Elections 2010 Magufuli CHATO na BULANDES Karagwe Chali!!!

Status
Not open for further replies.
kuhusu MAgufuli siyo kweli... si alipita bila kupingwa?????
 
sitakubali kumpoteza magufuli...cant be true huyu jamaa ni muwajibikaji.
 
Jamani acheni kuwapa watu ugonjwa wa moyo. Mbona bado hayajatangazwa?
 
....kama ni kweli...........naona CCM watakua wamechakachua vibaya .....................wakachakachua mpaka kura za Magufuli........duhhh!
 
kizuri hakijitembezi, Pombe yuko juu, ni vigumu kumtosa!
 
Acheni kejeli na mizaha. hakuna anayeweza kunywa ile pombe hadi yeye mwenyewe aipoze. Leteni data mpya.

Pombe ni pombe tu. Under the proper circumstances it evaporates. Huyu jamaa mjanja mjanja tu, mkandamizaji na mzulumaji mkubwa. Ni yeye ameanzisha utamaduni wa bomoa bomoa bila fidia na ndiye aliyefanyaa yale mazingaombwe ya kugeuza nyumba za serkali zikawa "nyumba zao!" Na wasomi wengine wakaona anavyofanya hivyo ni vizuri hadi wakamtunukia ile degree ya wakosefu (Honorary Degree)! Ni wazi kuwa Wananchi wa jimbo lake wanamfahamu vizuri zaidi na huenda ndiyo maana wameimwaga pombe chini, licha ya kujenga kanisa nyumbani kwao kwa hela yake mwenyewe - au labda kwa sababu hiyo!

Habari zaidi za Pombe hizi hapa:

http://www.podfeed.net/episode/Magufuli+Shujaa+au+Mjanja+kama+wengine/451425
 
Nimegundua kumbe humu ndani mnaongopeana. Magufuli is cruising in Chato, but JK is tight locked by Dk. Slaa. Hii post imenifanya nisiamini mengi sana niyasomayo humu. Ngoja nisubiri matokeo ya Tume tu
 
embu acheni kuleta taarifa za uongo hapa JF hatutaki tetesi wakati huu wa matokeo. Magufuri hawezi kubwagwa nyinyi
 
kwa kweli mambo ya chato si kweli,niko bukoba hapa,magufuli hajashindwa bado,wala karagwe matokeo bado ingawa mchuano ni mkubwa sana huko karagwe,kwa magufuli mchuano ni mkali lkn kuna dalili za magufuli kushinda
 
Umenifurahisha kwa tafsiri hiyo!
 
No Research No right to Speak!! Sasa tukiwa tunapeana habari za Nasikia ...... Nasikia !!! Hii Forum itaonekana ya Wababaishaji bure!!
Pata uhakika, Pata Data tumbukiza humu kuwajuva wengine.
 
Kwa Blandes ameingia mpambanaji JOVIN DEUSIDEDIT yule mwandishi mkongwe wa makala na mfanyakazi pale extelecoms
 
Kama huna data mkuu usituletee udake kutufanya tushangilie in vain!
 
muache utani mbaya magufuli pombe anaendeleza libeneke la kugida pombe
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…