu usituchoshe kama huna mada nyingine nyamaza
 
Una uhakika Laizer hakutambikia mizimu yake ya kimasai au hakwenda kwa waganga?
Mungu hadhihakiwi bro

sifa zake na utukufu wake haulinganishwi na chochote

Mungu katumia mawe kumtajirisha laizer

Bro Tubu kwa Mungu
 
Ww bado mjinga wa imani..ungesubir ukue kwanzs ndio uje huku. Watu tuko bize kumshukuru Mungu usituchoshe kama huna mada nyingine nyamaza
Wewe ndiye bwege usiyetumia akili, badala ya kutoa majibu ya kisayansi, wewe unakimbilia imani za kufikirika
 
Kwa hiyo wale wanaojaribu kutuambia Mungu ndiye aliyesaidia kupunguza maambukizi Tanzania, wanatoa wapi huo ujasiri?

Aha haa haaaa
😀😀😀
Wanapata ujasiri na mtazamo mzuri kutoka kwa Mungu, lkn labda wamelewa huo ujasiri na kuanza kuona mambo katika njia tofauti.
 
Back
Top Bottom