Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 986
- 208
MDADISI: Ehee, na wewe tueleze unahusikaje na ulitumwa na nani!
MSHUKIWA:Sihusiki sana mh, nilikuwa natekeleza matakwa ya mkuu wangu.
MDADISI: Ni nani huyo mkubwa wako? Mtaje ili wewe uwe huru.
MSHUKIWA: Kamanda wangu mh.( huku akimtaja)
MDADISI: Heh! haiwezekani.( Kimoyoyomoyo, nitahoji vipi mkubwa wangu!!!)
Hata hivyo anaamua kumhoji baada ya kupata go ahead!
MDADISI: Mh Kamanda, wewe unahusikaje na hili?
KAMANDA: Niliagizawa na mkuu wangu nimsaidie ili aweze kupanda cheo.
MDADISI: Kumsaidia kwa namna gani?
KAMANDA: Ili apande cheo!
MDADISI: Unaweza kumtaja huyo mkuu wako?
KAMANDA: Ki itifaki sitoweza kumtaja!
MDADISI: Una maanisha ni ( anamtaja)
KAMANDA: Haswaa, tena yule anakuja! ( huku akimnyoshea kidole)
MDADISI: Ok, ngoja ni mwite, Karibu mkubwa!
MKUBWA: Aksante.
MDADISI: Mbona uko huku?
MKUBWA: Nafuatilia mauaji ya Albino.
MDADISI: Tuambie mkuu, wewe unahusikaje kwenye hili?
MKUBWA: Mimi siyo msemaji wa Wizara, labda waziri mwenye dhamana, tena atakuwa hapa muda si mrefu.( mara waziri anaingia).
MDADISI: Mh. Waziri, karibu sana. Nini maoni yako kufuatia upigaji wa kura za kuwafichua wanaojihusisha na mauaji ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi?
WAZIRI: Eeh; nafikiri ni mapema mno kulizungmzia hili. Ninachoweza kusema ni kuwa serikali ina mkono mrefu, itawakamata tu!
MDADISI: Mbona uko huku, kunani?
WAZIRI: Natafuta njia ya kushinda katika uchaguzi ujao.
MDADISI: Unatafuta kutoka kwa nani!
WAZIRI: Wewe vipi! Si kwa hoo ndgu zetu waganga wa kienyeji!
MDADISI: Watakusaidiaje?
WAZIRI: Ndiyo maana tumeitisha kura pamoja na mambo mengine kutaka kujua pia ni akina nani wanataka kuchukua majimbo yetu na ni kina nani wanawafadhili!
MDADISI: Ooooh! kumbeeee!
MSHUKIWA:Sihusiki sana mh, nilikuwa natekeleza matakwa ya mkuu wangu.
MDADISI: Ni nani huyo mkubwa wako? Mtaje ili wewe uwe huru.
MSHUKIWA: Kamanda wangu mh.( huku akimtaja)
MDADISI: Heh! haiwezekani.( Kimoyoyomoyo, nitahoji vipi mkubwa wangu!!!)
Hata hivyo anaamua kumhoji baada ya kupata go ahead!
MDADISI: Mh Kamanda, wewe unahusikaje na hili?
KAMANDA: Niliagizawa na mkuu wangu nimsaidie ili aweze kupanda cheo.
MDADISI: Kumsaidia kwa namna gani?
KAMANDA: Ili apande cheo!
MDADISI: Unaweza kumtaja huyo mkuu wako?
KAMANDA: Ki itifaki sitoweza kumtaja!
MDADISI: Una maanisha ni ( anamtaja)
KAMANDA: Haswaa, tena yule anakuja! ( huku akimnyoshea kidole)
MDADISI: Ok, ngoja ni mwite, Karibu mkubwa!
MKUBWA: Aksante.
MDADISI: Mbona uko huku?
MKUBWA: Nafuatilia mauaji ya Albino.
MDADISI: Tuambie mkuu, wewe unahusikaje kwenye hili?
MKUBWA: Mimi siyo msemaji wa Wizara, labda waziri mwenye dhamana, tena atakuwa hapa muda si mrefu.( mara waziri anaingia).
MDADISI: Mh. Waziri, karibu sana. Nini maoni yako kufuatia upigaji wa kura za kuwafichua wanaojihusisha na mauaji ya ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi?
WAZIRI: Eeh; nafikiri ni mapema mno kulizungmzia hili. Ninachoweza kusema ni kuwa serikali ina mkono mrefu, itawakamata tu!
MDADISI: Mbona uko huku, kunani?
WAZIRI: Natafuta njia ya kushinda katika uchaguzi ujao.
MDADISI: Unatafuta kutoka kwa nani!
WAZIRI: Wewe vipi! Si kwa hoo ndgu zetu waganga wa kienyeji!
MDADISI: Watakusaidiaje?
WAZIRI: Ndiyo maana tumeitisha kura pamoja na mambo mengine kutaka kujua pia ni akina nani wanataka kuchukua majimbo yetu na ni kina nani wanawafadhili!
MDADISI: Ooooh! kumbeeee!