Mafundisho ya Joomla Sehemu 1.1 na 1.2 toka AfroIT

Mafundisho ya Joomla Sehemu 1.1 na 1.2 toka AfroIT

Kilongwe

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2008
Posts
423
Reaction score
116
20110216195829.jpg


Lengo la teknolojia ni kurahisisha na kuboresha maisha ya jamii. Hivyo AfroIT tukiwa kama wana jamii tumeanza kuandaa mafundisho ya kutengeneza tovuti kwa kutumia joomla.

Katika mafundisho hayo,mkufunzi Mkata Nyoni atatumia na kugawana uzoefu wake kwenye hii nyanja ya utengenezaji wa tovuti kwenye kipengele cha joomla ambapo hadi mwisho wa safari utaweza kuwa na tovuti nzuri na kuvutia.

Joomla Sehemu ya Kwanza - nenda Hapa

Walengwa wa mafundisho haya ni jamii nziima,ila ili kuhakikisha tunaenda sawia ni muhimu uwe na msingi ufuatao

- Ufahamu wa kompyuta kwa uchache wake

-Ufahamu wa HTML,PHP, na CSS kwa uchache wake(Kama hujui kabisa unaweza kusikila mafuundisho kwani mafundisho yamezingatia sana mlengo wa design na sio development)

-Ufahamu wa kucheza na picha(uhariri),Photosshop inashauriwa.

-Moyo na nia ya kupata ujuzi na kujua mambo mengi

Kozi hii ni ndefu kidogo ambapo itatuchukua mwezi mmoja hadi miwili huku tukitoa mafundisho mawili kwa wiki.

Tutachukua mtindo wa NUNU(Nini Unataka Ndio Unapata),hapa tunamaanisha,hadi mwisho wa safari basi tutaweza kuwa na tovuti bora kabisa.

Kama tulivyojiwekea malengo,baada ya kukamilisha mafundisho,tutaandaa CD na kuzigawa BURE mavyuoni na mashuleni ili kukuza hari na mapenzi ya ICT.

Hivyo kama unaona unaweza kuchangia kwa kusambaza,kuwezesha uchapaji wa CD nyingi zaidi nk basi tuandikie kwenda webmaster@afroit.com .

AfroIT Group
 
Mkuu Kilongwe, Tuko pamoja, hii imetulia sana. Tafadhali ikiwezekana, hizi video usioziondoe,kadri unavyoleta shule kila wiki ni vyema ukaziacha ili wale wanaochelewa kuziona nao wapate kuzisoma hapo baadae.
 
Video zote huwa haziondolewi ila zinabadilishwa na mpya,ili kupata video za awali unatakiwa kwenda Video Training ndani ya AfroIT - Elimu ni ushindi halafu chini kwenye Category Unachagua video unayotaka,za jumla zipo kwenye Development->CMS hapo utaona zote za jumla ba hata zile za Wordpress.

Pia ili kuwasaidia wale ambao hawana uwezo wa kusikiliza live,tutakuwa tunaziweka kwenye Hotfile baada ya kamuda.
 
Back
Top Bottom