Magodoro 30 (Milioni 2.5) Yagawiwa kwa Wanawake wa UWT Wilaya ya Momba

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE CONDESTER SICHALWE AKABIDHI MAGODORO 30 (MILIONI 2.5) KWA WANAWAKE UWT WILAYA YA MOMBA

Mbunge wa Jimbo la Momba Mkoa wa Songwe Mhe. Condester Mundy Michael Sichalwe tarehe 26 Julai, 2023 amekutana na Wanawake wa UWT Wilaya ya Momba na kuwakabidhi Magodoro 30 yenye thamani ya Shilingi Milioni 2,505,000

Mhe.Condester Sichalwe aliambatana na Maafisa Kilimo wa Wilaya ya Momba kwaajili ya kutoa elimu kuhusu mambo yote ya Kilimo kwani wananchi wanahitaji elimu ya Kilimo ili waweze kuwa na Kilimo chenye tija

Mhe. Condester Sichalwe amewataka Viongozi hao kuwa Mabalozi wazuri kwa kuitisha mikutano ya hadhara na kuwapa taarifa mbalimbali za uzalishaji Kilimo waliyoipata na amewaomba Viongozi wa UWT kuwasiliana na Maafisa Kilimo Wilaya ya Momba kwani wapo tayari muda wowote kwenda kuwasikiliza na kuwapa Elimu ya Kilimo chenye tija.

Aidha, Mhe. Condester Sichalwe alipata chakula cha pamoja cha mchana na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Momba ambao walimshukuru sana Mbunge Condester kwa kuwapa semina ya Kilimo na kuahidi kufanyia kazi elimu waliyoipata

Mhe. Condester Sichalwe amewashukuru UWT Momba kwa ushirikiano wanaompa na kuwataka wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuunga mkono juhudi za Serikali na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…