Magavana wa CORD kuzuru Amerika kukutana na wawekezaji

Magavana wa CORD kuzuru Amerika kukutana na wawekezaji

Ab-Titchaz

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2008
Posts
14,630
Reaction score
4,253
Magavana wa CORD kuzuru Amerika kukutana na wawekezaji

PM_Raila_Odinga.jpg



Imepakiwa - Wednesday, July 17 2013 at 08:03

Kwa Mukhtasari
:
Magavana wa muungano wa CORD wanatarajiwa kuzuru Amerika na Afrika Kusini mwishoni mwa mwezi huu kukutana na wawekezaji.


MAGAVANA wa muungano wa Cord wanatarajiwa kuzuru Amerika na Afrika Kusini mwishoni mwa mwezi huu kukutana na wawekezaji watarajiwa.

Duru kutoka kwa muungano huo zimedokeza kuwa magavana wa muungano huo wamegawanywa kwa makundi matatu ambayo yatafanya ziara za siku mbili kukutana na Wakenya wanaoishi nje katika harakati za kuchochea maendeleo katika kaunti zao.

Kundi la kwanza litaelekea Texas ilhali la pili litaenda Philadelphia na la mwisho Johannesburg, Afrika Kusini ambapo watafanya mikutano na majadiliano na wawekezaji.

Imeripotiwa kuwa aliyekuwa Waziri Mkuu na kiongozi wa Cord Raila Odinga ndiye aliyeomba na kupata nafasi ya magavana hao kukutana na wawekezaji.

Gavana wa Siaya Cornel Rasanga ambaye ni miongoni ya wale watakaoenda Texas, alithibitisha kwamba watasafiri Amerika na kwamba kundi lake litakuwa na magavana 12.

"Ni kweli tutasafiri Texas na lengo letu kuu ni kukutana na wawekezaji na kuwavutia kwa kaunti zetu," alisema Bw Rasanga katika mahojiano ya simu.

Duru za karibu na mipango hiyo zilifichua kuwa magavana hao watajifadhili wenyewe katika ziara hizo.

Mikutano

"Ziara hiyo ni za kutafuta watu ambao wanaweza kuwekeza kwa lengo la kuwavutia kutumia nafasi kadha ambazo zinapatikana katika kaunti tofauti," duru hiyo iliongeza.

Hatua hii imejiri mwezi moja baada ya magavana kutoka Rift Valley ambao ni wa chama cha United Republican Party (URP) kurejea nchini kutoka kwa ziara ya juma moja Amerika ambapo walihudhuria mikutano kadha na wawekezaji watarajiwa.

Gavana wa Bomet Isaac Ruto aliongoza ujumbe ambao ulijumuisha gavana wa Uasin Gishu Jackson Mandago Cleaophas Lagat wa Nandi na naibu gavana wa Elgeyo-Marakwet Gabriel Lagat.

Magavana wa CORD kuzuru Amerika kukutana na wawekezaji - HABARI ZA SIASA - swahilihub.com
 
So long as hawatafuti za kujaza matumbo yao, this is good for all of us.
 
This is the spirit of devolution which is Kenya's panacea to tribalistic allocations of State resources by the subsequent Kikuyu regimes ever since independence...minus Moi's dictatorship which as a direct offspring of Kenyatta!

Raila asks the USA to invest in counties

5_0.png


Former Prime Minister Raila Odinga has appealed to America's private sector and government to help Kenya's devolved units succeed by investing.

Speaking when officially opening the meeting between Cord governors and investors in Dallas, Texas, yesterday, Raila said America has always stood with Kenya in times of significant transition.

He said that because America has always stood with Kenya, it is "not a surprise" that Kenyan governors are in the US seeking to implement devolution which he described as "the most significant provision of our new constitution'.

Raila asked US businessmen to support Kenya's governors by directing investments to various counties saying it will ensure equitable economic growth and create jobs for the youth.

"Governors are at the frontline of our dreams for an equitable society where development opportunities are evenly spread in the country," he said.

The former PM said governors are the most prominent symbols of the new order being created in Kenya. "The Governors are able to observe what is working and what is not, what needs to be retained and what needs to be fixed. Their success will be our success as a country," he said.

The Cord leader said his party prioritised expenditure on social programmes that it believes will transform the lives of the people, reduce poverty, improve healthcare and create jobs.

He called for investment in infrastructure, healthcare and education.

"A trained and skilled workforce will attract investments and also ensure the youth are able to get jobs," Raila said.

He said a good network of feeder roads across counties, good healthcare and affordable, reliable, clean and efficient energy will change the lives of Kenyans.

Raila asks the USA to invest in counties | The Star
 
Back
Top Bottom