Mafuta ya Kula yaliyoathiri Wakazi wa Yombo Dovya (Temeke) yadhibitiwe yasisambae zaidi na Je, waathirika hawasaidiwi?

Mafuta ya Kula yaliyoathiri Wakazi wa Yombo Dovya (Temeke) yadhibitiwe yasisambae zaidi na Je, waathirika hawasaidiwi?

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Screenshot 2025-01-23 130930.png

Screenshot 2025-01-23 130758.png
Hivi karibuni iliripotiwa taarifa ya zaidi ya Wakazi 200 wa Mtaa wa Yombo Dovya, Wilayani Temeke kuathirika kwa kubabuka ngozi, kuumwa macho na wengine kupata changamoto ya mikono katika maeneo mbalimbali mwilini baada ya kudaiwa kutumia mafuta ya kula yanayodaiwa kuwa na sumu.

Ilielezwa kuwa mafuta hayo inasemekana yamenunuliwa katika duka la mfanyabiashara anayefahamika kwa jina la Kamau maarufu kama Mangi ambaye naye alipohojiwa alisema alinunua Tandika.

Baada ya taarifa hiyo mamlaka za Usalama zilitoka na kueleza kuwa watuhumiwa walikamatwa kwa ajili ya hatua za kisheria huku ikielezwa unafanyika uchunguzi wa mafuta hayo kubaini tatizo.

Imepita wiki sasa kupitia vyombo vya habari, Wananchi wamekuwa wakiendelea kudai kwamba bado hawajapatiwa huduma stahiki huku wengine kupitia vyanzo mbalimbali wanadai hata bado hawajafanyiwa vipimo vya aina yoyote na hakuna msisitizo wa tahadhari kuchukuliwa.


Pamoja na hivyo, bado hakuna taarifa za mwendelezo kutoka kwenye mamlaka za juu hata ngazi ya Mkoa, Wizara ya Afya, Mamlaka za Ubora wa Vyakula kuhusu suala hilo, badala yake chanzo cha kutoa taarifa inaonekana amebakia kuwa Mwenyekiti wa Mtaa, huku ikielezwa kuwa visa vingine vya aina hiyo vinaendelea kujitokeza, wahusika wanaotuhumiwa tunaambiwa walikamatwa na sasa wapo nje kwa dhamana.

Baada ya kusikia na kuona hali hiyo napata mashaka juu ya uwajibikaji wa mamlaka kwenye suala husika ambazo zilitakiwa kubeba suala hilo ambalo linagusa afya za Wananchi wetu, nabakia kujiuliza nini kipo nyuma ya pazia kwa ukimya huo mpaka kushindwa kuchukua hatua za kusaidia waathirika?

Wito wangu kwa mamlaka za Kiserikali kwanza wawasaidie Wananchi walioathirika, pili kuchukua hatua za haraka kubaini na kueleza chanzo cha tatizo hili kuondoa hofu Wananchi wengine kutokana na sintofahamu iliyopo sasa.

Mpaka sasa chanzo rasmi cha tatizo hakijaelezwa ni wiki imepita tunaambiwa uchunguzi unaendelea, tunajiuliza mpaka uchunguzi ukamilike watakuwa wameathirika wangapi?

Nini kinachelewesha uchunguzi kubaini kulikuwepo na changamoto gani kwenye mafuta yanayodaiwa kusababisha changamoto hiyo? Ni vyema tunafahamu ili kama kuna uzembe wahusika wawajibike.

Hili linanikumbusha lile la Wananchi wa Kijiji cha Imalamate, Wilaya ya Busega (Simiyu) ambao waliathiriwa na maji yanayodaiwa kuwa na sumu kutoka katika Mgodi wa Dhahabu wa EMJ, kilichotokea DC akasema Mgodi ulipigwa faini na yale maji yakadhibitiwa lakini walioathirika sijui kama walisaidia.

Sasa swali la kujiuliza Mamlaka za Afya zimeshajua muuzaji wa mwanzo wa mafuta hayo? je mafuta yalikuwa na vitu gani hasa? Hayo mafuta yamesambaa kwa Watu wangapi au maeneo mangapi? Kuna mkakati gani wa kudhibiti Watu wasiendelee kuumia zaidi? Wale walioathirika na hawana hela za kujihudumia wanasaidiwa vipi?
 
Natamani hayo mafuta yawafikie viungozi wetu nao watokwe na mapele makalioni hasa chalamila hapo ndipo tutakapoanza kuelewana lugha bila kujalisha ni ile lugha ya kunena kwa lugha au kiburundi au kimatengo cha msingi tuweze kuelewana tu.
 
Huyo mama kweny video ni Shangaz yang,Nilipita kumpa pole lakin hali yake y kiuchumi siyo nzuri,anasema walipelekwa Hospital mara moja(1) lakin Afya zao hazijatengemaa , kiugwana tu Serikali haijachukulia hili swala kiuzito waathilika ni wengi na Sumu hiyo ni hatari kwa madhara kwa waliyotumia, mfano kam ingekuwa Sumu y kutowa Uhai basi wananchi(jirani) zangu 200 leo hii wasinge kuwepo ...
Shame : on Government 😔 haiwi Seriously.
 
Back
Top Bottom