Mafuriko:Vodacom waanza kampeni ya simu; kuchangia Vod. Foundation


Utu wa mtu haupotei tu ikiwa kuna majanga. Utu wa mtu unapotea ikiwa kwa sababu yeyote ile atakosa mahitaji muhimu kwa maisha yake. Ni rahisi sana kuhalalisha matendo ikiwa kuna urgency/emergency na mfano mzuri ni majanga. Hapa kila mtu atataka kujifanya mwema. Lakini ninakwambia, wako watu wanaishi maisha yanayolingana hivi sasa na yale ya wakazi wa kilosa na maeneo mengine yaliyokumbwa na mafuriko kama ndio maisha yao ya kawaida. Hawana makazi, hawana chakula na hawana huduma za afya. Sisi wengine tumepata bahati ya kufanya shughuli zinazotupeleka kila siku kwa watu wa aina hiyo. Nobody think of them, kwanini, kwakuwa sio rahisi kuijustfy hiyo hali kama janga, lakini ni janga. Hawa hawawezi kusaidiwa na TPN, na Jamii forums, na Michuzi na red cross na red alert, wala hawawezi kusaidiwa na kina mkulo na lukuvi.
Je wanapaswa kusaidiwa na nani?
 

Kwahiyo unashawishi wanajf na wengine waanze kuflood Mail box za watu ? hujui kwamba huo ni uhalifu ? Mimi nimeuliza kisheria JF na TPN wanakusanyaje michango wanamakubaliano gani ambayo wanaJF wengine hawajui sisi ni wanachama tunatakiwa kujua sasa kwamba jf sasa ina kitengo cha kukusanya michango na kitengo hicho kimesajiliwa kisheria
 

Naongezea yafuatayo

  1. Tusambaze ujumbe kwa watanzania waishinikize serikali kupeleka huduma zote muhimu kwenye maeneo yote yaliyokumbwa na mafuriko na sio kufanya safari za uswisi kwenye mikutano isiyo tija wakati nchi ipo kwenye JANGA. Uwezo wa kupeleka huduma za msingi serikali inayo, kama vile ilivyo na uwezo wa kujenga reli haraka ili madini yapite kutoka mikoa ya kanda ya ziwa
  2. Tupeleke ujumbe kwa spika awatake wabunge wapitishe michango kama ile waliyopitisha na kuipa Taifa Stars ilipoifunga timu ya burkina faso. Karibu sh milioni 400 zilichangwa wakati ule
  3. Tusiandike barua kwa mkurungenzi wa vodacom, ila tusambaze tu ujumbe kwa wananchi kuwa wagomee harambee hiyo
  4. Tuandike ujumbe kwa Vodacom kuwa wapunguze gharama zao za promotion, ili wapunguze gharama za utumiaji simu kwa wananchi kwani kwa kutofanya hivyo hawawezi kujusfy committment yao kwa jamii
  5. Tusisubiri majanga ya mafuriko ndio tuanzishe mijadala kama hii, bali siku zote tutengeneza foundation ambayo inaweza kukabiliana na matatizo kama haya. Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya dharura na mismanagement of resources
 


mkuu soma hiyo poster yao ya rangi nyekundu. Kama wote tungekuwa tunajenga nyumba ile ile wala kusingekuwa na ugomvi..
 

FYI:
1. Executive Committe ya TPN ilikutana tarehe 09-01-2010 na kukubaliana kuanzisha kampeni hii ikishirikiana na wadau wengine.

2. TPN constitution inaruhusu TPN kuraise fund na kusaidia NGO/Socity nyingine

3. TPN constitution inasimamia pia kuboresha maisha ya Watanzania.

4. Viongozi wa Kitaifa / Red Cross walitoa mwito wa kuomba misaada

5. TPN na Wadau ilifanya mazungumzo na Red Cross na kuijulisha azma yake ya kuitikia wito wake na kusaidia kuichangia.
 
mkuu soma hiyo poster yao ya rangi nyekundu. Kama wote tungekuwa tunajenga nyumba ile ile wala kusingekuwa na ugomvi..
Nimekuelewa Mwanakijiji. Nilidhani wakishachangisha wanazipeleka moja kwa moja kwa walengwa kama TPN walivyofanya kupitia Red Cross. Sijui nani ataishtua serikali yetu ambayo baadhi ya viongozi wake "maarufu" au mawakala wao wana hisa huko VODACOM!
 
crap, as usual
 

Watueleze pia kwamba hiyo shs 250 kwa kila SMS wanayokata inapelekwa yote kwa waathirika wa mafuriko? Au wanapeleka tofauti kati ya gharama za SMS (Shs. 54 per SMS) na hiyo Tshs. 250? Halafu jinsi wasivyo makini, tangu lini CHARITY WORK ikatozwa kodi? Maana wanasema Shs. 250/SMS including VAT!!!???? This is pure business in the name of CHARITY, hivi hawana washauri?

Shame on them!
 
Hivi majuzi tumeshuhudia mpango wa vodacom wa kuchangisha fedha kutoka kwa wananchi kwaajili ya maafa. Sioni kama ni jambo baya lakini kwa mtazamo wangu hawakupaswa kuchangisha wenyewe kama vodacom.

Vodacom kama vodacom inapaswa kuwachangia wananchi sawa na mwananchi mwingine ambaye wanamuomba achangie hasa kwenye matatizo kama haya ya majanga ya dharula. Wanaopata matazizo ya maafa ni pamoja na wateja wao au kwa maana nyingine faida nyingi wanayoipata wanapaswa kurudisha kwa wananchi kiasi fulani.

Tumeona kazi nzuri inayofanywa na VodaCom Foundation basi ingejipanua na kuonyesha inasaidia na kwenye mafuriko kwa mfuko wa VodaCom Foundation. Hii ya kuchangisha au kutengeneza kitengo cha wananchi kujitolea ingekuwa ni kuwasaidia shirika fulani au taasisi fulani au idara fulani katika serikali. Itakuwaje kila Kampuni ya simu ikianzisha kitengo kama hicho? Hainiingii akilini eti vodacom hao hao wafanyabiashara tena wanaotengeneza faida kubwa sana eti nitoe tena hela kuwapelekea hao hao. Nafikiri mmekosea approach yenu. Nataka kuamini kwamba mmepata pressure fulani kufanya hivyo bila kuona upande mwingine wa shilingi.

Ni hayo tu kwa leo.
 

Mbona hujasema JF imeingiaje hapo ? au ndio wadau wengine ?
 

Ndio maana kumeandikwa masharti na vigezo kuzingatiwa sasa uliza hayo kwanza kabla ya kuanza kulaumu

Unakumbuka kulikuwa na topic moja mwanakijiji akishauri watu wagomee huduma za vodacom mwaka jana ? kilichotokea kule leo hii tena amekuja kwa njia nyingine
 
Naona tunataka kuiharibu JF sasa kwanini mada hii usingeunganisha na ile inayoendelea
 
sidhani kama ni Vodacom Alert soma vizuri ni Vodafone Red alert bana. hata nembo ni ya Vodafone kaka. nijuavyo mimi Vodafone foundation kwa kushirikiana na mshirika wake Vodacom Tz (Vodacom Foundation) wame launch hiyo huduma kwa wateja wake waweze kuchangia kupitia sms for the good cause. Vodacom kama kampuni inao uwezo wake wa kuchangia vile vile, hiihuduma inamruhusu mteja yeyote pande zozote za nchi hii kuchangia as little as 250/-. nikiwa kule Musoma na nna only tshs 250/- ntaipeleka wapi? RED CROSS? kuna ofisi pale Musoma? au kule Mpitimbi songea kuna RED CROSS pale? je wataipokea hiyo shs 250/- yangu? hii inakupa fursa mteja wa Vodacom kuchangia popote pale ulipo ktk nchi hii kwa kiwango hicho kidogo. Nijuavyo mimi VODAFONE wameongeza shares zao ktk Vodacom SA, na wao sasa ndio wenye shares kubwa na ndio onwer wa Vodacom SA(South Africa).Outomatically na hii Vodacom ya Bongo inakuwa iko chini ya VODAFONE sasa. Vodafone sasa inajitambulisha katika kusaidia walioathirika na maafa ya mafuriko, kwa kusaidiana na mshirika wake Vodacom TZ, ktk hizo foundations ambako hata VODAFONE ipo, ndio wanakuwezesha na wewe uweze kuchangia waliopatwa na maafa. kama ilivyo ada yetu tumesha jaji kwamba Vodacom badala ya kuchangia wanatuchangisha. lkn wapo watu wanaotaka kuchangia lkn hawajui wapeleke wapi michango yao na hawana mamilioni ya mchango lkn wana vijisenti kidogo km hiyo 250/-. Habari nilizonazo ni kwamba Vodafone alert Tanzania ni ya kwanza kuwa launched ktk nchi zote ambazo Vodafone ina operate. Aim yake ni kusaidia kuchangishana wakati wa majanga kama haya ktk nchi ambazo Vodafone group ipo. Michango bado inaendelea kuchangishwa sijasikia kama imesitishwa, sijasikia au kusoma ni makampuni mangapi tayari yameshachangia yenyewe, sijasikia tamko toka VODACOM kwamba inachangisha TU na haitatoa msaada yenyewe kama kampuni, serikali haijaweka deadline, sisi kama wanachi wa kawaida ni vizuri tukasubiri tuone hii Vodacom inaolaumiwa itafanya nini mwishoni, itatoa pesa yake yenyewe au itachangisha tu. Mwingine alidai ETi VAT ya nini kwenye hizi SMS? sasa hilo suala la VAT ni la ZAKAYO MTOZA USHURU(TRA) na si Vodacom, nijuavyo mie ukifanya biashara lazima ulipe kodi, kwa hiyo hapo VODACOM wanalipa kodi. Mwingine alisema Vodacom kwa nini isipeleke hiyo misaada kwa RED CROSS? kwani wao ndo waratibu wa misaada kwenye majanga mbali mbali, lkn nimeona akina SHYROSE BHANJI wamekwenda mpaka Kilosa (NMB) wakakabidhi misaada kule, kuna wahindi wafanya biashara pale Morogoro, wametoa misaada yao bila kuihusisha hiyo RED CROSS, haikuulizwa kwanini hawakuwasilisha RED CROSS. Anyway Poleni sana wandugu zangu wa kilosa, kuanzia Mbwade, Kimamba, Chanzuru, MADOTO, KILOSA YENYEWE, Ilonga nimeishi huko, mitaa yote naijua kuna secondary flani nilisoma, nakumbuka tukienda Kilosa mjini kuna sehemu mitaa flani ilikuwa ikiitwa DINGILISUSU, tukienda kupata menu pale dah!!! ilikuwa imesimama kinooooooooooooma.
 

Hayo ya MKJJ na kuomba wananchi wagomee huduma za Vodacom ni mengine. Tuzungumzie ukweli hapa tangu lini misaada ikatozwa kodi? Halafu ina maana Vodacom watapata faida kubwa kwa kuuza SMS nyingi sana katika mchakato mzima wa kuchangisha hizi fedha.

Wangeona aibu, kwani tulitegemea watoe msaada wa haraka kwa waathirka wa mafuriko kutokana na faida wanayotengeza toka kwa wananchi kila siku. Leo hii wanageuza majanga ya asili kuwa mtaji wa kujiongezea pato na kujitangaza? Aibu kubwa sana!
 
Mbona hujasema JF imeingiaje hapo ? au ndio wadau wengine ?

You got it right. Pia angalia Press Release ya TPN na JF. If u need more official confirmations, please let me know. Sidhani kama ni busara kila kitu kuweka hapa.

TPN is open in every aspect to the dot.

Karibu Shy tegemeo letu katika ICT.
 
Haya ndiyo matatizo ya kuendesha nchi ki-MADRASA MADRASA kila mtu anafanya atakalo, Kampuni kubwa kama VODAFONE hawawezi kufanya upuuzi huu kwenye nchi imara.
 
You got it right. Pia angalia Press Release ya TPN na JF. If u need more official confirmations, please let me know. Sidhani kama ni busara kila kitu kuweka hapa.

TPN is open in every aspect to the dot.

Karibu Shy tegemeo letu katika ICT.


Mkuu naomba niwapongeze kwa juhudi zote zilizofanyika kuhusiana na jambo hili.Mmeonesha mfano na kudhihirisha kwamba tukidhamiria tunaweza.
 

Ndugu yangu inaonyesha wewe ni mfanyakazi wa vodacom ndio maana una uhakika kabisa kwamba wanapata faida au ni mfanyakazi wa kampuni nyingine ya simu ambao ni wapinzani wa vodacom kwa maneno uliyotamka hapo juu
 

Niliuliza swali Vodacom ni mali ya nani? Mkuu Mtsimbe akanipa jibu hili na maelezo mengine kuhusu Vodacom Foundation.

Bado tu mnashangaa kuhusu Vodafone or whatever you call it, kuja na 'utapeli' wa aina hiyo? Jina la huyo Bwana mkubwa wakati wote linaendana na hujuma ya aina fulani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…