Mafuta yapanda Bei, EWURA imetangaza Bei Mpya za Machi 2023

Mafuta yapanda Bei, EWURA imetangaza Bei Mpya za Machi 2023

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), inatangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia Jumatano, Tarehe 1 Machi 2023. Pamoja na kutambua bei hizo, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:- (a Kwa Machi 2023, bei za rejareja za mafuta ya petroli,dizeli na mafuta ya taa yaliyopokelewa kupitia Bandari ya Dar es Salaam yamepandaa kwa shilingi 149/Lita, shilingi 25/lita na shilingi 37/lita, mtawalia, ikilinganishwa na toleo la tarehe 1 Februari 2023.

(b) Kwa Mikoa ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara), bei za rejareja za Machi 2023 kwa mafuta ya petroli na dizeli yanapungua kwa shilingi 64/Lita na shilingi 209/lita, mtawalia, ikilinganishwa na toleo la tarehe 1 Februari 2023.

Kutokana na kuisha kwa mafuta ya taa kwenye matanki ya kuhifadhia yaliyopo Tanga, waendeshaji wa vituo vya mafuta kwenye mikoa ya Kaskazini wanashauriwa kuchukua mafuta ya taa kutoka katika bandari ya Dar es Salaam na hivyo bei za rejareja za mafuta ya taa katika mikoa hiyo itakuwa kulingana na gharama za kupokelea mafuta ya taa kupitia Bandari ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.

(c) Kwa Mikoa ya Kusini (Mtwara, Lindi, and Ruvuma), bei za rejareja za Machi 2023 kwa mafuta ya petroli zinaongezeka kwa shilingi 138/lita wakati bei ya mafuta ya dizeli zinapungua kwa shilingi 68/lita.

Kwa kuwa hakuna matanki ya kuhifadhia mafuta ya taa katika bandari ya Mtwara, waendeshaji wa vituo vya mafuta kwenye mikoa ya Kusini wanashauriwa kuchukua mafuta ya taa kutoka katika bandari ya Dar es Salaam na hivyo bei za rejareja za mafuta ya taa katika mikoa hiyo itakuwa kulingana na gharama za kupokelea mafuta ya taa kupitia Bandari ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.

Bei za miji, wilaya na mikoa ni kama zinavyooneshwa katika Jedwali Na. 1.
1677654117751.png

1677654158024.png

1677654180836.png

1677654203456.png

1677654219698.png

1677654236539.png
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), inatangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia Jumatano, Tarehe 1 Machi 2023. Pamoja na kutambua bei hizo, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:- (a Kwa Machi 2023, bei za rejareja za mafuta ya petroli,dizeli na mafuta ya taa yaliyopokelewa

Jedwali liko wapi mkuu, nijue huku Ngara-Kagera Tanzania nitanunua Lt kwa shillings ngapi
 
Ewura imetangaza bei kikomo kwa Mafuta ya taa, Diesel na Petrol

Mafuta yaliyopokelewa kupitia Bandari ya DSM Bei imepanda

Source Ayo tv
 
Ewura imetangaza bei kikomo kwa Mafuta ya taa, Diesel na Petrol

Mafuta yaliyopokelewa kupitia Bandari ya DSM Bei imepanda

Source Ayo tv
Unaagiza mzigo wa milion 40, Kodi ni milion 29 (unalipa bandarini) halafu huo mzigo ukiufikisha kwenye sehemu yako ya kazi na ukianza kuuza huo mzigo, unaanza tena kuulipia kodi.
Lazima bei ya mafuta ipande.
 
Unaagiza mzigo wa milion 40, Kodi ni milion 29 (unalipa bandarini) halafu huo mzigo ukiufikisha kwenye sehemu yako ya kazi na ukianza kuuza huo mzigo, unaanza tena kuulipia kodi.
Lazima bei ya mafuta ipande.
Tunakaribia kuwa failed state
 
Bei ya mafuta mpya imetangazwa jana na leo bei imepanda, siku yakishuka wanapewa mda mpaka wamalize stock zao.
Kila Jumatano ya Kwanza ya Mwezi Bei hubadilika, au kubali vile vile.
 
Back
Top Bottom