Mafuta Dar yaanza kuadimika...

frema120

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2012
Posts
5,098
Reaction score
1,339
hAbari wana JF

Nimezunguka takirban shell za mafuta 7 sasa bila kupata mafanikio ya kuweka mafuta kwenye gari.....
~ je mnaweza kunisaidia yanapatikana wapi sasa?
~ je ni kwanini shell zimefungwa?
~ je ewura inatambua hili / au imesema chochote?
~ au kunanini wakuu?

Nawasilisha!

V
SENGEREMA
 

Umezunguka sheli zipi/wapi??
 
hilo linawezekana unajua nchi hii inakikundi cha watu wasiozidi 50, ambao wakiamua mwaka mzima hakuna umeme tz nzima ni kweli hakuna umeme ili wao wauze majenereta na wapige 10 % ya mafuta, wakiamua mwaka mzima hakuna maji ni kweli hakuna maji. So inawezekana hilo
 
Ni mbinu za kupandisha bei ya mafuta, hawa wauza mafuta ni genge la wahujumu uchumi, ila Diezel wanauza Petrol ndio wamezificha.
 
Bei mpya inanukia ukiona hivyo?
 

Mkuu pole sana na adha ya mafuta, ila kuweka mambo sawa Watanzania wengi(hasa vijana wa dotcom) hupenda Kituo cha mafuta kukiita Shell, ... kitu ambacho si sahihi hilo ni jina la Kampuni ya mafuta miaka hiyo ya 47, so ni kama BP, OilCom na mengine mengi, so its called a Petrol Station/ kituo cha mafuta...
Hutaki unaacha...
 
Ni kweli wameanza kuyaficha wakisubiria bei mpya. Si unajua tena mwezi ndio unakatika na bei kidogo ilikuwa chini.
Nchi hii kila mtu anaamua atakalo. Ndio madhara ya kuwa na OMBWE la uongozi.
 
Nilikosa pale Banana,

Nikajaza cha ng'ombe/ kawawa, nikamsikia dada anayeuza mafuta, anamwambia mteja kwamba aweke ya kutosha karibu yanakwisha.

Nlikuwa nimeongeza, nikaenda shell nyingine city center, ile pale india street/ aggrey nikaamua kujaza ful tank.

Nahisi, wenye mafuta wanasubiri ewura ipandishe bei, ili wapunguze makali ya bei ilivyoshuka kutoka Ths 2300 hadi 1994
 

POMPO nimekukubali aisee! hawa watoto waliozaliwa awamu ya nne ya JK wanajifanya wanajua kila kitu!!
 

its filling station and not petrol station
 

Hata torch inaitwa KURUNZI (KRUNTZ a torch brand from Germany) Kaptula ya kuchezea mpira inaitwa bukta( BUKTA ni brand kama ADIDAS).........ndivyo tulivyo

 
Mhhhhhhhhh Tanzania kila kitu kinawezekana!! Fujo, udini, ukabila, ukanda, ufisadi, ubepari, ukabaila, etc etc!!! Hayakuwepo ila yapo kwa sasa na yameshamiri!!!! Mwenye pesa mpishe Tz kila kitu ataamua!!! Hii ni kwa sababu tunawapigia magoti wakti wa uchaguzi ili kupata hela ya kuhonga!!! Sasa kwa nini asikuyumbishe atakavyo?
 
Sasa mbona mleta uzi katokomea?


Ama alikuwa anatuchungulia tu nini?
Tena akome kabisa!
 
Hivi serikali imeshindwa kuweka ruzuku ili kumpunguzia gharama mlaji kwenye ule mradi wa kubadilisha mfumo wa magari ili yaweze kutumia gesi yetu ya kizalendo?? Itaokoa pesa kiasi gani za kununulia nishati hii kutoka nje??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…