The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Rais Samia Suluhu Hassann ametoa magari mapya kwa wakuu wa wilaya zote za Mkoa wa Pwani, ili kurahisisha utendaji kazi wa viongozi hao.
Akikabidhi magari hayo kwa niaba ya Rais, mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametoa magari hayo ili kuwawezesha viongozi hao kwenda kwa urahisi kuwatumikia wananchi vijijini na kuwatatulia kero zao.
Wakuu wa wilaya waliokabidhiwa magari yao leo Desemba 04, 2024 ni mkuu wa Wilaya ya Mafia, Halima Mangosongo, mkuu wa wilaya ya Rufiji Luteni Kanali Fredrick Komba na mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Saimon.
Hii nia awamu ya pili kwa wakuu wa wilaya za Mkoa wa Pwani kukabidhiwa magari, ambapo awamu ya kwanza wakuu wa wilaya za.Kisarawe na Bagamoyo walikabidhiwa magari mapya, na mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo yeye atakabidhiwa katika awamu ya tatu.
Akikabidhi magari hayo kwa niaba ya Rais, mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametoa magari hayo ili kuwawezesha viongozi hao kwenda kwa urahisi kuwatumikia wananchi vijijini na kuwatatulia kero zao.
Wakuu wa wilaya waliokabidhiwa magari yao leo Desemba 04, 2024 ni mkuu wa Wilaya ya Mafia, Halima Mangosongo, mkuu wa wilaya ya Rufiji Luteni Kanali Fredrick Komba na mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Saimon.
Hii nia awamu ya pili kwa wakuu wa wilaya za Mkoa wa Pwani kukabidhiwa magari, ambapo awamu ya kwanza wakuu wa wilaya za.Kisarawe na Bagamoyo walikabidhiwa magari mapya, na mkuu wa Wilaya ya Kibiti Kanali Joseph Kolombo yeye atakabidhiwa katika awamu ya tatu.