stanluva
Senior Member
- Apr 7, 2009
- 153
- 33
Mfumo wa uombaji wa nafasi za mafunzo ya ualimu katika ngazi ya stashahada umefunguliwa. Kama una ndugu au jamaa mtaarifu ikiwa anavigezo vilivyoanishwa anaweza kutuma maombi. Ili kuweza kuona kozi na sifa zinazohitajika tafadhali soma maelekezo kwa kubonyeza hapa.
===
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia anatangaza nafasi za mafunzo ya Ualimu kwa ngazi ya Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari. Waombaji wa mafunzo haya ni wahitimu wa Kidato cha NNE na SITA wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Tatu (I-III). Wizara inakaribisha maombi ya kujiunga na mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Serikali na visivyo vya Serikali kwa kuzingatia sifa zilizobainishwa katika tangazo hili.
SIFA ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU
Sifa za jumla za kujiunga na Mafunzo ya Ualimu Tarajali ngazi ya Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali na Msingi ni wahitimu wa Kidato cha Nne wenye ufaulu wa Daraja la I-III . Waombaji wa Stashahada ya Ualimu Elimu ya Sekondari ni wahitimu wa Kidato cha Sita wenye ufaulu wa Daraja la I-III kwa kiwango cha “Principal Pass” mbili (02) za masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari kidato cha I-IV. Aidha kwa waombaji ambao moja ya “Principal Pass”mbili ni somo la Uchumi “Economics”, wanaweza kuomba kozi za fani ambazo ni Michezo (Physical Education and sports), Muziki, Sanaa za Ufundi (Fine Arts), na Sanaa za Maonesho (Theatre and Performing Arts).
AINA YA MAFUNZO NA SIFA
Jedwali lifuatalo linaonesha aina ya mafunzo ya Ualimu, sifa za kujiunga, vyuo vinavyotoa mafunzo hayo na muda wa mafunzo
A. MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA YA ELIMU YA AWALI NA MSINGI
B. MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI
C. MAFUNZO YA UALIMU KAZINI (STASHAHADA ELIMU MSINGI NA STASHAHADA ELIMU SEKONDARI)
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
===
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia anatangaza nafasi za mafunzo ya Ualimu kwa ngazi ya Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari. Waombaji wa mafunzo haya ni wahitimu wa Kidato cha NNE na SITA wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Tatu (I-III). Wizara inakaribisha maombi ya kujiunga na mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Serikali na visivyo vya Serikali kwa kuzingatia sifa zilizobainishwa katika tangazo hili.
SIFA ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU
Sifa za jumla za kujiunga na Mafunzo ya Ualimu Tarajali ngazi ya Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali na Msingi ni wahitimu wa Kidato cha Nne wenye ufaulu wa Daraja la I-III . Waombaji wa Stashahada ya Ualimu Elimu ya Sekondari ni wahitimu wa Kidato cha Sita wenye ufaulu wa Daraja la I-III kwa kiwango cha “Principal Pass” mbili (02) za masomo yanayofundishwa katika shule za sekondari kidato cha I-IV. Aidha kwa waombaji ambao moja ya “Principal Pass”mbili ni somo la Uchumi “Economics”, wanaweza kuomba kozi za fani ambazo ni Michezo (Physical Education and sports), Muziki, Sanaa za Ufundi (Fine Arts), na Sanaa za Maonesho (Theatre and Performing Arts).
AINA YA MAFUNZO NA SIFA
Jedwali lifuatalo linaonesha aina ya mafunzo ya Ualimu, sifa za kujiunga, vyuo vinavyotoa mafunzo hayo na muda wa mafunzo
A. MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA YA ELIMU YA AWALI NA MSINGI
| Na. | AINA YA MAFUNZO | SIFA ZA KUJIUNGA | VYUO | MUDA WA MAFUNZO |
| 1 | Stashahada ya Ualimu Elimu ya Msingi |
| Bustani TC, Ilonga TC, Kabanga TC, Katoke TC Kitangali TC, Kinampanda TC, Mandaka TC Mtwara (U) TC, Mhonda TC, Murutunguru TC Mpuguso TC, Singachini TC, Tandala TC, Tarime TC Vikindu TC, Nachingwea TC, Ndala TC, Mamire TC, Shinyanga TC, Marangu TC, na Dakawa TC | Miaka 3 |
| 2 | Stashahada ya Ualimu Elimu Maalum |
| Patandi TC | Miaka 3 |
| 3 | Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali |
| Kinampanda TC, Nachingwea TC, Mhonda TC Tarime TC, Vikindu TC, Mpuguso TC, Mandaka TC, Singachini TC Murutunguru TC, Kabanga TC, Bustani TC Ndala TC, Katoke TC, Bunda TC, Tarime TC | Miaka 3 |
| 4 | Stashahada ya Ualimu Elimu kwa Michezo |
| Tarime TC, Mtwara (K) TC, Ilonga TC | Miaka 3 |
| 5 | Stashahada ya Ualimu Elimu ya Msingi (English Medium) |
| Dakawa TC, Marangu TC | Miaka 3 |
B. MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI
| 1 | Stashahada ya Ualimu Sayansi na Hisabati | Ufaulu wa Kidato cha VI kwa kiwango cha daraja la I-III na alama zisizopungua ‘Principal Pass’ mbili katika masomo ya Tahasusi za Sayansi, Hisabati na TEHAMA kwa kuzingatia Masomo yanayofundishwa katika shule za Sekondari kama ifuatavyo: Basic Mathematics, Biology,Food &nutrition , Geography, Chemistry, Physics, Agriculture Science, Information and Computer Studies (ICS) na Computer Science. | Mamire TC, Monduli TC, Mandaka TC, Butimba TC, Kleruu TC, Songea TC, Tukuyu TC, Kasulu TC, Mpwapwa TC, Morogoro TC, Korogwe TC | Miaka 2 |
| 2 | Stashahada ya Sayansi ya Jamii, Biashara na Lugha | Ufaulu wa Kidato cha VI kwa kiwango cha daraja la I-III na alama zisizopungua ‘Principal Pass’ mbili kwa kuzingatia masomo yanayofundishwa katika shule za Sekondari Kidato cha I-IV. Masomo yanayofundishwa katika shule za Sekondari kidato cha I-IV ni : Kiswahili, English, History, Geography, Civics, Commerce and Book keeping. | Bunda TC, Mtwara (K) TC, Marangu TC, Nachingwea TC, Shinyanga TC, Mandaka TC, Mpuguso TC, Dakawa TC, Butimba TC, Tabora TC, Morogoro TC, Tarime TC, Shinyanga TC, | Miaka 2 |
| 3 | Stashahada ya Ualimu Michezo, Muziki, Sanaa za Ufundi na Sanaa za Maonesho | Ufaulu wa Kidato cha VI kwa kiwango cha Daraja la I-III na alama zisizopungua ‘Principal Pass’ mbili pamoja na ufaulu wa masomo ya liyoainishwa katika mtihani wa kidato cha IV kwa kila kozi kama ifuatavyo: | Butimba TC | Miaka 2 |
| (a) Sanaa za Ufundi: masomo ya Fine Arts, Basic Mathematics, Chemistry, History, Physics, English na Civil Engineering. | Butimba TC | Miaka 2 | ||
| (b) Sanaa za Maonesho: masomo ya English, Literature in English, Kiswahili, Geography na History. | Butimba TC | Miaka 2 | ||
| (c) Muziki: masomo ya ‘Music’ pamoja na masomo ya English, Kiswahili, Physics, Geography, History na Biology. | Butimba TC | Miaka 2 | ||
| (d) Elimu kwa Michezo: masomo ya Physical Education and sports, Languages, na Biology. | Butimba TC na Mtwara (K) | Miaka 2 |
C. MAFUNZO YA UALIMU KAZINI (STASHAHADA ELIMU MSINGI NA STASHAHADA ELIMU SEKONDARI)
| Na. | AINA YA MAFUNZO | SIFA ZA KUJIUNGA | CHUO | MUDA WA MAFUNZO | |
| 1 | Stashahada Elimu Maalum (Mafunzo kazini) Msingi | Mwalimu kazini aliyepitia mafunzo ya Ualimu Astashahada, Stashahada au Shahada kwa ufaulu wa angalau somo moja la Sayansi katika mtihani wa Kidato cha Nne na awe na uzoefu wa kazi ya Ualimu usiopungua miaka miwili (2) | Patandi TC | Miaka 2 | |
| 2 | Stashahada Elimu Maalum (Mafunzo Kazini) Sekondari | Mwalimu kazini aliyepitia mafunzo ya Ualimu Ngazi ya Stashahada, Stashahada ya Elimu ya Juu au Shahada mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu usiopungua miaka 2; na Aliyefaulu masomo ya Sayansi katika mtihani wa Kidato cha Sita | Patandi TC | Miaka 2 |
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
- Tangazo hili halitawahusu wahitimu wa kidato cha Nne 2019 waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu 2020/2021 kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI . Aidha wahitimu wengine waliohitimu kuanzia 2017 hadi sasa wanaruhusiwa kutuma maombi.
- Waombaji wa Mafunzo ya Ualimu katika vyuo vya Ualimu vya Serikali wanatakiwa kujisajili na kufanya maombi kielektroniki kupitia tovuti (TCM , au BOFYA HAPA KUJISAJILI/KUINGIA KWENYE MFUMO WA MAOMBI YA UALIMU)
- Waombaji wa Mafunzo ya Ualimu kwa vyuo visivyo vya Serikali watume maombi yao moja kwa moja katika Chuo anachotaka kusoma na Vyuo husika viwasilishe sifa za waombaji Baraza la Mitihani Tanzania kwa uhakiki.
- Waombaji wa mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Serikali watachagua tahasusi hadi tatu (03) kwa kuanza na ile anayoipenda zaidi.
- Waombaji wa nafasi za mafunzo walio kazini wanapaswa kuwa wamehitimu mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti, Stashahada au Shahada.
- Walimu Kazini watapaswa kuambatisha barua ya ruhusa kutoka kwa waajiri wao;
- Majibu kwa watakaochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu yatatolewa kupitia tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na katika Vyuo vya Ualimu walivyochaguliwa.
- Fomu za kujiunga na Mafunzo zitatolewa kupitia tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (www.moe.go.tz , au BOFYA HAPA KUPATA FOMU) na Chuo atakachopangwa mwombaji kwa kutumia anuani yake. Waombaji wote wanashauriwa kuandika anuani kamili, barua pepe na namba ya simu inayopatikana kwa mawasiliano zaidi.
- Mwisho wa kutuma maombi kwa Mafunzo ya Ualimu ni tarehe 10/09/2020.