Mafuta ya Zanzibar yataifanya Tanzania kuwa tajiri kama Libya?

Mafuta ya Zanzibar yataifanya Tanzania kuwa tajiri kama Libya?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kuna matumaini kuwa huenda mafuta yakagundulika Zanzibar. Ni habari njema!

Hilo likitukia, Tanzania itakuwa tajiri kama Libya ilivyokuwa kabla ya kuangushwa kwa utawala wa Gaddafi?

Sina uhakika kama Gaddafi alikuwa na Maalmasi, Matanzanite, Madhahabu, na Mamikaa ya mawe kama Tanzania, lakini kwa kuwa hayajatusaidia, labda tujaribu kwenye mafuta!

Hata gesi ilipoanza kuchimbwa, kulikuwa na matumaini ya hali kubadilika, lakini ni miaka sasa sisi tulioko huku mikoani hatujui kama bado inachimbwa au la! Hatuuoni utofauti wowote!

Labda, kwa kuwa Maserengeti, Mangororo, na Mamikumi, mabandari na mamito yameshindwa kututajirisha kama mafuta yalivyoitajirisha Libya, tujaribu mafuta!

Tutarajie nini mafuta yatakapoanza kuvunwa Zanzibar? Tanzania itakuwa tajiri?
 
Ubaya ni kwamba CHAKO NI CHETU , CHANGU NI CHANGU.

Kama unazaidi ya D mbili umeshanielewa
 
Kuna matumaini kuwa huenda mafuta yakagundulika Zanzibar. Ni habari njema!

Hilo likitukia, Tanzania itakuwa tajiri kama Libya ilivyokuwa kabla ya kuangushwa kwa utawala wa Gaddafi?

Sina uhakika kama Gaddafi alikuwa na Maalmasi, Matanzanite, Madhahabu, na Mamikaa ya mawe kama Tanzania, lakini kwa kuwa hayajatusaidia, labda tujaribu kwenye mafuta!

Hata gesi ilipoanza kuchimbwa, kulikuwa na matumaini ya hali kubadilika, lakini ni miaka sasa sisi tulioko huku mikoani hatujui kama bado inachimbwa au la! Hatuuoni utofauti wowote!

Labda, kwa kuwa Maserengeti, Mangororo, na Mamikumi, mabandari na mamito yameshindwa kututajirisha kama mafuta yalivyoitajirisha Libya, tujaribu mafuta!

Tutarajie nini mafuta yatakapoanza kuvunwa Zanzibar? Tanzania itakuwa tajiri?
Tuanzie kwenye gesi kwanza,hayo mengine ni ndoto.Kwanza Muungano wenyewe wa moto sembuse mafuta.
 
Zanzibar wanajitambua waliyaondoa mafuta kwenye masuala ya muungano.watayatumia wao na kutuuzia watanganyika Kwa bei sawa na mafuta tunayonunua ulaya.wazanzibari wajanja siyo kama watanganyika ni wajinga wajinga tu ambao wanakubali Cha kwao ni Cha wote na Zanzibar
 
Tafakari upya tena zanzibar ndo itakua tajiri sio tanzania
 
Wabongo kweli tuna low IQ, bado tu hamjachoka kudanganywa? Haya tuendelee kusubiri, nyama ziko chini
 
Back
Top Bottom