SoC04 Mageuzi katika sekta ya afya kupitia sayansi ya "molecular biology na biotechnology"

SoC04 Mageuzi katika sekta ya afya kupitia sayansi ya "molecular biology na biotechnology"

Tanzania Tuitakayo competition threads

James Godfrey

Member
Joined
Aug 27, 2022
Posts
19
Reaction score
12
Inatisha na kusikitisha jinsi changamoto za sekta ya afya zinavyoathiri watu kote ulimwenguni, Tanzania nchi yangu nayo haijaachwa nyuma na janga hili linalokua kila uchwao, linaloteka vichwa vya habari duniani kote, umekua kama wimbo unaojirudia masikioni mwetu kila siku, bila ubishi wengi wetu ni wahanga kwa namna moja au nyingine wa janga hili linaloikumba sekta hii nyeti kabisa, ambayo kila mtanzania anatamani kuona ikiboreshwa, maana linapokuja swala la afya hapa unagusa uhai wa mtu, kitu ambacho binadamu yeyote yupo tayari kukilinda kwa gharama yoyote ile, ndipo ninapomuelewa yule muhenga aliyesema "afya bora ni mali kuliko dhahabu".

Matatizo yanayoikumba sekta ya afya ni mengi sana natamani hata niandike waraka mrefu sana lakini nimepewa ukurasa mmoja tu hivyo sina budi kuutumia vizuri, napenda kuutumia ukurasa huu kuandika juu ya changamoto moja kati ya nyingi zinazoikumba sekta ya afya, changamoto ya usahihi wa vipimo vya mahabara katika hospitali nchini, makosa katika vipimo yanaweza kuwa na matokeo mabaya, ikiwa ni pamoja na uchunguzi usio sahihi, matibabu yasiyofaa, hata kifo kwa mgojwa.Kwa maono yangu Tanzania tumeachwa nyuma kwa kiasi fulani na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia katika vipimo vipya vya ulimwengu wa kileo. Maendeleo katika ulimwengu wa teknolojia ya upimaji na vipimo vya mahabara yanatupa tumaini jipya na endelevu la kupunguza hatari zinazohusiana na vipimo visivyo sahihi hivyo kuhakikisha usalama na afya ya mgonjwa.

literature-blood_pressure-frankenstein-checkup-check_up-physical-CX916155_low.jpg

Picha ikionyesha changamoto katika upimaji chanzo Google photos

Kabla sijaanza kuelezea vipimo hivi vya ulimwengu wa kileo vinavyotumia sayansi ya "molecular biology na biotechnology" hebu sikia hadithi hii fupi, "alikuepo mama mwenye watoto wawili wadogo aliyekua akiugua ugonjwa asioufahamu , akaenda kituo cha afya akapima, baadae kidogo akaambiwa "mama hatuoni kama una ugonjwa itakua ni mchafuko tu wa damu" hayo ni maneno ya daktari baada yakupata majibu ya vipimo vya mahabara, mama huyo akarudi nyumbani huku akiwa mwenye furaha kwamba yeye si mgonjwa, baada ya mwaka kupita hali ya mama yule ikazidi kuwa mbaya, afya yake ikazidi kuzorota ikabidi apelekwe hospitali ya wilaya alipofika huko akafanyiwa tena vipimo, majibu yakaonyesha mama yule haumwi, Lakini kutokana na hali yake kuwa mbaya ilibidi apewe uhamisho(transfer) kwenda hospitali ya Rufaa ya Kanda yake, alipofika akagundulika mama yule anaumwa saratani ya mapafu tena ipo katika hatua za mwisho kabisa, hivyo daktari akashauri ahamishiwe hospitali ya ocean road jijini dar es salaam, hospitali iliyotengwa kwajili ya wagonjwa wa Saratani nchini, baada ya kufika hospitali hali yake ikazidi kuwa mbaya zaidi, siku nne baadae mama yule akapoteza maisha, ilikuwa ni simanzi kubwa kwa familia ya mama yule.

Hii inaweza kuwa hadithi kama nilivyotangulia kusema hapo juu lakini kiuhalisia hii sio hadithi wala stori ya kufikirika hii ni hali inayowakumba wagonjwa wengi hapa nchini, wengine wanapoteza maisha ili hali kulikua na uwezo wa kuyanusuru.

Kupitia hadithi hiyo hapo juu hapa tunaweza kuona baadhi ya changamoto katika hospitali zetu pale linapokuja swala la upatikanaji wa vipimo, ufanisi wa vipimo hivyo na ubora wa majibu ya vipimo hivyo, kama kalamu yangu inavyofafanua hapo chini

1.UHABA WA VIPIMO KATIKA HOSPITALI ZA NGAZI ZA CHINI
Ndio maana mama yule hakuonekana akiumwa alipofika hospitali ya kijijini kwake hata ya wilayani kwake kutokana na kukosekana kwa vifaa vyenye uwezo wakugundua viashiria vya ugonjwa hata katika hatua za mwanzoni kabsa.

2.VIPIMO KUTOA MAJIBU YASIYO SAHIHI(UFANISI WA VIPIMO)
Mama yule alipimwa kweli Lakini vipimo bado havikuweza kutambua viashiria vya ugonjwa wa saratani, hii inaweza kutokana na vipimo hivyo kutumia teknolojia ya zamani ambayo kwa kiasi fulani inapata tabu katika utambuzi wa baadhi ya magonjwa haswa katika hatua za awali

3.UHABA WA HOSPITALI ZENYE VIPIMO VYA KIBINGWA
Sababu ya mama yule kusafirishwa kilometa nyingi kutoka kijijini kwake hadi Dar es salaam ni sababu ya uhaba wa hospitali za aina ya ocean road hapa Tanzania, mimi siamini kama ni kweli hospitali hii moja inaweza kukidhi mahitaji ya watu Zaid ya milioni 60 kutoka pande zote za Tanzania, maana sisi wote ni wagonjwa watarajiwa.

Kutokana na changamoto kama hizi ndipo nilipoona Kuna haja ya wizara ya afya kukubali na kuanzisha matumizi ya vipimo vinavyotumia teknolojia hii mpya katika hospitali zetu, hata zile za ngazi za chini, maana naona inaweza kutatua changoto zote hapo juu.

Je Vipimo vinavyotumia teknolojia ya molecular biology ni vipi na vinafanyaje kazi? Nazani bado mwandishi sijalijibu swali hili.

Inaweza kuonekana kama ni vifaa vya ajabu lakini amini usiamini vifaa hivi vipo nchini, lakini matumizi yake ni makubwa katika taasisi zinazojihusisha na maswala ya utafiti, kama vile National Institute of medical research(NIMR), Ifakara Health Institute(IHI), Kilimanjaro clinical research institute(KCRI) nakadhalika pia katika hospitali chache hapa nchini.

Naweza kuelezea sayansi inayotumika katika vifaa hivi kama ifwatavyo,
Kwa lugha rahisi kabisa, kama vile ambavyo ukinunua bidhaa dukani unakuta kuna lebo imebandikwa ambapo ukifanikiwa kuiisoma utafahamu taarifa zote za bidhaa hiyo kuanzia tarehe iliyotengenezwa, tarehe ya mwisho wa matumizi, vilivyotumika kuitengenezea hata faida za bidhaa hiyo, vivyo hivyo mwili wa binadamu una chembe chembe ndogo sana kama vile DNA, RNA, proteins n.k ambapo chembe hizi ndogo zimebeba taarifa zote zilizopo kwenye mwili wa binadamu(Hata taarifa zote za kiafya) hivyo tukipata njia ya kuweza kusoma chembe hizo tunaweza kujua taarifa zote za mwili wa binadamu(kujua afya ya mtu), ndipo wanasayansi wakabuni vifaa ambavyo vinaweza kusoma taarifa hizi, ndipo tukapata vifaa vinavyotumia teknolojia ya molecular biology.Hivyo vifaa hivi vinapotumiwa katika mahabara za hospitali hufanya kazi ya kuchunguza chembe hizo ndogo zilizozikusanywa kutoka katika sampuli kama vile mate, damu, kinyesi, mkojo n.k kuona kama kuna dalili au viashiria vyovyote vya ugonjwa au viashiria vya hatari yoyote ya kiafya kwa mgonjwa.

20240504_151903.jpg

Picha ikionyesha baadhi ya vifaa vinavyotumia teknolojia mpya, chanzo Google photos

FAIDA YA VIFAA HIVI KATIKA KUPIMA NA KUTOA MAJIBU SAHIHI

1. USAHIHI: Vifaa hivi vina usahihi mkubwa katika kupima sampuli za wagonjwa, vinapunguza makosa ya kibinadamu na kuongeza usalama wa mgonjwa.

2. UFANISI: Vifaa hivi vina uwezo wa kugundua ugonjwa hata katika hatua za awali, kuwezesha matibabu mapema na kupunguza vifo vinavyoepukika.

3.AJIRA: Matumizi ya vifaa hivi yataongeza fursa za ajira kwa vijana wa kitanzania, kwa sababu katika vyuo vyetu hapa nchini vijana wetu wanafundishwa kuhusu teknolojia hii mpya, lakini kutokana na kwamba teknolojia hii imebakia katika taasisi za utafiti ambazo ni chache hapa nchini ukilinganisha na idadi ya vijana wanaomaliza vyuo kila mwaka hivyo vijana wengi wanabaki mtaani bila ajira, lakini teknolojia hii ikikubalika na kutumika katika hospitali za ngazi zote hapa nchini fursa za ajira kwa vijana hawa zitaongezeka hivyo kukabiliana na tatizo la ajira hapa nchini.
 
Upvote 11
Andiko zuri kijana
Ila linawahitaji watu waliopo kwenye eneo Hilo la afya
Kwa mtu anaehudumia wagonjwa, atakuelewa saana
Serikali inajenga majengo mengi ya vituo vya afya na hospital ila linapokuja suala la vifaa tiba na wataalamu bado ni kasheshe, si ajabu hospital ya wilaya kukosa x ray machine , ultrasound au chemistry analyser na Wala si ajabu hospital ya kukosa dialysis unit , histopathology unit au CT scan, vinaonekana vipimo vya anasa
Kazi ya kupima mikojo na stool pamoja na malaria
 
Andiko zuri kijana
Ila linawahitaji watu waliopo kwenye eneo Hilo la afya
Kwa mtu anaehudumia wagonjwa, atakuelewa saana
Serikali inajenga majengo mengi ya vituo vya afya na hospital ila linapokuja suala la vifaa tiba na wataalamu bado ni kasheshe, si ajabu hospital ya wilaya kukosa x ray machine , ultrasound au chemistry analyser na Wala si ajabu hospital ya kukosa dialysis unit , histopathology unit au CT scan, vinaonekana vipimo vya anasa
Kazi ya kupima mikojo na stool pamoja na malaria
Uhakika kaka, serikali inaona watu tunaendelea Kuishi na vipimo hivyo vya zamani inahisi kama vile hakuna haja ya mabadiliko
 
Uhakika kaka, serikali inaona watu tunaendelea Kuishi na vipimo hivyo vya zamani inahisi kama vile hakuna haja ya mabadiliko
Ila naamini hapa jamiiforum pia limefika kwenye mikono salama, ni rahisi kuwafikia wahusika kuliko ningepost kama private post
 
ambayo kila mtanzania anatamani kuona ikiboreshwa, maana linapokuja swala la afya hapa unagusa uhai wa mtu, kitu ambacho binadamu yeyote yupo tayari kukilinda kwa gharama yoyote ile, ndipo ninapomuelewa yule muhenga aliyesema "
Mtanzania! Itabidi tumuulize Profesa Janabi uzoefu wake katika kushauri afya kwa watz. maana wabongo, kuna wanaosema waziwazi kabisa "Usiniambie hayo makanuni sijui kula hiki, acha kile....... kuna faida gani kufa na ini/figo/moyo/pafu zima?

akaambiwa "mama hatuoni kama una ugonjwa itakua ni mchafuko tu wa damu" hayo ni maneno ya daktari baada yakupata majibu ya vipimo
Ni masikitiko wanataaluma wakianza nao kutumia maelezo ya kimtaamtaa badala kueleza vizuri tatizo naye anatembelea mule mule, mchafuko wa damu, UTI sugu jamani jamanii.

Rai kwa madaktari kutumia kesi wanazokutana nazo kama sehemu ya kuelimisha jamii usahihi wa matatizo yao. Ndio maana ya daktari, to doctor is to teach too.
Ndio maana mama yule hakuonekana akiumwa alipofika hospitali ya kijijini kwake hata ya wilayani kwake kutokana na kukosekana kwa vifaa vyenye uwezo wakugundua viashiria vya ugonjwa hata katika hatua za mwanzoni kabsa.
Inatugharimu sana, kukosa nyenzo muhimu
2. UFANISI: Vifaa hivi vina uwezo wa kugundua ugonjwa hata katika hatua za awali, kuwezesha matibabu mapema na kupunguza vifo vinavyoepukika.
Tunachelewa sana, yaani utashangaa mataifa mengine wamefikia hatua ya kusoma vinasaba vyotevyote (genomics) lakini kwetu hata tu kupima pale inapobidi bado tunasuasua.

Japo kwa upande mwingine umesema hivyo vipimo vipo katika taasisi za utafiti na hospitali za kibingwa. Labda ndio ipo kiuchumi zaidi kwamba badala ya kisambaza vipimo vya gharama nchi nzima, vimewekwa katika ngazi za juu za rufaa. Maana kwenye tiba kuna suala la kwamba hakuna faida ya kupima (au screening) ya ugonjwa usoweza kuutibu. Sasa tukuulize mleta mada. Je inakuja kweli kuwa na vipimo vya kansa kwenye kituo cha afya kisichotibu saratani?
 
Tunachelewa sana, yaani utashangaa mataifa mengine wamefikia hatua ya kusoma vinasaba vyotevyote (genomics) lakini kwetu hata tu kupima pale inapobidi bado tunasuasua
Ni kweli kabisa, sasa hivi ulimwengu unaenda katika kumtibu mtu kutokana na vinasaba vyake(personalized medicine/precision medicine) ila kwetu hapa bado molecular biology and biotechnology ni mjadala inasikitisha kwa upande mwingine, natamani kuona juhudi za THGO(Tanzania Human genetics organization) zikifika mbali siku moja
 
Mtanzania! Itabidi tumuulize Profesa Janabi uzoefu wake katika kushauri afya kwa watz. maana wabongo, kuna wanaosema waziwazi kabisa "Usiniambie hayo makanuni sijui kula hiki, acha kile....... kuna faida gani kufa na ini/figo/moyo/pafu zima?


Ni masikitiko wanataaluma wakianza nao kutumia maelezo ya kimtaamtaa badala kueleza vizuri tatizo naye anatembelea mule mule, mchafuko wa damu, UTI sugu jamani jamanii.

Rai kwa madaktari kutumia kesi wanazokutana nazo kama sehemu ya kuelimisha jamii usahihi wa matatizo yao. Ndio maana ya daktari, to doctor is to teach too.

Inatugharimu sana, kukosa nyenzo muhimu

Tunachelewa sana, yaani utashangaa mataifa mengine wamefikia hatua ya kusoma vinasaba vyotevyote (genomics) lakini kwetu hata tu kupima pale inapobidi bado tunasuasua.

Japo kwa upande mwingine umesema hivyo vipimo vipo katika taasisi za utafiti na hospitali za kibingwa. Labda ndio ipo kiuchumi zaidi kwamba badala ya kisambaza vipimo vya gharama nchi nzima, vimewekwa katika ngazi za juu za rufaa. Maana kwenye tiba kuna suala la kwamba hakuna faida ya kupima (au screening) ya ugonjwa usoweza kuutibu. Sasa tukuulize mleta mada. Je inakuja kweli kuwa na vipimo vya kansa kwenye kituo cha afya kisichotibu saratani?
Hapo mwishoni nadhani ametumia kansa kama mfano lakini kuna huduma nyingi za msingi ambazo hazipatikani hospitali zetu za mikoa
Dialysis
CT scan
Histopathology
Hebu fikiria mtu aliepata ajali mbaya ya kuumia kichwa yupo huukooo Karema ,katavi ,mtu huyu anahitaji matibabu ya haraka ikiwemo CT scan lkn hawezi kupata mpaka apelekwe hospital ya Kanda mbeya, umbali wa kutoka Karema mpaka mbeya, jumlisha milolongo tuliyojiwekea kwenye rufaa, obvious atakufa kabla ya kupata hiyo huduma
Ama mgonjwa aliepata malaria kali ambayo imepeleka figo kufeli ghafla (AKI) akiwa hukohuko mwese , itabidi apelekwe mbeya wakati huduma inaweza kutolewa hospital ya mkoa
Bado tuna changamoto sana kwenye huduma ya afya
 
Mtanzania! Itabidi tumuulize Profesa Janabi uzoefu wake katika kushauri afya kwa watz. maana wabongo, kuna wanaosema waziwazi kabisa "Usiniambie hayo makanuni sijui kula hiki, acha kile....... kuna faida gani kufa na ini/figo/moyo/pafu zima?


Ni masikitiko wanataaluma wakianza nao kutumia maelezo ya kimtaamtaa badala kueleza vizuri tatizo naye anatembelea mule mule, mchafuko wa damu, UTI sugu jamani jamanii.

Rai kwa madaktari kutumia kesi wanazokutana nazo kama sehemu ya kuelimisha jamii usahihi wa matatizo yao. Ndio maana ya daktari, to doctor is to teach too.

Inatugharimu sana, kukosa nyenzo muhimu

Tunachelewa sana, yaani utashangaa mataifa mengine wamefikia hatua ya kusoma vinasaba vyotevyote (genomics) lakini kwetu hata tu kupima pale inapobidi bado tunasuasua.

Japo kwa upande mwingine umesema hivyo vipimo vipo katika taasisi za utafiti na hospitali za kibingwa. Labda ndio ipo kiuchumi zaidi kwamba badala ya kisambaza vipimo vya gharama nchi nzima, vimewekwa katika ngazi za juu za rufaa. Maana kwenye tiba kuna suala la kwamba hakuna faida ya kupima (au screening) ya ugonjwa usoweza kuutibu. Sasa tukuulize mleta mada. Je inakuja kweli kuwa na vipimo vya kansa kwenye kituo cha afya kisichotibu saratani?
Unachosema ni kweli, mimi kwa maoni yangu sio kweli kwamba kila kituo lazima kiwe na vifaa hivyo vya kisasa, ila nilikua naona kuna haja yakusogeza huduma hizi kwa raia angalau hata katika ngazi ya wilaya mtu awe anaweza kupata huduma ambayo saivi inabidi aende hospitali ya rufaa, naamini kama vile tulivoweza katika kujenga shule katika kila kata, hata hili la afya linawezekana
 
Unachosema ni kweli, mimi kwa maoni yangu sio kweli kwamba kila kituo lazima kiwe na vifaa hivyo vya kisasa, ila nilikua naona kuna haja yakusogeza huduma hizi kwa raia angalau hata katika ngazi ya wilaya mtu awe anaweza kupata huduma ambayo saivi inabidi aende hospitali ya rufaa, naamini kama vile tulivoweza katika kujenga shule katika kila kata, hata hili la afya linawezekana
Pia katika andiko hili nilijaribu kuongelea sana vifaa vinavyotumia teknolojia mpya hasa ya molecular biology, naamini inabidi tutoke kwenye hizi diagnosis za kila siku, tuhamie kweny ulimwengu wa molecular biology, tuextract DNA tuka analysis tupata majibu yakuaminika.
 
Hapo mwishoni nadhani ametumia kansa kama mfano lakini kuna huduma nyingi za msingi ambazo hazipatikani hospitali zetu za mikoa
Dialysis
CT scan
Histopathology
Hebu fikiria mtu aliepata ajali mbaya ya kuumia kichwa yupo huukooo Karema ,katavi ,mtu huyu anahitaji matibabu ya haraka ikiwemo CT scan lkn hawezi kupata mpaka apelekwe hospital ya Kanda mbeya, umbali wa kutoka Karema mpaka mbeya, jumlisha milolongo tuliyojiwekea kwenye rufaa, obvious atakufa kabla ya kupata hiyo huduma
Ama mgonjwa aliepata malaria kali ambayo imepeleka figo kufeli ghafla (AKI) akiwa hukohuko mwese , itabidi apelekwe mbeya wakati huduma inaweza kutolewa hospital ya mkoa
Bado tuna changamoto sana kwenye huduma ya afya
Ni kweli, tunakubaliana kuna haja ya kuona huduma za msingi zipate miundombinu wezeshi kutoa huduma zinazopaswa kutolewa katika maeneo yao.

Hilo ni sambamba na wataalamu na vipimo kama ulivyoorodhesha chief.
 
Back
Top Bottom