Pre GE2025 Mahakama Kuu yatupilia mbali shauri la Luhaga Mpina dhidi ya Uagizaji wa Sukari

Pre GE2025 Mahakama Kuu yatupilia mbali shauri la Luhaga Mpina dhidi ya Uagizaji wa Sukari

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam leo tarehe 14, Februari 2025 imetupilia mbali shauri la kikatiba lililofunguliwa na Mbunge wa Jimbo la Kisesa Luhaga Mpina juu ya kupinga uaagizwaji wa sukari nje ya nchi.

Uamuzi wa shauri hilo umesomwa na Jaji Salma Maghimbi akieleza kulifuta huku akisistiza kuwa mahakama haijaona athari kwa wakulima wa ndani bali ni uoga tu. Hata hivyo ameeleza kuwa wakulima hao wana nafasi ya kukata rufaa kama hawajaridhika na hukumu hiyo.

Soma Pia: Luhaga Mpina: Usambazaji wa sukari haukuwa ukifanywa na mfanyabiashara mmoja wa Mwanza pekee, Waziri Bashe alidanganya

Kwa upande wake mwakilishi wa wakulima wa miwa kutoka Kilombero, George Mzigowande amesema hawajaridhishwa na hukumu hiyo hivyo watakata rufaa katika Mahakama ya Rufani.

 

Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam leo tarehe 14, Februari 2025 imetupilia mbali shauri la kikatiba lililofunguliwa na Mbunge wa Jimbo la Kisesa Luhaga Mpina juu ya kupinga uaagizwaji wa sukari nje ya nchi.​

Uamuzi wa shauri hilo umesomwa na Jaji Salma Maghimbi akieleza kulifuta huku akisistiza kuwa mahakama haijaona athari kwa wakulima wa ndani bali ni uoga tu. Hata hivyo ameeleza kuwa wakulima hao wana nafasi ya kukata rufaa kama hawajaridhika na hukumu hiyo.​

Kwa upande wake mwakilishi wa wakulima wa miwa kutoka Kilombero, George Mzigowande amesema hawajaridhishwa na hukumu hiyo hivyo watakata rufaa katika Mahakama ya Rufani.​

Ikumbukwe Mpina, alifungua kesi ya kikatiba dhidi ya Waziri wa Kilimo, Waziri wa Fedha, Bodi ya Sukari, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mwanasheria Mkuu wa Serikali, na kampuni binafsi, akipinga uhalali wa utoaji wa vibali vya kuagiza sukari kutoka nje ya nchi. Mpina anadai kuwa vibali hivyo vilitolewa kinyume na sheria na taratibu zilizopo.​

Katika hatua za awali za kesi hiyo, Mahakama Kuu ilitupilia mbali ombi la Mpina la kutaka kuwasilisha majibu ya nyongeza baada ya kupokea majibu kutoka kwa upande wa walalamikiwa. Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Arnold Kirekiano mnamo Septemba 18, 2024​


Hata hivyo hadi sasa Mahakama Kuu ya Tanzania imeshindwa kutoa nakala ya Hukumu ya Kesi ya Wakulima wa Miwa wa Kilombero kupitia mtandao wa Mahakama uitwao Tanzill jambo linaloibua maswali mengi juu ya hukumu hiyo.


View: https://youtu.be/8aYRuSvQAhg?si=Mck2ZmZmtabkeKvO
 
Swali nje ya topic kidogo.
Tunaambiwa tuna mihimili mitatu inayojitegemea Tanzania
1. Mahakama
2. Bunge
3. Serkali tendaji( Excutive)
Swali langu ni hili nani anafanya mwingiene kuwepo kwake na mipaka yake?
Hii sio janja janja kwi mbona mihimili mingine inaupigia mapambio mhimili mmoja zaidi?
 
Swali nje ya topic kidogo.
Tunaambiwa tuna mihimili mitatu inayojitegemea Tanzania
1. Mahakama
2. Bunge
3. Serkali tendaji( Excutive)
Swali langu ni hili nani anafanya mwingiene kuwepo kwake na mipaka yake?
Hii sio janja janja kwi mbona mihimili mingine inaupigia mapambio mhimili mmoja zaidi?
Kulikuwa na wakati Mahakama judiciary ilikuwa judiciary kweli, na Bunge Parliament ilikuwa kweli Parliament wakati wa JK!!! 😅😅

Sasa Mahakama
 
Nyie ndio mnakesha humu kutukana JK
Natukana vipi wakati namsifia kwamba was smart 🤓

Au wewe hujui mambo mazuri ya nchi hii utawala wa sheria ulionekana wakati wa kikwete??
Au wewe ni mgeni hapa Tz??
 
Back
Top Bottom