Nimesoma baadhi ya comments za wanaume, nimeishia kuumia. Majority ya wanaume hawajali hisia za watoto wao, wao wanachojali ni kutoa pesa tu. Eti mtu kakomaa "nimempa millioni 7, nimemnunulia Rav 4", so kama unampa hela ndo umkane mwanao? That's too from a person aliyekanwa na baba ake, angalau yeye alipewa hata na jina la mzee Naseeb, naona Hamissa aliambiwa atumie jina la baba ake as if yeye ndo alimtia mimba. Mtu kumkubali mtoto wake hata kama ana uwezo wa kumpa sh 200 means a lot to the kid. Hivi huyu mtoto angekuaje kwneye mazingira ya kumuona baba anaspend some quality times na watoto wake wengine afu wewe mwenzangu hata kupiga picha na baba ni uchochezi maana picha ikivuja ni tatizo, watu wanaelewa kweli what it means to be a father? Huyu mtoto angekua kwenye saikolojia ya hali gani? Tena bora baba anayekukataa mazima, kuliko ambaye anakufanya siri sijui anakuonea aibu kisa nini sijui. Afu baba zima na akili zake linakuja eti "Hamissa kajikosesha mengi", pumbaff linawaza material things tu. Hivi kuna mmama anayebeba mimba miezi 9 akashindwa kumlea mwanae hata kama ni kwa kunywa uji?
Kama diamond alishakiri na kuomba msamaha kwa familia yake (zari na kwa ndugu zake), ni nini kilimfanya aendelee kumficha mtoto? Trust me hata dunia nzima ikugeuke, as long as familia yako imekuelewa na inakussuport, kila kitu kitakuwa sawa tu eventually.
Alikuwa anawahofia wabongo? Hao wanaume wa kumnyooshea diamond vidole wako wapi, hawa ambao kucheat ni nature yao na ndo ufahari wao? Na sisi wanawake ambao tunaamini all men cheat? Seriously alikuwa anajisikiaje mtoto wake anavyotukanwa eti hana baba? Mbona angekubali tu mapema, siku mbili tu tungeshasahau. Albert msando yalimkuta kwa giggy lakini he owned up his mistake na tushasahau na ndoa yake imesimama kama kawaida. Sidhani kama yangefikia yalipofikia leo kama Dai angekubali mapema tena angeweka mazingira mazuri na angekuwa free kukata mazoea yasiyo na msingi na Hamissa, in case of chochote, anawaomba tu familia isimamie
Kwa hilo Hamissa la kutoa hiyo misiri hadi dai kamuaccept mtoto publicly nampongeza kabisa, hakuna mtoto wa public na private. Ila liwe somo kwake na kwa mabinti wote tunaoembrace kuwa the other woman na kufanywa kisirisiri, maana mwishowe na mtoto atakuwa wa sirini, dhambi kubwa sana. Angekuwa mwanamke mwingine hapa ungemsikia "Aah nimenunuliwa gari na nyumba, mwanangu anasoma vizuri hata asipomuweka wazo mtoto ni sawa tu" pambaff yani watu wanafanya watoto vitega uchumi afu mtoto anaishia kupata a lifetime psychological torture. Kuhudumia hata loan board imehudumia watu wengi tu, ila sio baba ake mtu. Hili limeshapita mbona, amlee tu mwanae kwa uhuru