Magufuli usiwafanyie stars kama mtibwa sugar walivyofanyiwa na RC wako

She loves Me

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2017
Posts
809
Reaction score
939
Habari wababa na wamama
Kwanza kabisa nimshukuru sana Rais Magufuli kwa ahadi ya kuwapa viwanja mashujaa wetu wa Taifa Stars baada ya ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Uganda.

[emoji17]NAWAKUMBUSHA;[emoji17]

Kama tujuavyo MTIBWA SUGAR ndo mabingwa wa ligi ya shirikisho maarufu kama F.A. msimu uliopita(2017/2018)
Kwenye shamrashamra za kusherehekea ushindi huo RC wa Morogoro aliwaahidi kuwapa viwanja ndani ya Mkoa wake wachezaji wote wa Mtibwa kama zawadi na motisha lakin mpaka sasa kimyaaa.
Vijana wa watu walijiandaa vizuri sana kuanza ujenzi lakin hamna cha viwanja mpaka sasa. Wapigwa na butwaa kuona mwaka sasa unakata kimya.

Na hii imekuwa kama tabia kwa viongozi wetu ya kuwatoa watu mate na kuwaacha solemba.

CHONDE RAISI HAKIKISHA UNATIMIZA AHADI YAKO, ILI TUWEZE KUKUTOFAUTISHA NA RC WAKO TAPELI.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…