Nunua tu. Kwa mwezi tenga 100k ya service & maintenance (inaweza kushuka hadi zero au kupanda ata double kwa service kubwa)
Sema nini? Ukiwa na gari matumizi unnecessary yanaongezeka sana man. Mfano:
1. Mademu wanaanza excuses za nipeleke pale twende pale etc. uko utatumia mafuta, muda na gharama zingine. Utakachopata ni utelezi na asante tu.
2. Unaanza uvivu wa kifala sana. Mfano, kwenda tu saloon weekend kunyoa, unaona kama ukienda kwa ngoko utaoshwa maji baridi. Unawasha chuma.
3. Lazima utaanza starehe ambayo ulikua zamani haufanyi. Mfano kwenda bar, beach, kula wadada wazuri, etc. ambayo itaongeza gharama za kindezi.
4. Kuna mahala hautaenda kula tena mfano kwa mama ntilie, huwezi kushuka kununua wali wa buku na magarage huku umepark chuma pembeni.
Cha kujiandaa:
1. Kama kwako kuna space, weekend uwe unafanya mazoezi kwa kuosha gari. Tumia huo muda kukagua matairi, oil level, coolant, fluid washer etc. Kama una watoto anza kufanya nao inakua kama ndio muda wa wewe na mtoto ku-recconect kwa kufanya kazi kwa Pamoja.
2. Baki kama ulivyo. Mtu wa watu. Simple. Pia baadhi ya siku nenda job kwa ngoko. Inasaidia ata siku ukifulia wese au gari bovu watu wajue kaka ni yule yule.
Kwahiyo jiandae kisaikilojia. Ila nikuambie tu, nunua chuma. Ukimiliki hautajuta.
Tukirudi kwenye Terios Kid, ni gari zuri kwa kuanzia. Tena sana, naweza lipa 7.5/10 kwasababu upatikanaji wa spare, reliability, ulaji wa wese, na kubwa zaidi kwasababu ya changamoto za mikoani barabara yenyewe ina ground clearance kubwa.
Oya watamalizia wengine. Karibu kwenye ulimwengu wa wenye mandinga.