Mahitaji muhimu ya mwanadamu yameongezeka sana, sasa sio chakula, malazi na mavazi tu, ila elimu, gari, internet na biashara/ kazi, haki na usalama

Mahitaji muhimu ya mwanadamu yameongezeka sana, sasa sio chakula, malazi na mavazi tu, ila elimu, gari, internet na biashara/ kazi, haki na usalama

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Zama zile za kati, mahitaji ya mwanadamu ya msingi yalikuwa matatu tu. Lakini sasa mambo yamebadilika kabisa.

Leo tunahitaji internet kama hutaji muhimu la mawasiliano, bila internet mawasiliano yetu yako kwenye mashaka makubwa sana.

Maisha ya leo bila kuwa na biashara au KAZI, wewe ni mfu na utadharaulika na kila MTU. KAZI sio lazima uwe umeajiriwa, chochote unachokifanya na kukuingizia kipato ni KAZI.

Leo bila kusafiri hali ni tete. Unawezaje kutoka Gongo la Mboto hadi kazini kwako Posta?

Kwenye dunia yetu ya sasa Usalama ni Jambo la msingi sana. Tunawezaje kufanya shughuli zetu kwenye mazingira ambayo Panya Road wanapita mchana kweupe wakipora Mali, kupiga watu, kubaka na kujeruhi?

Haki pia ni hitaji muhimu la mwanadamu licha ya kwamba halipatikani kirahisi.

Ila tukae tukijua kwamba amani ni tunda la haki. Bila haki hakuna amani.
 
Mahitaji muhimu ya mwanadamu yanazidi kuongezeka aisee
 
Zama zile za kati, mahitaji ya mwanadamu ya msingi yalikuwa matatu tu. Lakini sasa mambo yamebadilika kabisa.

Leo tunahitaji internet kama hutaji muhimu la mawasiliano, bila internet mawasiliano yetu yako kwenye mashaka makubwa sana.

Maisha ya leo bila kuwa na biashara au KAZI, wewe ni mfu na utadharaulika na kila MTU. KAZI sio lazima uwe umeajiriwa, chochote unachokifanya na kukuingizia kipato ni KAZI.

Leo bila kusafiri hali ni tete. Unawezaje kutoka Gongo la Mboto hadi kazini kwako Posta?

Kwenye dunia yetu ya sasa Usalama ni Jambo la msingi sana. Tunawezaje kufanya shughuli zetu kwenye mazingira ambayo Panya Road wanapita mchana kweupe wakipora Mali, kupiga watu, kubaka na kujeruhi?

Haki pia ni hitaji muhimu la mwanadamu licha ya kwamba halipatikani kirahisi.

Ila tukae tukijua kwamba amani ni tunda la haki. Bila haki hakuna amani.
India elimu

We don’t it… tunahiteji maarifa tu
 
Back
Top Bottom