Mafisadi waiingilia idara ya usalama ya Botswana , wataka kumuua Rais Mokgweetsi Masisi ili kupora rasilimali za nchi hiyo

Mafisadi waiingilia idara ya usalama ya Botswana , wataka kumuua Rais Mokgweetsi Masisi ili kupora rasilimali za nchi hiyo

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
4bec4aee2ea140afa6d21aff494764ab_18.jpg

Raisi Masisi akila kiapo wakati akiapishwa kuwa raisi wa Botswana mwaka 2018. Picha na AFP

Maisha ya raisi wa Botswana Mokgweetsi Masisi yako hatarini baada ya mafisadi wakishirikiana na baadhi ya raia wa kigeni wenye uwezo wa kifedha kutoka nje ya Botswana kupanga kumuua kiongozi huyo.

Mpango huo wa kumuua kiongozi huyo unadaiwa kuratibiwa na aliewahi kuwa mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama ya DISS bwana Isaac Kgosi ambae aliondolewa kwenye nafasi yake hiyo mara baada ya raisi Masisi kuingia madarakani.

Mara baada ya kuingia madarakani mwezi April mwaka 2018, raisi Masisi alianzisha kampeni ya kuwashughulikia wale wote ambao wamekuwa wakijishughulisha na ufisadi na kujitochotea maliasili ya nchi hiyo hususan madini ya almasi.

Mwezi Julai mwaka jana mahakama kuu ya nchi hiyo iliamuru kutaifishwa kwa mali zote za bwana Kgosi na pia kuamuru uchunguzi kufanywa juu ya kujishughulisha kwake na masuala ya kifisadi na uendekezaji vitendo vya rushwa.

Kwa mujibu wa mkuu mpya wa idara ya usalama DISS brigedia Peter Magosi, ulinzi wa raisi Masisi umeangaliwa na kubadilishwa kulingana na ngazi ya tishio hilo la kuuawa na tayari idara ya DISS inaajiri wanajeshi na makomandoo wa zamani kutoka jeshi la Botswana ili kuongeza ulinzi kwa kiongozi huyo.

Tishio hilo linadaiwa kuhusisha watu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Bitswana ambao maslahi yao kwa namna moja ama ingine yamegushwa na hatua kadhaa za serikali ya raisi Masisi kuweka sheria mbalimbali dhidi ya udhibiti wa maliasili za nchi hiyo.

Endapo raisi Masisi ataondolewa kiongozi ajae atakuwa na woga juu ya kuchukua hatua zozote zenye kuwabana mafisadi ambao wapo kwenye mkao wa kugawana rasilimali za nchi hiyo.

Brigedia Magosi anadai pia kuwa ndani ya idara ya DISS wamegundulika baadhi ya maofisa ambao ni ndumila kuwili au double Agents ambao wanafanya kazi mbili kati ya serikali ya Botswana na na umoja wa mafisadi.

Brigedia Magosi ambae amewahi kuwa mkuu wa kitengo cha ujasusi ndani ya jeshi la Botswana BDF amedasi kuwagundua baadhi ya maofisa ambao wengi wameonekana kutokubaliana na aina ya uongozi wake na aina ya mawazo yake mapya ndani ya idara ya DISS.

xMagosi2.jpg.pagespeed.ic.QknwtMKbLk.jpg

Mkurugenzi wa sasa wa sasa wa DISS Brigedia Magosi (kushoto) na mkurugenzi wa zamani bwana Isaac Kgosi(kulia)

Kutokana na hali hiyo Brigedia Magosi amesema idara ya DISS kwa sasa inaajiri maofisa wastaafu wa idara ya ujasusi wa jeshi yaani military intelligence au MI na wengine kutoka jeshi la nchi hiyo BDF.

Mpaka sasa raisi Masisi na familia yake wanaishi kwenye ikulu namba mbili ambayo hukaliwa na makamu wa raisi na makamu wake huyo sasa anaishi kwenye nytumba yenye hadhi ya uwaziri.

Rekodi nzuri ya uchumi wa Botswana inajengwa na misingi mizuri ya usimamizi wa uchumbaji madini ya Almasi.

Ni nchi inayoaminika kuwa na kiwango kidogo sana cha vitendo vya rushwa na ufisadi, hivyo kuifanya kuwa nchi oekee inayoweza kugundua kwa uharaka mara raia wake wanapojishirikisha na vitendo hivyo kwa kushirikiana na wageni.


Richard na vyombo vya habari vya Botswana nikiwa Gaborone.
 
Hii habari ya 2018 inatusaidia nini kwa sasa? What is your point?
 
Kongo hapo kabila alikula risasi kisa almasi mkuu.

Walioshiriki mauaji wako huko uswizi wanakula bata kama wakimbizi.

Hawa watu usipoleta ushirikiano kwenye wizi wa rasilimali hawana mswalia mtume.
 
Hii habari ya 2018 inatusaidia nini kwa sasa? What is your point?
Swali la hovyo kabisa!

Kwa asilimia kubwa Dunia inaendeshwa kwa matukio yanayofanana.
Ndio maana kesi nyingi huamuliwa kwa kuangalia historia ya kesi zilizopita zinazofanana na hizo na hukumu zake.

Hata kama ingekuwa ni issue ya miaka 20 nyuma bado kuna jambo la kujifunza la hali tuliyo nayo kwa sasa.
 
Kongo hapo kabila alikula risasi kisa almasi mkuu.

Walioshiriki mauaji wako huko uswizi wanakula bata kama wakimbizi.

Hawa watu usipoleta ushirikiano kwenye wizi wa rasilimali hawana mswalia mtume.

Hata Che Guevara alimwona Kabila senior kama mtu ambae hakuwa na nia ya dhati.

Sasa kama Che Guevara aliona hilo vipi wale wanaharakati wengine?
 
Hata Che Guevara alimwona Kabila senior kama mtu ambae hakuwa na nia ya dhati.

Sasa kama Che Guevara aliona hilo vipi wale wanaharakati wengine?
Kosa la kabila senior ilikuwa ni kuondoa ile monopoly iliyokuwepo, na kuruhusu hata watu toka asia kujitwalia almasi. Hapo nipo alipopoteza Urais na maisha yake. Mabeberu wanahitaji kuiba tu.
 
Inawezekana hata sisi huku tulikuwa na tishio kama hilo baada ya Rais kuwatisha mabeberu. Naona ulinzi wa Rais wetu umeimarishwa tofauti na mwanzo. Hongera kwa vyombo vinavyohusika
 
Kongo hapo kabila alikula risasi kisa almasi mkuu.

Walioshiriki mauaji wako huko uswizi wanakula bata kama wakimbizi.

Hawa watu usipoleta ushirikiano kwenye wizi wa rasilimali hawana mswalia mtume.

Kabila hakuwa na nia ya dhati ndo maana alikosa support kubwa, any way uwoga wako ndo umasikini wako. Nchi nyengine zimeweza kupambana kwani nyie msiweze tazama Asia, Baadhi ya nchi za North Afrika
 
Kosa la kabila senior ilikuwa ni kuondoa ile monopoly iliyokuwepo, na kuruhusu hata watu toka asia kujitwalia almasi. Hapo nipo alipopoteza Urais na maisha yake. Mabeberu wanahitaji kuiba tu.

Suala la Congo DRC ni very complex.

Na sasa hivi nchi kama Uingereza zimetangaza kuondokana na magari yanayotumia diseli na petrili ifikapo 2035 kutoka uamuzi wa nyuma wa 2040.

Wanataka watengenezaji wote wa magari waanze mchakato wa kuunda magari yanayotumia batteries.

Malighafi ya kutengeneza batteries za magari inatoka Congo DRC.

Congo DRC haiwezi kuwa nchi huru tena na dalili hizo hazipo.
 
Back
Top Bottom