Mahusiano ya familia yangu yananiharibu kisaikolojia

Mahusiano ya familia yangu yananiharibu kisaikolojia

Status
Not open for further replies.

Kwamacho

Member
Joined
Apr 11, 2020
Posts
80
Reaction score
126
Ndugu zangu, napenda kushiriki hali yangu na ninaomba ushauri wenu.

Nimekuwa nikilelewa na bibi yangu tangu nikiwa na umri wa miaka 2 na sasa nina miaka 24 na wazazi wangu wote wapo hai mpaka sasa. Sijawahi kuonana na baba yangu kabisa ingawaje kwa sasa tunawasiliana katika simu, Mama yangu nafahamu alipo ila yupo busy sana na maisha yake na utafutaji labda kwasababu anajua ninalelewa na bibi ambaye ni mama yake hivyo sipati msaada wowote zaidi ya ninaopata kutoka kwa bibi yangu.

Bibi ndie ananisimamia kwa kila kitu na amekua ndio nguzo yangu kuu.

Nimesomeshwa shule ya msingi na bibi yangu hadi nilipohitimu na kuendelea na masomo ya sekondari lakini kuanzia hapo bibi yangu alimpatia mtu mwingine majukumu ya kunisimamia wakati wa masomo ya sekondari na rasmi nilianza kusimamiwa na kaka wa mama yangu ambaye ni mjomba.

Nimepitia mengi sana katika maisha nilipokua sekondari kwasababu nilikua kama mkimbizi au yatima na nilipopitia magumu na kukosa nuru niliulizwa wazazi wangu wako wapi wanisaidie.

Nilipiga moyo konde hadi Mungu aliponisaidia katika masomo yangu yangu ya sekondari na uvumilivu wangu ukanifanya nifanye vyema ili niendelee na masomo ya kidato cha tano.

Kuanzia hapo nilipata nafasi ya kurudi kwa bibi ambaye alitamani niendelee na masomo nikiwa karibu yake.

Kutoka hapo Nipo karibu kuhitimu diploma yangu ya Udaktari na nguvu zote ni bibi yangu pekee ambaye hajataka kumpatia majukumu mtu mwingine yoyote ingawaje kipindi hiki nipo masomoni ndio kipindi kigumu cha maisha hata kuafford kandambili ni tatizo sana lakini kikubwa ni bibi anapambana ada inalipwa na kodi ya chumba inalipwa pale inapopatikana.

Baba yangu amekuwa hajaniunga mkono kifedha kwa muda mrefu hata kuna wakati nilisikia ametumia zaidi ya milioni 2 kwa siku kwaajili ya kula kunywa na wanawake nisikumbukwe hata kwa elfu moja.

Ni miezi miwili imebaki nihitimu masomo yangu ya chuo na maandalizi ya kusherehekea mafanikio hayo kutimiza ndoto niliyokua nayo kwa mda mrefu.

Lakini napewa taarifa natakiwa niandike mahitaji yangu yote siku hio ya kusherehekea na baba yangu ambaye anajiandaa na safari kusherehekea pamoja na mimi na ndie atakaegharamikia kila kitu.

Bibi hajahafiki suala hilo ila wazazi walimuambia mimi ni mtu mzima natakiwa kuchagua mimi cha kufanya, bibi kanieleza hatokua msaada katika kusherehekea zaidi anashughulika na deni la ada ninalodaiwa pekee na mama pia hatokua msaada kwakua hana pesa yoyote.

Sina mpango wa kusherehekea mafanikio yangu siku itakapowadia ila nimechanganyikiwa sana na aina hii ya mahusiano ya wazazi hasa baba.

Ningependa kusikia maoni yenu na ushauri juu ya jinsi ya kushughulikia hali hii. Asanteni kwa msaada wenu."
 
Andika hayo mahitaji uliyoambiwa msubiri baba aje msheherekee

Kuhusu kujudge wazazi kutokuwepo kwenye maisha yako tangu una miaka miwili hilo ni la kwako na amani ya moyo wako....fanya unachoona kitakupa amani

Suala la mahusiano(ya mzazi na mtoto) sio la kuingilia sana
 
Andika hayo mahitaji uliyoambiwa msubiri baba aje msheherekee

Kuhusu kujudge wazazi kutokuwepo kwenye maisha yako tangu una miaka miwili hilo ni la kwako na amani ya moyo wako....fanya unachoona kitakupa amani

Suala la mahusiano(ya mzazi na mtoto) sio la kuingilia sana
Umeandika kwa busara sana Joanah. Una undugu na Mama Maria Nyerere? Nimehifadhi comment yangu kwa heshima yako.
 
Dogo piga kitabu umalize shule vizur ukiendelea hivi la sivyo utapigwa disco au wakuhurumie wakupe supp ushindwe kuchomoa wakurudishe mwaka,
Unataka usherekee kumaliza Diploma ya utabibu kwa kipi? safari ya shule bado ni ndefu sherekea ukimaliza MD na sio u CO hayo mambo ya wazazi wako Yako juu ya uwezo wako achana nayo miaka 24 ni mtu mzima jiongeze
 
Mwanaume anawindwa sana.
Akipatikana mwanaume akaharibikiwa, mwanamke ataharibikiwa tu, na watoto wataharibika pia na jamii kwa ujumla haiwez baki salama.

Jiwe la msingi kwa ustawi wa jamii yoyotebile toka ngaz ya familia mpaka taifa ni MWANAUME ma ndio maana program zoote haribifu zinaundwa dunian mpaka sasa ni Dhidi ya WANAUME.

Mungu japo haifahamiki jinsia yake, ila maandiko yanam reffer kama Baba.
 
Mama amekupa msaada ambao sio wa moja kwa moja,,,kwa maana kupitia mama yake ambaye ndio bibi yako amesimamia show nzima pamoja na ankoli,,,shukuru kwa hilo pia

Wamama smtm tuwaelewe tu,,,wanakuwa na mahusiano mengine na kuwafanya washindwe kulea vijana wao kwa kuhofia ndoa kuota mbawa,,,tuwaelewe tu

Ishu ipo kwa mshua,,,baba yako kama ulivyosema ni mtu wa mambo mengi huenda katekwa huko mpaka wewe anakuona takataka,,,lakini msamehe kwa maana matendo yake yasipoteze dira yako


Kama mzee anataka kusimamia show ya sherehe yako,,ikubali huenda ikwawa mwanzo mpya wa kwenda nae sawa,,afterall huna baba mwingine

Kikubwa katika maisha yako mpe kipaumbele sana bibi yako na mfanye afurahie matunda yake.


Gracias
 
Kabla ya kuandika mahitaji,mwambie babaako unadeni la ada bado halijalipwa.Siku zote alikua wapi atake kuja kusherehekea mafanikio asiyopanda mbegu.
 
Beggers can't be choosers,

Wewe weka madeni yako yote tena 3 to 4 times,

Then useme Una receive cash only.

Ukipokea endelea na mambo yako.

Mungu akikusaidia ukawa vzr utajua namna ya kudeal na mambo yako.


Ila kwa sasa hujui mbele yako ikoje, huwez kuchagua unapata wapi msaada
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom